Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Ni Mubaya Kupatia Mutoto Malipizi?

Ni Mubaya Kupatia Mutoto Malipizi?

Katika miaka fulani iliyopita, maisha ya familia yamebadilika sana katika inchi za Mangaribi. Wakati fulani wazazi ndio walikuwa wanaongoza na watoto walifuata muongozo wa wazazi. Lakini, sasa katika familia fulani ni watoto ndio wanaongoza na wazazi wanafuata muongozo wa watoto. Kwa mufano, fikiria hali tatu zenye kufuata. Kila hali inaonyesha mambo yenye yanatokea mara nyingi.

  • Mutoto mumoja mwanaume mwenye miaka ine iko na mama yake katika duka. Mutoto huyo anataka kukamata kitu fulani cha kuchezea lakini mama yake anajaribu kumukataza. Anamuambia hivi: “Uko na vitu vingi vya kuchezea, sivyo?” Lakini, hakuna tena cha kufanya, mama anatambua kama hangepaswa kumalizia na ulizo. Mutoto analia na kusema, “Lakini ninaitaka.” Mama anaogopa kama mutoto atalalamika kwa hasira kama vile anafanya kila mara, kwa hiyo anamununulia kitu hicho cha kuchezea.

  • Mutoto mumoja mwanamuke mwenye miaka tano anamukatiza baba yake mwenye kuzungumuza na mutu mwengine mukubwa. Anasema hivi: “Nimechoka, ninataka kuenda nyumbani!” Baba anainama kumuelekea, na kumuambia hivi kwa sauti ya kubembeleza: “Uchunge zingine dakika kidogo tu, sawa?”

  • James mwenye miaka 12 ameshitakiwa tena kuwa alimufokea mwalimu wake. Baba ya James anakasirika; hamukasirikie mutoto wake lakini anamukasirikia mwalimu. Anamwambia James hivi: “Anakusumbua kila mara. Nitamushitaki kwa wakubwa wa masomo yenu!”

Mifano hiyo ni ya kutunga tu, lakini inaonyesha mambo yenye yanafanyika mara nyingi. Inaonyesha matatizo ya kweli yenye kuwa katika familia ambamo wazazi wanavumilia tabia ya kukosa adabu ya watoto, wanawapatia kila kitu wanaomba, na “kuwalinda” ili wasipate matokeo ya tabia yao ya mubaya. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Inaendelea kuwa jambo la kawaida kuona wazazi wanaachia watoto mamlaka yao. Miaka fulani iliyopita watoto walijua ni nani alikuwa anaongoza; na walijua kama haikuwa wao.” (Narcissism Epidemic)

Bila shaka, wazazi wengi wanajikaza kufundisha watoto wao tabia ya muzuri, kwa kuwawekea mufano muzuri na pia kwa kuwapatia malipizi yasiyobadilika lakini yenye upendo wakati ni lazima kufanya hivyo. Hata hivyo, kama vile kitabu chenye tumekwisha kutaja kinaonyesha, wazazi wenye wanatambua faida ya kufanya hivyo, “wanatenda tofauti na namna watu wengine wanafanya.”

Ni nini ilifanya mambo yakuwe hivi? Ni mubaya kupatia mutoto malipizi?

Mamlaka ya Wazazi Inapunguka

Watu fulani wanasema kuwa mamlaka ya wazazi ilianza kupunguka katika miaka ya 1960, wakati watu wenye elimu walikuwa wanashauria wazazi wakuwe wanavumilia watoto zaidi. Walisema hivi: ‘Ukuwe rafiki, usijionyeshe kuwa na mamlaka.’ ‘Ni muzuri kusifu mutoto kuliko kumupatia malipizi.’ ‘Kuliko kurekebisha tabia za mubaya za watoto wako, ujikaze kuona mambo mazuri yenye wanafanya.’ Kuliko kuonyesha usawaziko kati ya kusifu watoto na kuwapatia malipizi, ilionekana kuwa watu wenye elimu wanapenda kusema kama kukaripia watoto kunaweza kuwaumiza katika moyo, na kunaweza kufanya wakasirikie wazazi wao baadaye katika maisha.

Kisha muda fulani, watu wenye elimu walianza kukazia kama ni muzuri mutoto ajisikie kuwa mutu wa maana. Ilikuwa kama vile siri ya kulea watoto ilikuwa imevumbuliwa mara moja, na siri hiyo ilikuwa: Fanya watoto wako wajione kuwa watu wa maana. Kwa kweli, ni jambo la lazima kufanya watoto wajitumainie. Lakini watu hao wenye elimu walipitisha mipaka wakati walikuwa wanakazia faida ya kufanya watoto wajione kuwa watu wa maana. Waliambia wazazi hivi: ‘Muepuke kutumia maneno ya kukataza, kama vile hapana ao ni mubaya.’ ‘Muendelee kuambia watoto wenu kama wao ni watu wa maana na wanaweza kuwa kile wanapenda.’ Ilikuwa kama, kujiona kuwa mutu wa maana ni jambo la lazima kuliko kuwa mutu wa maana.

Kufanya watoto wajione kuwa watu wa maana kunafanya wajisikie kuwa na haki zote

Mwishowe, watu fulani wanasema kama kufanya watoto wajione kuwa watu wa maana kunafanya wajisikie kuwa na haki zote; ni kama vile wengine wako na deni yao. Kitabu kimoja kinasema kuwa hilo limefanya watoto wengi “wasikuwe tayari kupambana na hali zenye watakuta katika maisha wakati wengine watawachambua, ao hata wakati watashindwa kutimiza mambo fulani.” (Generation Me) Baba mumoja mwenye anatajwa katika kitabu hicho alisema hivi: “Katika kazi hakuna mambo ya kujiona kuwa mutu wa maana. . . . Ikiwa unatoa ripoti ya mubaya kwenye biro, mukubwa wako wa kazi hatasema, ‘Ee, ninapenda rangi ya karatasi yenye ulichagua.’ Kukomalisha watoto kwa njia hiyo ni kuwakosea sana.”

Mawazo ya Watu Yanabadilika

Kwa miaka mingi, namna wazazi wanalea watoto imeonyesha mara nyingi kama mawazo ya wanadamu yanabadilika kila mara. Mushauri Ronald Morrish aliandika hivi: “Namna ya kulea watoto inaendelea kubadilika. Inaonyesha mabadiliko katika maisha yetu.” * Kama vile Biblia inasema, ni mwepesi kwa wazazi “kurushwa huku na huku kama kwa mawimbi na kuchukuliwa huku na huku na kila upepo wa fundisho.”—Waefeso 4:14.

Ni wazi kuwa mawazo yenye kuenea sana leo juu ya kukosa kupatia watoto malipizi yamekuwa na matokeo mabaya. Yamepunguza mamlaka ya wazazi, lakini pia yamefanya watoto wabakie bila muongozo wenye wanahitaji ili kufanya maamuzi mazuri na kujitumainia kwa njia yenye kufaa katika maisha.

Kuna namna ya muzuri ya kufanya?

^ fu. 15 Ni sisi tumetia maandishi hayo katika italiki; yametoka katika kitabu Secrets of Discipline: 12 Keys for Raising Responsible Children.