Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MALAIKA​—WAKO KABISA? SABABU GANI TUFIKIRIE JAMBO HILO?

Malaika​—Wanatimiza Jambo Fulani Katika Maisha Yako?

Malaika​—Wanatimiza Jambo Fulani Katika Maisha Yako?

Siku ya Yenga moja kisha midi, Kenneth na Filomena, wenye wanaishi Curaçao, walitembelea bibi na bwana fulani wenye walikuwa wanajifunza nao Biblia.

Kenneth anasema hivi: “Wakati tulifika, mulango wa nyumba ulikuwa wenye kufungwa na hakukuwa motokari. Lakini jambo fulani lilinichochea kuita namba ya telefone ya mwanamuke.”

Mwanamuke huyo alijibu na kuonyesha kwamba bwana yake alikuwa kwenye kazi. Lakini, wakati tu alitambua kama Kenneth na Filomena walikuwa inje, alikuja kwenye mulango na kuwakaribisha ndani.

Mara moja walitambua kwamba mwanamuke huyo alikuwa analia. Wakati Kenneth alianza funzo la Biblia kwa sala, mwanamuke huyo alianza tena kulia. Kwa hiyo, kwa upole Kenneth na Filomena walimuuliza nini haikuendeka.

Mwanamuke huyo alionyesha kwamba alikuwa anapanga kujiua siku hiyo kisha midi, na alikuwa anaandika barua kwa bwana yake ili kuonyesha sababu yake ya kujiua wakati Kenneth alimuita kwenye telefone, na akaacha kufanya hivyo. Aliwaambia kwamba alikuwa mwenye kushuka moyo, kwa hiyo wakasoma naye maandiko fulani ya Biblia yenye kutia moyo. Kitia-moyo hicho kiliokoa uzima wake.

Kenneth anasema hivi: “Tulimushukuru Yehova kwa kutupatia nafasi ya kumusaidia mwanamuke huyo mwenye kushuka moyo na zaidi sana kwa kutuongoza​—pengine kupitia malaika ao roho yake takatifu​—ili kuita mwanamuke huyo!” *

Kenneth na Filomena wako na sababu nzuri ya kuamini kwamba Mungu aliingilia kati, ikuwe kupitia malaika ao roho yake takatifu, ni kusema, nguvu yake ya utendaji? Ao ilikuwa bahati tu kuita kwa wakati huo wenye kufaa?

Hatuwezi kuhakikisha jambo lolote. Lakini jambo lenye tunajua ni kwamba, Mungu anatumia malaika zake ili kusaidia watu kiroho. Kwa mufano, Biblia inasema kwamba Mungu alitumia malaika ili kuongoza Filipo, mweneza-injili Mukristo, ili kusaidia ofisa mumoja Mwethiopia mwenye alikuwa anatafuta muongozo wa kiroho.​—Matendo 8:26-31.

Dini nyingi zinafundisha imani katika viumbe wa roho ambao wamoja wanaonyeshwa kuwa viumbe wema wenye kutimiza mapenzi ya Mungu ao kutumika kama walinzi wa watu. Watu wengi hawaamini tu kwamba malaika wako lakini wanaamini pia kwamba roho hao wanaweza kuwafanyia jambo fulani katika njia fulani ya maana. Lakini, watu wengine wengi hawana imani yoyote katika malaika.

Malaika wako kabisa? Kama malaika wako, walitoka wapi? Biblia inafundisha nini kuhusu malaika? Wanaweza kutimiza jambo fulani katika maisha yako? Acha tuchunguze ushuhuda fulani kuhusu malaika.

^ fu. 8 Yehova ni jina la Mungu kama vile inaonyeshwa katika Biblia.​—Zaburi 83:18.