Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mapumuziko Mazuri Zaidi Katika Maisha Yangu!

Mapumuziko Mazuri Zaidi Katika Maisha Yangu!

Barua Kutoka Irlande

Mapumuziko Mazuri Zaidi Katika Maisha Yangu!

WAZAZI wangu waliniambia hivi: “Ni vizuri ufanye jambo fulani lenye kupendeza ili ubadilishe mawazo na hilo litakusaidia usiendelee kuhangaikia sana mashindano ya masomo mutakayofanya. Acha tuende kuangalia watoto wa shangazi yako huko Irlande na tuhubirie watu ambao mara nyingi hawapate nafasi ya kusikia habari njema ya Ufalme.”

Mimi sikufurahia wazo hilo. Kwa sababu sikuwa mwenye kujitayarisha vizuri juu ya mashindano na tena niliogopa safari: Ilikuwa mara yangu ya kwanza kutoka katika inchi ya Angleterre na kusafiri kwa avion. Mimi binti wa miaka 17 nilikuwa nimezoea maisha motomoto ya muji mukubwa ulio karibu na Londres, nilijiuliza namna gani ningeishi katika muji mudogo ulio sehemu ya mbali sana huko kusini-mangaribi mwa Irlande.

Lakini sikuwa na sababu ya kuogopa. Wakati tu avion iliyotubeba ilitua, nilivutiwa sana na inchi ya Irlande. Hata hivyo, nilianza kulala kwa sababu asubuhi sana tulianza safari yetu ya motokari. Mara kwa mara, niliamuka na kuona maeneo mazuri lakini yenye majiwe makubwa​-makubwa ambayo ningeweza kuona kupitia barabara ndogo zilizokuwa na kuta zenye majiwe.

Usiku wa kwanza, tulifika katika muji wa Skibbereen na tukapitisha mangaribi nzuri sana na familia moja iliyohamia huko Irlande ili kuendeleza kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Mazungumuzo tuliyokuwa nayo mangaribi hiyo yalikuwa yenye kujenga kiroho. Tulicheza michezo ya Biblia. Kila mutu kati yetu aliokota karatasi iliyo na jina la mutu fulani anayezungumuziwa katika Biblia na kisha alieleza kupitia ishara habari fulani ya maisha ya mutu huyo. Wengine walipaswa kusema mutu huyo ni nani.

Siku iliyofuata, mimi, wazazi wangu, ndugu yangu mudogo, watoto wa shangazi, na familia nyingine tulisafiri kwa mashua ili kwenda kwenye Kisiwa kidogo cha Heir, kilicho na watu karibu 30. Yesu alisema kama habari njema ya Ufalme inapaswa kuhubiriwa katika dunia yote inayokaliwa. Kwa hiyo, tulitumia siku nzima tukizungumuza na watu hao wenye urafiki na wakaribishaji mawazo ya Maandiko yenye kutia moyo na pia tulitazama maeneo mazuri ambayo mwanadamu hajaharibu.

Jua liliangaza katika anga lisilo na mawingu. Maua ya manjano yenye kungaa ya miti ya minazi ilifanya hewa iwe na harufu nzuri na yenye kupendeza. Maua ya wakati wa joto yaliyoanguka kwenye miti yalifunika udongo kama tapi. Sehemu za bahari zilizoingia katika inchi kavu zilituongoza kwenye miteremuko yenye majiwe-majiwe ambako ndege wa baharini walikaa katika chicha zao pamoja na vitoto vyao. Mahali popote, tuliona visiwa vingine vidogovidogo, vingi visivyo na watu, vyote viliitwa kwa jina la Roaringwater Bay. Tulifurahia kabisa maajabu hayo ya uumbaji mbalimbali wa Yehova!

