Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Wakati Urafiki Unakuwa wa Nguvu Sana

Wakati Urafiki Unakuwa wa Nguvu Sana

TATIZO

Una rafiki mwanamuke ao mwanaume ambaye anakuelewa vizuri kabisa. Ninyi wawili munaweza kuongea kila kitu, na munaongea kabisa. Unajiambia, ‘Tuko tu marafiki,’ hata ikiwa bibi ao bwana yako anaweza kuwa na mawazo tofauti ikiwa haumuingize katika mazungumuzo yenu marefu.

Inaonekana kwamba urafiki wenu umekuwa wa nguvu sana na ni lazima kubadilisha hali hiyo. Hata hivyo, fikiria kwanza ni nini labda ilikufanya uijiingize katika urafiki kama huo.

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

Kutafuta kutimiziwa mahitaji yako ya moyoni. Kwa kifupi, mutu anajisikia vizuri wakati mwanaume ao mwanamuke mwengine anavutiwa na yeye. Tunapendezwa tunapojua kwamba tunaonwa kuwa watu wa maana na jambo hilo linatufanya tujisikie kuwa wenye kuvutia. Kisha kufunga ndoa kwa muda fulani, unaweza kuanza kujisikia salama unapokuwa na mutu mwengine asiyekuwa bibi ao bwana yako. Lakini jua jambo hili: Kutimiziwa mahitaji hayo na mutu ambaye si bibi ao bwana yako kunaleta matokeo mabaya. Unapokuwa na uhusiano usiofaa pamoja na mutu ambaye si bibi ao bwana yako, unafanya uhusiano pamoja na bibi ao bwana yako uwe zaifu. Katika njia fulani, unamuiba bibi ao bwana yako upendo ambao unapaswa kumuonyesha.

• Ujiulize, ‘Ni mahitaji gani ambayo urafiki huu unanitimizia ambayo yangetimizwa vizuri katika ndoa yangu?’

Unaweza kuvutiwa kwa vyepesi na mutu mwengine kwa sababu ya matatizo ya ndoa yako. Biblia inasema kwamba wale wenye kufunga ndoa watakuwa na ‘ziki’ kwa kadiri fulani. (1 Wakorintho 7:28) Kwa mufano, wakati fulani unaweza kujisikia kuwa bibi ao bwana yako anakupuuza ao hakuone kuwa wa maana, ao unaweza kuwa na kinyongo sababu ya tatizo fulani ambalo halitatuliwe. Labda bibi ao bwana yako anaepuka kuzungumuzia matatizo hayo, na hivyo kukufanya uwe mwenye kuvunjika moyo na kwa sababu hiyo unaweza kuvutiwa kwa vyepesi na mutu mwengine. Watu fulani wenye elimu wanasema kwamba kuepuka kuzungumuzia matatizo ya ndoa kunaweza kumufanya mutu akose furaha katika ndoa, na hata kufanya ndoa ivunjike.

• Ujiulize, ‘Nina tatizo fulani katika ndoa yangu ambalo limenifanya niwe na urafiki usiofaa na mutu mwengine asiyekuwa bibi ao bwana yangu?’

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Utambue hatari. Biblia inasema hivi: ‘Je, mutu anaweza kukusanya moto kifuani pake na mavazi yake yasiungue?’ (Methali 6:27) Kwa kweli, ni vibaya sana kufanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwengine wakati ambapo tayari umefunga ndoa na mutu fulani. (Yakobo 1:14, 15) Hapa hatuzungumuzie mambo ambayo labda yanaweza kutokea. Lakini tunazungumuzia mambo ambayo tayari yamekwisha kutokea. Kwa kuvutiwa na mutu mwengine ambaye si bibi ao bwana yako, unaiba bibi ao bwana yako uangalifu ambao unapaswa kumuonyesha.

Acha kuwazia​-wazia mambo yasiyo ya kweli. Urafiki wa nguvu na mutu fulani unaweza kukufanya uanze kuwazia​-wazia ikiwa maisha yako yangekuwa namna gani kama ungefunga ndoa na mutu huyo. Hata hivyo, si jambo linalofaa kulinganisha uwezo wa rafiki yako na uzaifu wa bibi ao bwana yako. Kumbuka pia kwamba namna unavyochangamuka kwa furaha unapofikiri juu ya rafiki yako ni hivyo ulijisikia pia ulipoanza urafiki pamoja na mutu ambaye ulioa ao kuolewa naye.​—Kanuni ya Biblia: Yeremia 17:9.

Jitilie mipaka. Watu wanatia chombo kinachotoa mulio katika motokari yao ao katika nyumba yao ili kuzuia watu wanaoiba. Unaweza kufanya jambo lenye kufanana na hilo kwa ajili ya ndoa yako. Biblia inasema hivi: “Linda moyo wako.” (Methali 4:23) Unaweza kufanya hivyo namna gani? Jaribu kufanya mambo yanayofuata:

  • Onyesha waziwazi kwamba umekwisha kufanya agano la ndoa, kwa mufano kwa kuweka picha za bibi ao bwana yako nafasi yako ya kazi.​—Kanuni ya Biblia: Mwanzo 2:24.

  • Amua ni mambo gani ambayo unaweza ao hauwezi kuruhusu mutu ambaye si bibi ao bwana yako afanye. Kwa mufano, haitakuwa vizuri kabisa kumuelezea rafiki huyo matatizo ya ndoa yako ao kuenda kunywa pombe pamoja na mufanyakazi mwenzako asiyekuwa bibi ao bwana yako.

  • Ikiwa unakuwa na urafiki wa nguvu na mutu ambaye si bibi ao bwana yako, achana na urafiki huo. Ikiwa inaonekana kuwa vigumu kwako kukatiza urafiki huo, ujiulize ni sababu gani. Kuliko kutetea urafiki huo, unga mukono bibi ao bwana yako na uchukue hatua za kulinda ndoa yako.​—Kanuni ya Biblia: Methali 5:18, 19.