Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Hawako Sehemu ya Ulimwengu”

“Hawako Sehemu ya Ulimwengu”

“Hawako Sehemu ya Ulimwengu”

“Ulimwengu umewachukia, kwa sababu hawako sehemu ya ulimwengu.”​—YOHANA 17:14.

Maana Yake Nini?: Juu Yesu hakukuwa sehemu ya ulimwengu, hakujiingiza mu mambo ya watu ao ya politike. Alisema hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu. Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana ili nisitiwe katika mikono ya Wayahudi. Lakini, kwa kweli, Ufalme wangu hautoke katika chanzo hiki.” (Yohana 18:36) Tena aliambia wanafunzi wake waepuke tabia, maneno, na mwenendo wenye Biblia inakataza.​—Matayo 20:25-27.

Wakristo wa Kwanza-kwanza Walifanya Vile Namna Gani?: Jonathan Dymond, mwandishi wa mambo ya dini, alionyesha kama Wakristo wa kwanza-kwanza “walikatala kujiingiza mu mambo ya [vita]; hata kama ile ingefanya watukanwe, wafungwe, ao kuuawa.” Walichagula kuteseka kuliko kujiingiza mu mambo ya politike ao ya vita. Zaidi ya ile, mwenendo wao ulifanya wakuwe tofauti na watu wengine. Wakristo waliambiwa hivi: “Kwa sababu hamuendelee kukimbia pamoja nao katika mwendo uleule mubaya sana wa upotovu, basi wanawatukana ninyi.” (1 Petro 4:4) Mwanahistoria Will Durant aliandika kama juu walikuwa na mwenendo muzuri na walimuogopa Mungu, ile “ilisumbua wapagani wenye kupenda raha.”

Nani Njo Wako Nafanya Vile Leo?: Kuhusu musimamo wa Wakristo wa kutounga mukono upande wowote, kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema hivi: “Ni mubaya kukatala kujiingiza mu vita juu ya zamiri.” Gazeti Reformierte Presse ilizungumuzia ripoti yenye ilitolewa na shirika fulani ya haki za kibinadamu yenye kuitwa African Rights. Ile ripoti, yenye ilizungumuzia mauaji yenye ilifanyika Rwanda mu mwaka 1994, ilionyesha kama dini zote zilishiriki mu ile mauaji “isipokuwa tu Mashahidi wa Yehova.”

Wakati alikuwa anazungumuzia mauaji makubwa ya Wayahudi, mwalimu fulani wa segondere alisema hivi kwa huzuni: “Hakuna kikundi ya watu ao tengenezo yenye ilipinga mambo ya uongo, matendo ya bila huruma, na mateso makali yenye ilifuata.” Kisha kutafuta habari ku jumba ya makumbusho ya Amerika kuhusu mauaji makubwa ya Wayahudi, aliandika hivi: “Sasa nimepata jibu.” Alivumbula kama Mashahidi wa Yehova hawakuacha imani yao hata kama walitendewa mubaya sana.

Tuseme nini juu ya mwenendo wao? Gazeti Catholic U.S. inasema kama leo vijana wengi Wakatoliki hawakubaliane na mambo yenye kanisa inasema kuhusu kuishi pamoja bila kufunga ndoa na kufanya ngono mbele ya kufunga ndoa. Ile gazeti inarudilia maneno ya mutumishi fulani wa kanisa, mwenye alisema hivi: “Ninaonaka kama watu wengi, naweza hata kusema zaidi ya nusu ya watu wenye wanakuyaka kufunga ndoa mu kanisa, wanakuwaka walishaanza kuishi pamoja.” Kitabu The New Encyclopedia Britannica inaonyesha kama Mashahidi wa Yehova “wanakaziaka kama ni jambo ya maana sana kufuata kanuni za mwenendo mu maisha ya kila siku.”