Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | MAMBO YENYE MUNGU AMEKUFANYIA

Tukio Ambalo Haupaswi Kukosa

Tukio Ambalo Haupaswi Kukosa

Usiku, mbele ya kutoa uzima wake, Yesu aliwaagiza wanafunzi wake waaminifu wakumbuke, ao kuazimisha, zabihu yake ya ukombozi. Akitumia mukate usiotiwa chachu na divai nyekundu mbele yao, alianzisha kile kinachoitwa Chakula cha Jioni cha Bwana na akawaagiza hivi: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”​—Luka 22:19.

Kila mwaka, Mashahidi wa Yehova katika dunia yote wanakutana ili kukumbuka kifo cha Yesu. Katika mwaka huu wa 2014, Ukumbusho huo utafanywa Siku ya Kwanza, tarehe 14 Mwezi wa 4 kisha jua kushuka.

Tunafurahi kukualika uje kukusanyika pamoja na sisi ili kusikiliza habari itakayoeleza zaidi maana ya zabihu ya ukombozi ya kifo cha Yesu. Kwenye mukutano huo watu hawaombwe watoe feza ao sadaka. Mutu aliyekupatia gazeti hili atakuambia wakati na mahali ambapo Ukumbusho huo utafanywa katika eneo lenu ao unaweza kufungua adresi yetu ya Internete, jw.org. Tafazali, unaweza kuandika tarehe ya tukio hilo, ambalo tunatumaini kuwa hautakosa.