Namna ya Kuwa na Amani Hata Kama Kuko Vita
Gary mwenye alikuwaka natumika mu kazi ya kijeshi anasema, “Mbele nianze kujifunza Biblia, sikukuwa najua juu ya nini kulikuwa mauaji mingi, kukosa haki, na mivurugo mingi mu dunia. Lakini sasa niko na amani ya akili. Najua kama Yehova atafanya dunia kuwa fasi yenye kuwa salama.”
Haiko tu Gary njo alijisikia vile. Ona namna Biblia imesaidia bengine.
BIBLIA INASEMA: “Wewe, Ee Yehova, uko mwema na uko tayari kusamehe.”—Zaburi 86:5.
NAMNA ILE INASAIDIA: “Hii andiko inanihakikishiaka kama Yehova anasameheaka. Najua kama iko tayari kunisamehe juu ya mambo yote yenye nilifanyaka zamani wakati nilikuwa naenda ku vita.”—Wilmar, Kolombia.
BIBLIA INASEMA: “Ninaumba mbingu mupya na dunia mupya; na mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayataingia katika moyo.”—Isaya 65:17.
NAMNA ILE INASAIDIA: “Juu ya mambo yenye ilinifikia wakati nilikuwa mu jeshi, niko na ugonjwa wa kushuka moyo (dépression) na ugonjwa wenye unafanyaka nihangaike sana. Lakini ile andiko inanikumbushaka kama hivi karibuni Yehova atanisaidia nisahau kabisa ile mambo yote. Sitakuwa tena nabiwaza ao kubitia mu moyo. Ile ni zawadi ya muzuri sana!”—Zafirah, Amerika.
BIBLIA INASEMA: “Katika siku zake mwenye haki atasitawi, na amani itakuwa nyingi mupaka wakati mwezi utakuwa hauko tena.”—Zaburi 72:7.
NAMNA ILE INASAIDIA: “Mara mingi nafikiriaka sana ile maneno. Hivi karibuni, vita na mambo yote ya mubaya yenye inaletaka, bitaisha na hatutakuwa tena nahangaika juu ya usalama ya batu benye tunapendaka.”—Oleksandra, Ikrene.
NAMNA ILE INASAIDIA: “Karibu batu yote ya familia yangu Batutsi balikufa mu mauaji ya génocide. Lakini ile andiko inanihakikishiaka kama nitabaonaka tena. Nachunga sana kwa hamu kusikia masauti yabo saa batafufuliwa!”—Marie, Rwanda.
BIBLIA INASEMA: “Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena. . . Lakini wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”—Zaburi 37:10, 11.
NAMNA ILE INASAIDIA: “Hata vita imalizike batu babaya na kukosa haki, bitakuwa bingali tu. Ile maandiko inanisaidiaka sana. Yehova anaonaka kila kitu na anaelewaka hali yangu. Anaahidi kama hivi karibuni, mateso yote haitakuwa tena na itasahaulika.”—Daler, Tajikistan.
Batu benye bametajwa mu hii gazeti, biko kati ya mamilioni ya Mashahidi wa Yehova, benye Biblia imesaidia kupata amani. Bamejifunza namna ya kupiganisha ubaguzi wa rangi ya ngozi, wa inchi, wa kabila, na hali ya kuchukia bengine. (Efeso 4:31, 32) Mashahidi wa Yehova habajiingizake mu mambo ya politike na banakatalaka kujiingiza mu mambo ya vita.—Yohana 18:36.
Mashahidi wa Yehova wanasaidianaka sawa vile batu ya familia yenye upendo. (Yohana 13:35) Kwa mufano, dada Oleksandra, mwenye tulishataya, alipaswa kuenda kuishi mu inchi ingine na dada yake juu ya kukimbia vita. Anasema hivi: “Kisha tu kuvuka mipaka ya inchi, tuliona mara moya Mashahidi wa Yehova wenye walikuya kutukaribisha. Juu balitusaidia, tuliweza kujipatanisha na hali ya maisha ya mu ile inchi ya mupya hata kama tulikuwa bakimbizi.”
Tunakualika kwa furaha ukuye ku mikutano yetu kwenye utajua mambo mingi juu ya namna ya kuwa na amani leo na kuhusu ahadi ya Mungu juu ya dunia, mwenye mutakuwa amani. utajifunza ujumbe wa Biblia wa amani na namna unaweza kutumikisha mambo yenye utajifunza. Uende ku site yetu jw.org juu ya kupata fasi kwenye mikutano yetu inafanyikaka karibu na kwako, ao juu ya kulomba kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kwa bure kupitia kitabu Furahia Maisha Milele!