Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unabii wa Biblia Haukose Kutimia

Unabii wa Biblia Haukose Kutimia

Unabii wa Biblia Haukose Kutimia

“Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya maneno yote mema ambayo Yehova Mungu wenu amewaambia ninyi.”​—YOSHUA 23:14.

SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Inajulikana sana kama mambo ambayo waaguzi walikuwa wakitabiri hayakuwa hakika na hayangeweza kutumainiwa, ni vilevile juu ya wale wanaotabiri leo matukio ya wakati ujao kwa kuangalia nyota (kama vile mambo ya horoscope). Elimu ya uchunguzi wa mambo yanayowezekana kufanyika wakati ujao kwa kutegemea muelekeo wa wakati wa sasa haiwezi kutabiri bila kukosea matukio fulani ya wakati ujao miaka mingi mbele yatukie. Lakini unabii mbalimbali wa Biblia unaonyesha mambo yote waziwazi na mambo hayo yanatimia kabisa, hata ikiwa unabii unasemea “kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa.”​—Isaya 46:10.

KWA MUFANO: Katika miaka ya 500 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, nabii Danieli alitabiri namna ufalme wa Wamedi na Waperse utakavyoangushwa na ufalme wa Ugiriki (Grèce). Tena, alitabiri kama mufalme wa Ugiriki ‘atakapokuwa mwenye nguvu,’ ufalme wake ‘ungevunjwa.’ Ni nani angechukua nafasi yake? Danieli aliandika hivi: ‘Kuna falme ine zitakazosimama kutoka katika taifa lake, lakini si kwa nguvu zake.’​—Danieli 8:5-8, 20-22.

YALE WANAHISTORIA WANASEMA JUU YA JAMBO HILO: Miaka zaidi ya 200 kisha Danieli kutabiri hivyo, Alexandre le Grand akawa mufalme wa Ugiriki. Katika miaka kumi, Alexandre alishinda ufalme wa Wamedi na Waperse na akapanua ufalme wa Ugiriki mupaka Muto Indus (leo muto huo unapatikana katika Pakistan). Lakini alikufa kwa kushitukia akiwa na miaka 32. Mwishowe, ufalme wake ulivunjwa kabisa kutokana na vita iliyofanyika karibu na Ipsus huko Asia Ndogo. Wale majenerali ine walioshinda katika vita hiyo wakagawanya ufalme wa Ugiriki kati yao. Lakini kati yao hakuna aliyekuwa mwenye nguvu kama Alexandre.

UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine ambacho kilitabiri mambo na yakatokea hivyo bila kukosea? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 4]

Katika kitabu chake (A LAWYER EXAMINES THE BIBLE), IRWIN LINTON alisema hivi: “Unabii wa Biblia uliotimia ni mwingi sana, . . . hatuwezi kuwaza kama ingewezekana utimie kwa bahati tu.”

[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 4]

© Robert Harding Picture Library/SuperStock