Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Namna Gani Ninaweza Kuzungumuza na Wazazi Wangu Juu ya Sheria Zenye Waliweka?

Namna Gani Ninaweza Kuzungumuza na Wazazi Wangu Juu ya Sheria Zenye Waliweka?

 “Wakati nilikuwa na miaka 15, nilikubaliana kabisa na sheria za wazazi wangu, lakini sasa niko na miaka 19 na ninawaza kama niko na lazima ya uhuru zaidi.”​—Sylvia.

 Uko na mawazo kama ya Sylvia? Kama ni vile, habari hii itakusaidia ujue namna unaweza kuzungumuza na wazazi wako juu ya jambo hilo.

 Mambo yenye unapaswa kujua

 Mbele uzungumuze na wazazi wako juu ya sheria zenye waliweka, fikiria mambo hii:

  •  Maisha bila sheria ni muvurugo. Fikiria barabara kubwa yenye magari mingi. Itakuwa namna gani kama hakuna alama katika barabara, hakuna taa za kuongoza magari, na hakuna sheria zenye kuonyesha mwendo wenye magari haipaswe kuvuka? Kama vile sheria za barabara zinasaidia kukuwe utaratibu, sheria za wazazi pia zinasaidia familia ikuwe na utaratibu.

  •  Sheria za wazazi zinaonyesha kama wanakuhangaikia. Kama hawangekuwekea hata sheria moja, ile ingeonyesha kama hawahangaikie mambo yenye inakupata. Kwa kweli, ile ingeonyesha kama hawako wazazi wazuri.

 ULIJUA? Wazazi nao wako na sheria zenye wanapaswa kutii! Kama uko na mashaka, soma Mwanzo 2:24; Kumbukumbu la Torati 6:6, 7; Waefeso 6:4; na 1 Timoteo 5:8.

 Lakini, hata kama unaelewa kwamba sheria ni za lazima, utafanya nini ikiwa unaona kama sheria za wazazi wako hazifae?

 Mambo yenye unaweza kufanya

 Fikiri mbele ya kuzungumuza nao. Unazoea kutii sheria za wazazi wako? Kama haiko vile, pengine haiko njo wakati wa kuwaomba uhuru zaidi. Lakini, ujikaze kwanza kutii sheria zao ili wakutumainie.

 Kama unazoea kutii sheria za wazazi wako, tayarisha mambo yenye ungependa kuwaambia. Kupanga mawazo yako mbele ya wakati kutakusaidia uchunguze ikiwa mambo yenye unaomba inapatana na akili. Kisha, omba wazazi wako wapange wakati na wachague fasi kwenye ninyi wote mutajisikia muzuri kuzungumuza. Halafu, wakati utazungumuza na wazazi wako, kumbuka mambo hii:

 Onyesha heshima. Biblia inasema hivi: “Neno la ukali linachochea hasira.” (Mezali 15:1) Kwa hiyo, usisahau jambo hili: Kama unabishana na wazazi wako ao kuwaambia kama hawako wazazi wazuri, hamutasikilizana.

 “Wakati ninaonyesha wazazi wangu heshima zaidi, nao wananionyesha heshima zaidi. Iko mwepesi zaidi kukubaliana wakati kila mumoja anaheshimia mwenzake.”​—Bianca, iko na miaka 19.

 Usikilize. Biblia inatuambia kama tunapaswa kuwa ‘wepesi wa kusikiliza, hapana wepesi wa kusema.’ (Yakobo 1:19) Kumbuka kama, uko unazungumuza na wazazi wako, lakini hauko unawatolea hotuba.

 “Kadiri tunaendelea kukomaa, tunaweza kuwaza kama tunajua mambo mingi kupita wazazi wetu, lakini haiko vile hata kidogo. Ni muzuri tusikilize mashauri yao.”​—Devan, iko na miaka 20.

 Uwaelewe. Jaribu kuelewa mawazo ya wazazi wako. Fuata shauri la Biblia la ‘kuendelea kuangalia, hapana faida zako wewe mwenyewe tu, lakini pia faida za wengine,’ ni kusema, faida za wazazi wako.​—Wafilipi 2:4.

Unawaza ni njia gani ya kuzungumuza yenye itakusaidia upate uhuru zaidi?

 “Nilizoea kuona wazazi wangu kuwa maadui, kuliko kuwaona kuwa marafiki. Lakini sasa ninatambua kama walikuwa wanajikaza kuwa wazazi wazuri sawa vile mimi pia nilikuwa ninajikaza kuwa mutu muzima. Kila jambo walifanya ni juu walikuwa wananipenda.”​—Joshua, iko na miaka 21.

 Utoe mapendekezo. Kwa mufano, wazia wazazi wako wanakuwekea sheria hii: hawapendi uende ku karamu yenye unapenda kuhuzuria yenye itafanywa mangaribi sana. Jaribu kutafuta ni jambo gani njo linawahangaisha sana, ni saa ya karamu, ao ni karamu yenyewe?

  •   Kama ni saa ya karamu, wanaweza kubadilisha mawazo yao ikiwa unaenda na mutu mwingine?

  •   Kama ni karamu yenyewe, wasiwasi wao unaweza kupunguka ikiwa unawaambia ni watu gani watakuwa kule na ni nani atasimamia ile karamu?

 Usikose kuzungumuza kwa heshima na kusikiliza kwa uvumilivu mambo yenye wazazi wako watapenda kukuambia. Onyesha kama ‘unaheshimia baba yako na mama yako’ kupitia maneno na matendo yako. (Waefeso 6:2, 3) Watabadilisha mawazo yao? Pengine ndiyo. Pengine hapana. Ikuwe wanabadilisha mawazo yao ao hapana, unapaswa kufanya mambo hii . . .

 Kubali kwa heshima uamuzi wa wazazi wako. Hilo ni jambo la maana sana lenye watu wanazarau mara mingi. Kama haupate mambo yenye ulipenda kupata na hivyo unaanza kubishana na wazazi wako, itakuwa nguvu wazazi wako wakupatie uhuru zaidi wakati utazungumuza nao tena. Lakini, kama uko tayari kukubali uamuzi wao, inaonekana kabisa wataregeza sheria fulani zenye waliweka.