Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kumutumikia Mungu Ndiyo Dawa Yake!

Kumutumikia Mungu Ndiyo Dawa Yake!

Wakati ndugu wawili mapainia walialikwa kuingia katika nyumba fulani huko Kenya, walishangaa kuona mwanaume mudogo akilala juu ya kitanda. Alikuwa na kifua kidogo sana na mikono mifupi. Walipoanza kumuelezea kwamba Mungu anaahidi kwamba “kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya,” mwanaume huyo alianza kuonyesha sura yenye furaha.​—Isa. 35:6.

Mapainia hao waliambiwa kwamba Onesmus, ambaye sasa ana miaka 30 hivi, alizaliwa na ugonjwa unaofanya mifupa iwe zaifu. Mifupa yake ilikuwa zaifu sana hivi kwamba ingeweza kuvunjika kwa urahisi. Kwa kuwa hakuna dawa inayoweza kuponyesha kabisa ugonjwa huo, Onesmus alipaswa kusumbuliwa na maumivu maisha yake yote na alilazimika kutumia kinga ya vilema.

Onesmus alikubali kujifunza Biblia. Lakini, mama yake alikataa asiende kwenye mikutano ya Kikristo, alisema kwamba hilo linaweza kumufanya avunjike na kumuongezea maumivu. Kwa hiyo ndugu walirekodi mikutano ili Onesmus aisikilize akiwa nyumbani. Kisha kujifunza Biblia kwa miezi mitano, Onesmus alisema kwamba alitaka kuhuzuria mikutano ijapokuwa matatizo ambayo angepata.

Je, kuhuzuria mikutano kulimuongezea Onesmus maumivu? Mambo yalikuwa tofauti. Onesmus anasema hivi: “Nilipokuwa kwenye mikutano, nilijisikia kwamba maumivu yangu ya kawaida yalipunguka.” Alifikiri kwamba tumaini ambalo alikuwa amejifunza ndilo lilimusaidia ajisikie muzuri. Mama ya Onesmus alitambua kwamba maoni ya mwana wake yalikuwa yamebadilika na alifurahi sana hivi kwamba naye alikubali kujifunza Biblia. Alisema hivi: “Kumutumikia Mungu ndio dawa ya mwana wangu.”

Kisha muda muchache, Onesmus alikuwa muhubiri asiyebatizwa. Baadaye, alibatizwa na sasa yeye ni mutumishi wa huduma. Ijapokuwa hawezi kutumia miguu na mukono wake mumoja, Onesmus alikuwa na tamaa ya kufanya yote anayoweza katika kazi ya Yehova. Alitaka kuwa painia musaidizi lakini aliogopa kujaza fomu. Sababu gani? Kwa sababu alifikiri kwamba hatapata mutu atakayemusukuma kila siku. Alipoelezea Wakristo wenzake nia yake, waliahidi kumusaidia. Na kwa kweli walimusaidia alipokuwa painia musaidizi.

Onesmus alitamani kuwa painia wa kawaida, lakini aliogopa tena. Hata hivyo, wakati fulani alipata kitia-moyo alichohitaji katika andiko la siku. Andiko la siku hiyo lilikuwa Zaburi 34:8: “Onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema.” Kisha kutafakari juu ya maneno hayo, Onesmus aliamua kuwa painia wa kawaida. Leo anahubiri siku ine kwa juma na anaongoza mafunzo mengi ya Biblia yenye kufanya maendeleo. Katika 2010, alihuzuria Masomo ya Mapainia. Onesmus alifurahia sana kufundishwa na ndugu aliyekuwa mumoja wa ndugu wawili waliomutembelea mara ya kwanza!

Wazazi wa Onesmus wamekwisha kufa, lakini ndugu na dada katika kutaniko wanamutolea mahitaji ya kimwili ya kila siku. Anafurahia sana baraka zote ambazo anapata sasa, na anangojea kwa hamu wakati ambapo “hakutakuwa na mukaaji atakayesema: ‘Mimi ni mugonjwa.’”​—Isa. 33:24.