MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 10, 2014

Gazeti hili lina habari za kujifunza za tarehe 1 mupaka tarehe 28 Mwezi wa 12, 2014.

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika Taïwan

Ndugu na dada zaidi ya 100 wa inchi mbalimbali wamehamia katika inchi ya Taïwan ili kutumikia katika maeneo iliyo na lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Tafuta kujua mambo ambayo walikutana nayo na pia kile kiliwasaidia kupata matokeo mazuri.

Ukuwe na Imani Yenye Nguvu Katika Ufalme

Yehova alitumia maagano sita ili kutuhakikishia kwamba Ufalme wake utatimiza kusudi lake. Namna gani maagano hayo yanaweza kutusaidia kuwa na imani yenye nguvu?

Mutakuwa “Ufalme wa Makuhani”

Maagano tatu ya mwisho kati ya maagano sita ambayo tumezungumuzia yanaweza kutusaidia tukuwe na imani yenye nguvu katika Ufalme wa Mungu na inaweza kutuchochea kuhubiria wengine habari njema ya Ufalme huo.

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Matukio ya Maana Sana Katika Utumishi Wangu

Mildred Olson ametumikia Yehova zaidi ya miaka 75, kutia ndani miaka 29 ambayo alifanya katika kazi ya umisionere katika El Salvador. Ni nini inamusaidia aendelee kujisikia kama kijana katika moyo wake?

Furahia Pendeleo Lako la Kutumika Pamoja na Yehova

Sababu gani waabudu wa Yehova wako tayari kutia pembeni faida zao fulani?

‘Muendelee Kukaza Akili Zenu juu ya Mambo Yaliyo juu’

Sababu gani watu walio na tumaini la kuishi milele duniani wanakaza akili zao juu ya mambo yaliyo juu? Namna gani wanaweza kufanya hivyo?