MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 4, 2014

Gazeti hili linaeleza namna gani tunaweza kuonyesha imani kama vile Musa. Namna gani Yehova anaona madaraka ya familia na namna gani anatusaidia kuyatimiza?

Tuige Imani ya Musa

Namna gani imani ilimuchochea Musa atupilie tamaa za mwili na kufurahia kazi yake? Sababu gani Musa ‘alikaza macho kwenye malipo ya zawadi’?

Unamuona “Yeye Asiyeonekana”?

Namna gani imani ya Musa katika Mungu ilimulinda asiogope mwanadamu na kumusaidia aonyeshe imani katika ahadi za Mungu? Tia nguvu imani yako kwa kumuona Yehova kama Mutu anayeonekana ambaye iko tayari kukusaidia.

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Mahali Ambapo Utumishi wa Wakati Wote Umeniongoza

Wazia miaka 64 katika utumishi wa wakati wote, jifunze sababu gani Robert Wallen anasema kwamba amebarikiwa sana na kuwa na maisha yenye kusudi.

Hauwezi Kuwatumikia Mabwana Wawili

Watu fulani wanahamia katika inchi za kigeni ili kupata feza nyingi. Kutumikia mbali na familia yetu kuna matokeo gani juu ya ndoa yetu, watoto wetu, na uhusiano wetu pamoja na Mungu?

Usiogope—Yehova Atakusaidia!

Namna gani baba mumoja alifanya maisha ya familia yake yawe mazuri tena kisha kuishi mbali na familia yake kwa sababu ya kazi ya kimwili? Namna gani Yehova alimusaidia ategemeze familia yake wakati wa kipindi cha matatizo ya feza?

Unafurahia Namna Yehova Anavyokuchunguza?

Jifunze sababu tano zinazofanya Mungu atuchunguze na namna gani kila mumoja wetu anaweza kufaidika na uchunguzi huo.

Je, ulijua?

Ilimaanisha nini mutu kupasua nguo zake kwa makusudi katika siku za Biblia?