Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

Italia

Katika mwaka wa 2011 huko Italia, hesabu ya baiskeli ao kinga ambazo ziliuzishwa ilipita hesabu ya motokari. Kati ya sababu ambazo zilitolewa kuna sababu hizi: matatizo ya kifeza, kupanda kwa bei ya mafuta ya motokari, na feza za kuendelea kulinda motokari iwe katika hali nzuri. Lakini, kinga haziombe feza nyingi ili kuendelea kuzilinda katika hali nzuri, ni rahisi kutumia, na zinafaa.

Armenia

Mahakama ya Ulaya ya Haki za Binadamu imetoa uamuzi kwamba serikali ya Armenia ilivunja haki za vijana wanaume 17, Mashahidi wa Yehova, ambao walifungwa kwa sababu walikataa kufanya utumishi wa kiraia ambao unaongozwa na wakubwa wa jeshi. Serikali iliombwa kuwalipa wale vijana 17 feza kwa sababu ya mambo mabaya ambayo walitendewa na kuwalipa garama za kisheria.

Japani

Kati ya watoto ambao walitendewa vibaya kupitia adresi za kupashana habari kwenye Internete, watoto 63 juu ya 100 hawakuonywa na wazazi wao kuhusu hatari ambazo zingeweza kuwapata. Kati ya watu 599 waliotendea watoto vibaya ambao walichunguzwa, watu 74 juu ya 100 walikubali kwamba kusudi lao la kutumia adresi hizo lilikuwa kufanya ngono na watoto wadogo.

China

Ili kujikaza kupunguza musongamano wa motokari katika barabara, miji mikubwa inapunguza kupana vikaratasi vya uandikishaji wa motokari za mupya. Kwa mufano, katika muji wa Beijing hawakubali kupana vikaratasi vya motokari zaidi ya 240 000 kwa mwaka. Katika Mwezi wa 8, 2012, watu 1 050 000 hivi walicheza muchezo wa feza na kati yao watu 19 926 walipewa vikaratasi vya kukubaliwa kuendesha motokari, hilo linamaanisha kwamba, kati ya watu 53 waliocheza, ni mutu 1 tu ndiye aliweza.