Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HEKIMA YA ZAMANI YENYE FAIDA LEO

Muache Kuhangaika

Muache Kuhangaika

KANUNI YA BIBLIA: ‘Muache kuhangaika juu ya nafsi zenu.’—Mathayo 6:25.

Kuacha kuhangaika kunamaanisha nini? Yesu alisema maneno hayo katika Mahubiri yake ya Mulimani. Kulingana na kitabu kimoja chenye kufasiria maneno ya Biblia, neno la Kigiriki lenye lilitafsiriwa “kuhangaika” linaweza kumaanisha “namna mutu anatenda kwa kawaida wakati anapatwa na umasikini, njaa, na shida zingine zenye kumufikia katika maisha yake ya kila siku.” Mara nyingi, mahangaiko yanamaanisha pia kuogopa sana juu ya mambo yenye yanaweza kutokea wakati unaokuja. Ni jambo la kawaida na lenye kufaa kuhangaika juu ya mambo yenye tuko nayo lazima na juu ya hali ya muzuri ya watu wenye tunapenda. (Wafilipi 2:20) Lakini, wakati Yesu alisema, ‘muache kuhangaika,’ alikuwa anashauria wanafunzi wake waepuke mahangaiko yasiyokuwa ya lazima, ni kusema, kuogopa sana juu ya kesho, jambo lenye linaweza kumunyanganya mutu furaha ya kuishi leo.—Mathayo 6:31, 34.

Kuacha kuhangaika kuko na faida leo? Ni jambo la hekima kufuata shauri hilo la Yesu. Sababu gani? Vitabu fulani vinaonyesha kama wakati mutu anaogopa kupita kiasi, sehemu ya mufumo wa neva yenye kuchochea mupigo wa moyo na mishipa ya damu (système nerveux sympathique) inatumika sana, na hali hiyo “inaleta matatizo ya afya kama vile vidonda kwenye estoma, magonjwa ya moyo, na asthme.”

Yesu alitupatia sababu ya muzuri ya kuacha kuhangaika sana: Kuhangaika ni jambo lenye halina maana. Yesu aliuliza hivi: ‘Ni nani kati yenu kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye uhai [uzima] wake?’ (Mathayo 6:27) Kuogopa sana hakuwezi kuongeza hata sehemu kidogo juu ya maisha yetu ao hata kuyafanya yakuwe ya muzuri. Tena, kusema kweli, mara nyingi mambo hayakuwe kama vile tuliogopa yatakuwa. Mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia anasema hivi: “Kuogopa juu ya wakati unaokuja ni kupoteza wakati, na mara nyingi wakati unaokuja unakuwa muzuri kuliko vile tuliwazia.”

Namna gani tunaweza kuacha kuhangaika? Jambo la kwanza, umutumainie Mungu. Ikiwa Mungu analisha ndege na kupamba maua muzuri, hataweza kutoa mambo ya lazima kwa watu wenye kutia ibada yake pa nafasi ya kwanza katika maisha yao? (Mathayo 6:25, 26, 28-30) Jambo la pili, uhangaikie tu mambo ya leo. Yesu alisema hivi: ‘Musihangaike kamwe juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe.’ Haukubali kama kila siku iko na ubaya wake?—Mathayo 6:34.

Kama tunafuata shauri hilo la Yesu lenye hekima, tunaweza kuepuka kujiletea magumu ya kimwili. Zaidi ya hilo, tutapata utulivu wa ndani wenye Biblia inaita “amani ya Mungu.”—Wafilipi 4:6, 7.