Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Kweli ya Biblia Inafika Katika Inchi ya Japani

Kweli ya Biblia Inafika Katika Inchi ya Japani

Mialiko kwa ajili ya hotuba ya watu wote ilitolewa katika muji wa Tokyo na ilimwangwa katika muji wa Osaka kwa njia ya avion

TAREHE 6 Mwezi wa 9, 1926, piligrimu mumoja (mwangalizi mwenye kusafiri) wa États-Unis mwenye alizaliwa katika inchi ya Japani, alirudia katika inchi yake ili kuwa misionere. Wakati alifika katika inchi ya Japani, alipokelewa tu na mutu mumoja mwenye alijiandikisha ili akuwe anapokea gazeti Munara wa Mulinzi. Mutu huyo, alikuwa ameanzisha katika muji wa Kobe kikundi cha kujifunza Biblia. Wanafunzi hao wa Biblia, walifanya mukusanyiko wao wa kwanza tarehe 2 Mwezi wa 1, 1927, katika muji huo. Watu 36 walihuzuria mukusanyiko huo, na watu 8 wakabatizwa. Huo, ulikuwa mwanzo muzuri, lakini namna gani kikundi hicho kidogo kingeweza kuhubiria watu milioni 60 wenye walikuwa na lazima ya kupata kweli ya Biblia?

Katika Mwezi wa 5, 1927, Wanafunzi hao wa Biblia walianzisha kampanye ya kutoa ushahidi mahali pa watu wengi. Kupitia kampanye hiyo, walialika watu kwenye hotuba mbalimbali zenye kutegemea Biblia. Ili waweze kualika watu kwenye hotuba ya kwanza yenye ilipaswa kutolewa katika muji wa Osaka, ndugu walitumia pankarte na vibao vikubwa-vikubwa vya matangazo katika kila eneo la muji, na wakatuma mialiko 3000 kwa watu wenye kujulikana sana. Tena waligawanya mialiko 150000, na wakatumia magazeti ya Osaka yenye kujulikana sana na pia tiketi (billets) 400000 za treni (train) ili kutangaza hotuba hiyo. Siku ya hotuba hiyo, avion mbili zilimwanga katika muji huo, mialiko 100000. Watu karibu 2300 walijaza Jumba la Osaka Asahi ili waweze kusikiliza hotuba “Ufalme wa Mungu Unakaribia.” Kwa sababu fasi ilikuwa kidogo, watu wengine karibu 1000 waliombwa warudie nyumbani. Kisha hotuba hiyo, zaidi ya watu 600 walibakia kwa ajili ya sehemu ya maulizo na majibu. Na katika miezi yenye ilifuata, ndugu walitoa hotuba za watu wote zenye kutegemea Biblia katika muji wa Kyoto na miji mingine.

Katika Mwezi wa 10, 1927, Wanafunzi wa Biblia walipanga kutoa hotuba mbalimbali katika muji wa Tokyo. Walialika watu wengine wenye kujulikana sana. Walialika waziri wa kwanza, watu wenye kutumika katika bunge ( parlement), na pia viongozi wa dini na viongozi wa maaskari. Walitumia picha kubwa-kubwa, magazeti, na pia mialiko 710000; hilo lilifanya watu 4800 wakuje kusikiliza hotuba tatu zenye zilitolewa katika muji mukubwa wa Japani.

WAKOLPORTERE WENYE BIDII

Katsuo na Hagino Miura

Wakolportere (mapainia) walitumika sana ili kupelekea watu ujumbe wa Ufalme kwenye nyumba zao. Dada Matsue Ishii ni mumoja kati ya wakolportere wa kwanza katika inchi ya Japani. Yeye na Jizo bwana yake, walihubiri katika sehemu kubwa sana ya inchi, ni kusema, katika Sapporo kaskazini mwa Sendai, Tokyo, Yokohama, Nagoya, Osaka, Kyoto, Okayama, na Tokushima. Dada Ishii pamoja na dada yake mukubwa mwenye anaitwa Sakiko Tanaka, walivaa kimono ao mavazi ya heshima ya inchi yao ili kutembelea wakubwa wa serikali. Mumoja kati ya wakubwa hao aliomba furushi 300 ya vitabu La Harpe de Dieu na La Délivrance ili avitie katika maktaba mbalimbali za gereza.

