Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 16

Watumishi wa Huduma Wanafanyaka Kazi Gani?

Watumishi wa Huduma Wanafanyaka Kazi Gani?

Myanmar

Mugao kwenye mukutano

Kikundi cha mahubiri

Kutunza Jumba la Ufalme

Biblia inazungumuzia vikundi mbili vya wanaume Wakristo wenye wanafanyaka kazi mbalimbali mu kutaniko. Ni “waangalizi [ao, wazee] na watumishi wa huduma.” (Wafilipi 1:1) Kwa kawaida, kila kutaniko linakuwaka na wazee na watumishi wa huduma. Watumishi wa huduma wanafanyaka kazi gani yenye kutuletea faida?

Wanasaidia baraza la wazee. Watumishi wa huduma ni ndugu wenye kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova, ni wenye kutumainika, na ni wenye kuchukua madaraka yao kwa uzito; wamoja kati yao ni vijana na wengine ni watu wazima. Wanafanya kazi mbalimbali za kawaida lakini za lazima mu kutaniko. Hilo linasaidia wazee wakaze akili yao juu ya kazi ya kufundisha na ya uchungaji.

Wanafanya kazi mbalimbali za maana. Watumishi wa huduma fulani wanafanyaka kazi ya kukaribisha watu wote wenye wanakuja ku mikutano. Wengine wanaweza kushugulikia vyombo vya kuongeza sauti, vichapo, visanduku vya michango, na kupatia wahubiri wa kutaniko maeneo ya kuhubiri. Wanasaidia pia kutunza Jumba la Ufalme. Wazee wanaweza kuomba watumishi wa huduma wasaidie ndugu na dada wenye kuzeeka. Watumishi wa huduma wako tayari kufanya kazi yoyote yenye wanapewa, na ndugu na dada wote mu kutaniko wanawaheshimia kwa sababu ya bidii yao.​—1 Timoteo 3:13.

Wanaonyesha mufano muzuri. Ndugu fulani wanawekwa kuwa watumishi wa huduma kwa sababu wanaonyesha sifa za muzuri. Wakati wanafanya migao yao ku mikutano, wanatia nguvu imani yetu. Wao ni mufano muzuri katika mahubiri, kwa hiyo, wanatuchochea tuhubiri kwa bidii. Kwa sababu wanaunga wazee mukono, wanafanya kutaniko likuwe na furaha na umoja. (Waefeso 4:16) Kisha wakati fulani, nao wanaweza kutimiza sifa zenye kuombwa ili kuwa wazee.

  • Watumishi wa huduma ni watu wa namna gani?

  • Watumishi wa huduma wanafanyaka nini ili kusaidia kutaniko?