Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | BIBLIA ILIOKOKA NAMNA GANI?

Historia ya Maana

Historia ya Maana

Hakuna kitabu kingine cha dini chenye kuwa kama Biblia. Hakuna kitabu kingine chenye watu wengi wametumia sana katika mafundisho yao kwa muda murefu kama Biblia. Tena, hakuna kitabu kingine chenye kimechunguzwa kwa uangalifu sana na kuchambuliwa kama Biblia.

Kwa mufano, wachunguzi fulani hawako hakika kwamba Biblia za leo ni kopi zenye kutegemeka za maandishi ya kwanza. Profesa mumoja mwenye kufundisha mambo ya dini anasema hivi: “Hatuwezi kuwa hakika kwamba tumepata kopi za maandishi ya kwanza zenye hazina makosa. Tuko na kopi zenye kujaa makosa, na kopi nyingi kati ya kopi hizo zimeandikwa mamia ya miaka kisha maandishi ya kwanza, na maandishi ya kopi hizo yako tofauti na maandishi ya kwanza katika njia nyingi.”

Wengine wako na mashaka juu ya Biblia kwa sababu ya mambo yenye wamefundishwa katika dini zao. Kwa mufano, Faizal alifundishwa katika familia yake yenye haiko ya Kikristo kwamba Biblia ni kitabu kitakatifu, lakini imebadilishwa. Anasema hivi: “Kwa hiyo, nilikuwa na mashaka fulani wakati watu walitaka kuzungumuza na mimi juu ya Biblia. Tena, hawakuwa na Biblia yenye kuwa na maandishi ya kwanza. Ilibadilishwa na watu!”

Ni jambo la lazima kujua kwamba Biblia imebadilishwa hao hapana? Tufikirie maulizo yenye kufuata: Unaweza kutumainia ahadi za Biblia zenye kufariji juu ya wakati wenye kuja ikiwa haujue kama ahadi hizo zilikuwa katika maandishi ya kwanza? (Waroma 15:⁠4) Unaweza kutumia Biblia ili kukamata maamuzi makubwa juu ya kazi, familia, ao ibada kama Biblia za leo ni kopi zenye makosa ambazo ziliandikwa na wanadamu?

Hata kama hatuna tena vitabu vya kwanza vya Biblia, tunaweza kuchunguza kopi za zamani. Kati ya kopi hizo, kuna maelfu ya kopi za maandishi ya Biblia. Namna gani maandishi hayo yaliokoka hatari ya kuharibika, upinzani, na hatari ya kutaka kubadilisha ujumbe wa Biblia? Namna gani kuokoka kwa maandishi hayo kunaweza kukusaidia ukuwe hakika kabisa kwamba Biblia ya leo yenye unaweza kupata ni ya kweli? Uchunguze majibu ya maulizo hayo katika habari zenye kufuata ambazo zinaonyesha namna Biblia iliokoka.