Katsuo Miura pamoja na Hagino walikubali vitabu vyenye Dada Ishii aliwatolea, na bila kukawia wakatambua kwamba wamepata kweli. Walibatizwa katika mwaka wa 1931 na kisha wakakuwa  wakolportere. Haruichi Yamada pamoja na dada Tane bibi yake, na watu wengi katika jamaa yao walikubali ujumbe wa Ufalme muda fulani mbele ya mwaka wa 1930. Kisha, ndugu Yamada pamoja na bibi yake walikuwa wakolportere, na Yukiko binti yao akaenda kutumikia kwenye Beteli ya Tokyo.

“YEHU” NDOGO NA “YEHU” KUBWA

Yehu Kubwa ilikuwa na fasi kwa ajili ya mapainia sita

Wakati huo, motokari zilikuwa bei sana na barabara zilikuwa mbaya sana. Kwa hiyo, ndugu Kazumi Minoura pamoja na vijana wengine wakolportere walitumia magari ya kukokotwa na yenye ilitumiwa pia kama nyumba. Waliita magari hayo kwa jina la Yehu, muendesha-gari mwenye bidii ambaye alikuja kuwa mufalme wa Israeli. (2 Fal. 10:15, 16) Yehu kubwa-kubwa zilikuwa tatu. Kila Yehu ilikuwa na urefu wa metre 2,20; upana wa metre 1,90; na kimo cha metre 1,90; na kila Yehu ilikuwa na fasi kwa ajili ya mapainia sita. Tena, Beteli ya Japani ilitengeneza Yehu ndogo 11 zenye kukokotwa na kinga na zenye zilikuwa na fasi ya kutosha kwa ajili ya mapainia wawili. Ndugu Kiichi Iwasaki, mwenye alisaidia kujenga Yehu, anasema hivi: “Kila Yehu ilikuwa na hema na bateri ya motokari yenye ilisaidia kupata mwangaza.” Wakolportere walieneza nuru ya kweli katika inchi ya Japani kwa kutumia Yehu zenye ziliwasaidia kushuka na kupanda milima, na kupita katika mabonde, kuanzia Hokkaido, eneo la kaskazini, mupaka Kyushu kusini mwa Japani.

Yehu Ndogo ilikuwa na fasi kwa ajili ya mapainia wawili

Kolportere mumoja mwenye anaitwa Ikumatsu Ota anasema hivi: “Wakati tulifika katika muji, tulisimamisha Yehu yetu pembeni ya mutoni ao mahali fulani penye kuonekana wazi. Mbele ya yote tulienda kuwaona wanaume wenye mamlaka katika muji, kama vile kiongozi wa muji, na kisha hapo tulitembelea watu kwenye nyumba zao ili tuwatolee vichapo. Kisha kuhubiri katika eneo lote la muji huo, tulienda katika muji mwingine.”

Ilikuwa “siku ya mambo madogo” wakati hao Wanafunzi wa Biblia 36 walifanya mukusanyiko wao wa kwanza katika muji wa Kobe. (Zek. 4:10) Lakini kisha tu miaka 5, ni kusema, katika mwaka wa 1932, hesabu ya wakolportere na wahubiri wenye walitoa ripoti katika Japani ilikuwa 103, na walitolea watu zaidi ya vitabu 14000. Leo, mahubiri ya mahali pa watu wengi yanapangwa vizuri katika miji mikubwa-mikubwa ya Japani, na karibu wahubiri 220000 wanaendelea kueneza kweli ya Biblia katika inchi yote ya Japani.—Habari hii ilichukuliwa katika vitu vya maana sana vya historia yetu kutoka Japani.

Ilichorwa na ndugu Kiichi Iwasaki, mwenye alijenga Yehu kwenye Beteli ya Japani