Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Mashahidi wa Yehova Wanahubiri Nyumba kwa Nyumba?

Sababu Gani Mashahidi wa Yehova Wanahubiri Nyumba kwa Nyumba?

 Yesu aliwaagiza wafuasi wake ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mathayo 28:19, 20) Alipowatuma wafuasi wake wa kwanza-kwanza, Yesu aliwaagiza waende kuhubiri katika nyumba za watu. (Mathayo 10:7, 11-13) Kisha kifo cha Yesu, Wakristo wa kwanza-kwanza waliendelea kueneza ujumbe wao ‘hazarani na nyumba kwa nyumba.’ (Matendo 5:42; 20:20) Tunaiga Wakristo hao na tunatambua kwamba kuhubiri nyumba kwa nyumba ni njia nzuri ya kuwapata watu.