Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Ibilisi alitoka wapi?

Mungu hakuumba Ibilisi. Lakini, aliumba malaika ambaye baadaye aligeuka kuwa Ibilisi, anayejulikana pia kwa jina Shetani. Yesu alionyesha kwamba wakati fulani Ibilisi hakuwa muongo na hakuwa na kosa. Kwa hiyo, mwanzoni Ibilisi alikuwa malaika muzuri, mwana wa Mungu.​—Soma Yohana 8:44.

Namna gani malaika muzuri angegeuka kuwa Ibilisi?

Malaika aliyegeuka kuwa Ibilisi aliamua kumupinga Mungu na akawachochea mwanaume na mwanamuke wa kwanza wajiunge naye. Kwa hiyo, akajifanya mwenyewe kuwa Shetani, jina linalomaanisha “Mupinzani.”​—Soma Mwanzo 3:1-5; Ufunuo 12:9.

Kama vile viumbe wengine wa Mungu wenye akili, yule malaika aliyegeuka kuwa Ibilisi alikuwa na uhuru wa kuchagua kati ya kufanya mambo yaliyo sawa na mambo yaliyo mabaya, lakini akakomalisha tamaa ya kuabudiwa. Tamaa yake ya kutaka utukufu ilikuwa yenye nguvu zaidi kuliko tamaa yake ya kumupendeza Mungu.​—Soma Mathayo 4:8, 9; Yakobo 1:13, 14.

Namna gani Ibilisi ameendelea kuwashawishi wanadamu? Je, unapaswa kumuogopa? Unaweza kupata majibu kwa maulizo hayo katika Biblia.