Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuwa Pamoja na Watu wa Jamaa

Kuwa Pamoja na Watu wa Jamaa

Kuwa Pamoja na Watu wa Jamaa

“Tazama! Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza ndugu kukaa pamoja kwa umoja!”​—ZABURI 133:1.

Sababu inayowafanya watu wengine wafanye sikukuu ya Noeli.

Waisraeli wote walikuwa “ndugu,” watu wa familia moja, kwa sababu walitokana na mutu mumoja, ni kusema, Yakobo ao Israeli. Walipokusanyika kwa ajili ya sikukuu huko Yerusalemu, hilo lilikuwa jambo ‘njema’ na lenye ‘kupendeza.’ Kama wao, familia nyingi leo zinaona kuwa ni jambo ‘njema’ na lenye ‘kupendeza’ kukutana pamoja wakati wa Noeli.

Je, hiyo ni sababu yenye kufaa?

Kitabu kimoja (Encyclopedia of Christmas and New Year’s Celebrations) kinasema hivi: “Matatizo madogo ambayo watu wa jamaa wamekuwa nayo kwa muda wa mwaka muzima, wanaweza kuyafanya kuwa makubwa sana wanapokutana pamoja wakati huo wa sikukuu.”

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutusaidia?

‘Endelea kuwalipa wazazi wako na wazazi wa wazazi wako.’ (1 Timotheo 5:4) Panga kuwatembelea mara kwa mara watu wa jamaa yako, kadiri unavyoweza. Ikiwa watu wa jamaa yako wanaishi mbali, unaweza kupashana nao habari kwa ukawaida. Unaweza kuwaandikia barua, kuwaita kupitia telefone, kuwatumia ujumbe ao kuongea nao kupitia Internete. Kupashana habari kwa ukawaida kunapunguza kutoelewana.

‘Mumesongwa mukakosa nafasi katika upendo wenu muororo. . . . Panukeni.’ (2 Wakorintho 6:12, 13) Watu wa jamaa ambao tunaonana nao mara moja tu kwa mwaka wanaweza kuonekana kama wageni, zaidi sana kwa watoto. Watoto fulani wanajisikia kuwa hawana uhusiano wowote na wazazi wa wazazi wao ao watu wengine wa jamaa. Kwa hiyo, uwatie watoto wako moyo ‘wapanuke’ katika upendo wao kwa kuwaalika nyumbani watu wa jamaa waliozeeka. * Watoto wanaopitisha wakati mara kwa mara pamoja na watu wa jamaa waliozeeka wanakuwa wenye huruma na upendo zaidi kuelekea watu walio na umri mukubwa kuliko wao.

‘Neno linalosemwa wakati unaofaa ni njema kama nini!’ (Methali 15:23) Namna gani unaweza kuzuia kutoelewana ao matatizo yasiharibu uhusiano wa jamaa? Njia moja ni kuchagua “wakati unaofaa” ili kuzungumuzia matatizo yenye kufaa. Ikiwa munapashana habari kwa ukawaida, utaona kama ni vyepesi kuendea kipekee watu wa jamaa ili kutatua tatizo lolote na hivyo mutaona kuwa ni jambo ‘njema’ na lenye ‘kupendeza’ munapokutana pamoja.

[Maelezo ya chini]

^ Soma habari yenye kichwa “Kwa Nini Niwajue Vyema Babu na Nyanya?” na “Ninawezaje Kusitawisha Uhusiano wa Karibu Pamoja na Babu na Nyanya?” katika Amkeni! ya tarehe 22 Mwezi wa 4, 2001 na Amkeni! ya tarehe 22 Mwezi wa 5, 2001, zilizochapishwa na Mashahidi wa Yehova.