Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 5

Garika Kubwa​—Ni Nani Walimusikiliza Mungu? Ni Nani Hawakumusikiliza?

Garika Kubwa​—Ni Nani Walimusikiliza Mungu? Ni Nani Hawakumusikiliza?

Watu wengi wenye waliishi wakati wa Noa walikuwa wanafanya mambo ya mubaya. Mwanzo 6:5

Adamu na Eva walizaa watoto, na watu wakakuwa wengi ku dunia. Kisha wakati fulani, malaika fulani walijitia ngambo ya Shetani, ili kumupinga Mungu.

Walikuja ku dunia, wakavaa miili ya watu ili waweze kuoa wanamuke. Wale wanamuke walizaa watoto wenye walikuwa na nguvu mingi kupita watu wengine na walikuwa wabaya sana.

Ku dunia kulijaa watu wenye walikuwa wanafanya mambo ya mubaya. Biblia inasema hivi: “Uovu wa mwanadamu ulikuwa mwingi juu ya dunia na kila muelekeo wa mawazo ya moyo wake ulikuwa tu mubaya wakati wote.”

Noa alimusikiliza Mungu na akajenga safina. Mwanzo 6:​13, 14, 18, 19, 22

Noa alikuwa mutu muzuri. Yehova alimuambia kama ataua watu wabaya kwa kutumia garika kubwa (mvua ya mingi sana).

Tena Mungu alimuambia Noa ajenge mashua kubwa sana; mashua hiyo iliitwa safina. Na alimuambia aingize ndani ya mashua hiyo, familia yake na kila namna ya munyama.

Noa alitolea watu angalisho juu ya Garika yenye ilikuwa karibu kuja, lakini hawakumusikiliza. Watu fulani walimuchekelea Noa na wengine walimuchukia.

Wakati Noa alimaliza kujenga safina, aliingiza wanyama ndani.