Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

TATIZO

Amani na Usalama Wetu Viko Katika Hatari

Amani na Usalama Wetu Viko Katika Hatari

“Kizazi hiki kinatumia teknolojia ya hali ya juu, sayansi na feza mingi . . . Lakini pia, pengine njo kizazi cha kwanza chenye kitafanya mifumo [ya mambo ya politike, mambo ya feza, na mazingira] ya ulimwengu iharibike.”​—The Global Risks Report 2018, World Economic Forum.

JUU YA NINI WATU WENGI WENYE ELIMU WAKO NA WASIWASI JUU YA WAKATI WETU WENYE KUJA NA ULE WA DUNIA? FIKIRIA MAGUMU FULANI KATI YA MAGUMU YENYE TUNAPAMBANA NAYO.

  • KUKOSA USALAMA KU ENTERNETE: Gazeti moja la Australia linasema kama “Enternete inaendelea kuwa fasi yenye kuwa hatari. Ni fasi kwenye unaweza kupata watu wenye kupenda kufanya ngono na watoto, wachokozi, watu wenye kuchochea ugomvi, na watu wenye kujaribu kuingia katika mufumo wa ordinatere ili kupata habari za siri. Kuiba watu utambulisho ni moja kati ya uvunjaji wa sheria wenye unaendelea kuongezeka haraka zaidi mu dunia. . . . Enternete inapatia watu nafasi ya kuonyesha tabia za mubaya zaidi; watu wanakuwa waovu na wakali.”

  • KUKOSA USAWAZISHO MU MAMBO YA FEZA: Kulingana na ripoti ya hivi karibuni ya Shirika la Kimataifa la Oxfam, watu 8 wenye kuwa matajiri zaidi wako na mali yenye kulingana na mali ya watu miliare 3,6 wenye kuwa maskini zaidi mu dunia. Ile ripoti ilisema kama “hakuna usawazisho mu mambo ya feza juu watu kidogo wenye ni matajiri sana wanaendelea kuwa matajiri zaidi na watu wenye ni maskini wanaendelea kuwa maskini zaidi; na kati ya watu maskini zaidi, wengi ni wanamuke.” Watu wengi wanaogopa kama pengine kukosa usawazisho mu mambo ya feza kutachochea watu wakuwe waasi.

  • VITA NA MATESO: Ripoti ya 2018 ya Shirika la Umoja wa Mataifa Lenye Kuhangaikia Wakimbizi ilisema hivi: “Leo kuliko wakati mwingine wowote katika historia, watu wengi sana wanaacha nyumba zao.” Watu zaidi ya milioni 68 wamelazimika kuacha nyumba zao, zaidi sana kwa sababu ya vita ao mateso. Ripoti ilisema kama “kila segonde mbili, karibu mutu 1 analazimika kuacha nyumba yake.

  • MAZINGIRA IKO MU HATARI: Ripoti moja ya The Global Risks ya 2018 inasema kama “aina mingi za mimea na wanyama zinaendelea kupotea haraka sana,” na kama “kuchafuliwa kwa hewa na maji ya bahari kunaendelea kuwa hatari sana kwa afya ya wanadamu.” Pia, hesabu ya vidudu mu inchi fulani inaendelea kupunguka sana. Kwa kuwa vidudu vinasaidia mimea izae, wanasayansi wanasema kama kuko uwezekano mukubwa kwamba mazingira yetu itaharibika.

Je, tunaweza kufanya mabadiliko yenye kuombwa ili ulimwengu ukuwe wenye amani na usalama zaidi? Watu fulani wanawaza kama ili kuweza kufanya mabadiliko, watu wanapaswa kufundishwa. Kama ni vile, ni mafundisho ya namna gani yenye wanapaswa kupata? Habari zenye kufuata zitazungumuzia ile maulizo.