Tuliporudi huko Skibbereen, nilipata marafiki wengi wazuri katika kutaniko ambamo tulifikia na nilijaribu kufanya mambo ambayo nilikuwa sijafanya katika maisha yangu. Jambo ambalo nilifurahia sana mara ya kwanza katika maisha yangu lilikuwa kusafiri ndani ya mutumbwi. Ilifurahisha sana kuona sehemu za Irlande zilizo pembeni ya bahari nikiwa katika mutumbwi! Tulienda kuvua samaki kwa ajili ya chakula cha mangaribi, lakini familia iliyokuja nyuma ilipata samaki mbele yetu. Huko kwenye bahari, tuliunda michezo yetu wenyewe, na hata nilijaribu kucheza dansi ya wakaaji wa Irlande.

Tena, tulitumia muda mufupi ili kujifunza historia ya muji wa Skibbereen. Njaa ilipotokea katika mwaka wa 1840 kwa sababu ya ukosefu wa viazi vya Irlande, njaa ilikuwa kali sana katika muji huo na katika sehemu zake za kandokando. Watu wengi sana walikufa kwa njaa, na watu karibu 9 000 kati yao walizikwa katika kaburi moja. Tulifarijiwa kukumbuka kama, hivi karibuni katika utawala wa Ufalme wa Mungu, hakutakuwa njaa tena, na watu wengi ambao walikufa watafufuliwa na kuishi katika paradiso duniani.

Tulijiunga na Mashahidi wa Yehova wa huko Skibbereen ili kutembelea watu katika maeneo ambayo hayakuhubiriwa mara nyingi. Tulisafiri kwa motokari katika barabara ndogo iliyoteremukia kwenye nyumba zilizojengwa kwenye majiwe pembeni ya bahari ya Irlande. Watu ambao tulikuta huko walikuwa pia wenye urafiki na wakaribishaji. Kama tulivyofanya kwenye Kisiwa cha Heir, tuliwajulisha kwanza watu kama tulikuwa katika mapumuziko na kama tulipenda kupitisha sehemu fulani ya wakati huo ili kuwajulisha ujumbe wa Biblia wenye kuchangamusha moyo.

Mama yangu alizungumuza na mwanamuke mumoja, mwanamuke huyo alikubali magazeti yetu Munara wa Mulinzi na Amkeni! Tulipokutana naye tena baada ya siku chache, alisema kama alifurahia sana mambo aliyosoma katika magazeti hayo.

Mwanamuke huyo alituambia hivi: “Tafazali, mukuje tena kuzungumuza nami na muniletee magazeti mengine.” Tulimuambia kama tulikaribia kurudia katika inchi yetu na kama tutamutumia Shahidi mwengine.

Tena akamuambia mama hivi: “Sawa, lakini ikiwa unakuja tena, usisahau kunitembelea. Na hata kama haurudie haraka, sitakusahau!”

Tulipitisha siku yetu ya mwisho ya mapumuziko pembeni ya bahari pamoja na ndugu na dada wa kutaniko ambamo tulifikia. Tulitengeneza mahali pa kuchomea nyama kwa majiwe na tulitumia kuni ambazo zililetwa na mawimbi ya bahari. Tukapika vitu kama kome (ao escargot) ambavyo tuliookota katika majiwe yaliyoletwa na maji safi sana ya bahari. Nilifurahia sana jambo hilo hata ikiwa nilizaliwa katika muji mukubwa!

Basi, sasa niliwaza nini juu ya mapumuziko hayo ya juma moja huko Irlande? Kwa kweli, hayo yalikuwa mapumuziko mazuri zaidi katika maisha yangu! Hayakuwa tu na mambo mazuri yenye kufurahisha, lakini yalinifanya nitosheke kwa sababu nilifanya jambo fulani lenye kumupendeza Yehova na kumuletea sifa. Ninapenda kumutumikia Mungu wetu, na kwa sababu nina marafiki wazuri na familia inayomupenda pia na inayoniunga mukono, hilo linaniletea furaha hata zaidi. Niliporudia nyumbani, nilimushukuru Yehova kwa sababu amenipatia marafiki wengi wanaonipenda na wanaomupenda Yehova pia. Nilimushukuru pia kwa ajili ya mambo hayo mazuri ambayo nitaendelea kukumbuka katika maisha yangu yote.

[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 25]

Karte Postale, Irlande