Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Juu ya Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Jibu ya Biblia

 Mara mingi Biblia inaita Yesu “Mwana wa Mungu.” (Yohana 1:49) Maneno “Mwana wa Mungu” inaonyesha kama Mungu njo aliumba vitu vyote vyenye uzima, na hata Yesu. (Zaburi 36:9; Ufunuo 4:11) Biblia haifundishe kama Mungu alizalaka Yesu sawa vile baba wanadamu wanazalaka watoto.

 Biblia inaita malaika pia kuwa “wana wa Mungu wa kweli.” (Yobu 1:6) Na Biblia inasema kama mwanadamu wa kwanza, ni kusema, Adamu, alikuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Biblia inaita Yesu Mwana wa pekee wa Mungu juu yeye njo Mungu aliumbaka mbele aumbe vitu vingine vyote, na yeye tu njo Mungu aliumbaka moja kwa moja.

 Yesu aliishi mbinguni mbele azaliwe ku dunia?

 Ndiyo. Yesu alikuwa kiumbe wa roho mbinguni mbele azaliwe hapa ku dunia. Yesu yeye peke alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni.”​—Yohana 6:38; 8:23.

 Mungu aliumba Yesu mbele aumbe kitu ingine yoyote. Biblia inasema hivi juu ya Yesu:

  •   “Yeye ni . . . muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.”​—Wakolosai 1:15.

  •   Yeye ni “mwanzo wa uumbaji wa Mungu.”​—Ufunuo 3:14.

 Yesu alitimiza unabii wenye kuzungumuzia ule mwenye “asili yake ni ya kuanzia nyakati za zamani, kuanzia siku za zamani sana.”​—Mika 5:2; Matayo 2:4-6.

 Yesu alikuwa nafanya nini mbele akuye ku dunia?

 Alikuwa na cheo ya juu mbinguni. Yesu alizungumuzia cheo yenye alikuwa nayo wakati alisali hivi: “Baba, unitukuze . . . kwa utukufu wenye nilikuwa nao pembeni yako mbele ya ulimwengu kuwa.”​—Yohana 17:5.

 Alisaidia Baba yake kuumba vitu vingine vyote. Yesu alitumika na Mungu ‘akiwa fundi wa kazi.’ (Mezali 8:30) Biblia inasema hivi juu ya Yesu: “Kupitia yeye vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani.”​—Wakolosai 1:16.

 Mungu alimutumia Yesu juu ya kuumba vitu vingine vyote. Kwa mufano, alimutumia juu ya kuumba viumbe vya roho, na ulimwengu. (Ufunuo 5:11) Tunaweza kusema kama Mungu alitumika pamoya na Yesu sawa vile mutu mwenye kufanya plani ya majengo anatumikaka na mujenzi. Mutu mwenye kufanya plani, analetaka plani, kisha mujenzi anaitumia juu ya kujenga.

 Alikuwa Neno. Wakati Biblia inazungumuzia maisha ya Yesu mbele akuwe mwanadamu, inamuita “Neno.” (Yohana 1:1) Ni kusema, Mungu alikuwa namutumia juu ya kujulisha viumbe vingine vya roho habari fulani na maagizo yake.

 Inaonekana pia kama Mungu alikuwa natumia Yesu juu ya kujulisha wanadamu ku dunia habari fulani na maagizo yake. Inawezekana Mungu alimutumia Yesu juu ya kujulisha Adamu na Eva maagizo yake mu bustani ya Edeni. (Mwanzo 2:16, 17) Inawezekana Yesu njo ule malaika mwenye aliongozaka Waisraeli wa zamani mu jangwa na mwenye Waisraeli walipaswa kutii kabisa.​—Kutoka 23:20-23. *

^ Haiko Neno tu njo malaika mwenye Mungu alikuwa natumia juu ya kufikishia viumbe vyake habari fulani na maagizo yake. Kwa mufano, alitumia malaika wengine juu ya kupatia Waisraeli wa zamani Sheria.​—Matendo 7:53; Wagalatia 3:19; Waebrania 2:2, 3.