Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
MUNARA WA MULINZI
Ulizo: Malaika wako kabisa?
Andiko: Zab 103:20
Namna ya kutoa: Munara wa Mulinzi huu unaonyesha mambo Biblia inasema kuhusu malaika na mambo wanatimiza leo katika maisha yetu.
FUNDISHA KWELI
Ulizo: Unawaza kama sayansi imepinga Biblia?
Andiko: Isa 40:22
Kweli: Wakati Biblia inazungumuzia mambo ya sanyasi haiseme uongo.
MUALIKO KWA AJILI YA MIKUTANO YA KUTANIKO (inv)
Namna ya kutoa: Napenda kukualika kwenye hotuba yenye kutegemea Biblia. Itatolewa kwenye Jumba la Ufalme, kwenye tunafanyiaka ibada. [Umuachie mutu mualiko, umuonyeshe mahali na saa, na umuambie kichwa cha hotuba.]
Ulizo: Ulishaka fika kwenye Jumba la Ufalme? [Kama inawezekana, umuonyeshe mutu video Kwa Kawaida Tunafanya Nini Kwenye Jumba la Ufalme?]
ANDIKA NAMNA UNAWEZA PIA KUANZISHA MAZUNGUMUZO
Fuata mufano wenye kuwa hapo juu ili kuandika namna yako ya kuanzisha mazungumuzo.