Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SERIKALI YENYE ITAMALIZA MAGUMU

“Amani Haitakuwa na Mwisho”

“Amani Haitakuwa na Mwisho”

Umoja wa Mataifa unatia watu wote moyo waungane mukono, waheshimie haki za kibinadamu, na walinde mazingira. Juu ya nini? Kama vile Maher Nasser anaeleza katika gazeti la UN Chronicle, “vikundi vya wavunjaji wa sheria, kubadilika kwa hali ya hewa, kuongezeka kwa kukosa usawazisho katika hali ya maisha, kushindwa kumaliza vita, watu wengi kuacha nyumba zao, ugaidi (ao, terrorisme), magonjwa yenye kuambukiza, na mambo ingine yenye kufanana na hayo inafanyika . . . kila mahali.”

Wengine hata wameenda mbali zaidi kwa kutetea wazo la kuwa na serikali moja tu mu dunia yote. Watu hao wanatia ndani Dante mwenye alikuwa mwanafilozofia wa Italia, mwandikaji wa mashairi (ao, poète), na mukubwa wa politike mwenye kuheshimiwa (1265-1321) na mwanafizikia mwenye kuitwa Albert Einstein (1879-1955). Dante aliamini kama amani haingefanya wakati murefu katika ulimwengu wenye kugawanyika mu mambo ya politike. Akitaja maneno ya Yesu Kristo, Dante alisema kama “ufalme wenye umegawanyika juu yake wenyewe unafikia kwenye uharibifu wake.”​—Luka 11:17.

Muda mufupi kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, vita mwenye mabomu mbili ya atomu ilitumiwa, Albert Einstein aliandikia Baraza Kubwa la Umoja wa Mataifa barua​—barua yenye ilitangazwa katika magazeti. Alisema hivi: “Umoja wa Mataifa unapaswa kufanya haraka sana ili kutokeza hali zenye zitafanya kukuwe amani katika dunia yote kwa kuweka misingi ili kuwa na serikali moja tu ya kweli katika dunia yote.”

Lakini, tunaweza kusema kama wakubwa wa politike wenye wangekuwa mu ile serikali wangekataa kabisa kata-midomo, wangeweza kutimiza mambo yenye waliahidi, na hawangetesa watu? Ao wangekuwa tu wabaya kama watawala wengine? Ile maulizo inatukumbusha maneno ya mwanahistoria wa Mwingereza Lord Acton, mwenye alisema hivi: “Nguvu inaharibu, na nguvu kamili inaharibu kwa ukamili.”

Hata hivyo, ili familia ya wanadamu zikuwe na umoja na amani ya kweli, tunapaswa kuungana. Lakini hilo linawezekana namna gani? Je, inawezekana hata kufanya vile? Jibu la Biblia ni ndiyo. Inawezekana na ni vile itakuwa. Namna gani? Haitawezekana kupitia serikali moja ya dunia yenye kufanyizwa na wakubwa wa politike wenye ni wabaya. Lakini itawezekana kupitia serikali yenye Mungu ametayarisha. Zaidi ya hilo, ile serikali itaonyesha haki yake ya kutawala viumbe wake. Ni serikali gani? Biblia inataja hata jina la ile serikali​—“Ufalme wa Mungu.”​—Luka 4:43.

“UFALME WAKO UKUJE”

Yesu Kristo alikuwa anafikiria Ufalme wa Mungu wakati alisema hivi katika sala yake ya mufano: “Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani.” (Matayo 6:9, 10) Ndiyo, Ufalme wa Mungu utahakikisha kama Mapenzi ya Mungu imefanyika ku dunia, hapana mapenzi ya wale wenye wako na pupa ya mamlaka na wenye ni wachoyo.

Ufalme wa Mungu unaitwa pia “Ufalme wa mbinguni.” (Matayo 5:3) Juu ya nini? Ni juu utatawala kutoka mbinguni hapana kutoka duniani. Utatawala dunia. Maana yake nini? Ni kusema, ile serikali haitaomba watu feza ao mambo kama vile kodi (ao, taxes). Itakuwa kitulizo kabisa kwa raia wa ile serikali!

Kama vile tu maneno “ufalme” inaonyesha, Ufalme wa Mungu ni serikali ya kifalme. Ile serikali iko na Mufalme​—Yesu Kristo—​mwenye alipata mamlaka yake kutoka kwa Mungu. Kumuhusu Yesu, Biblia inasema hivi:

  • “Utawala utakaa juu ya bega lake . . . Kuongezeka kwa utawala wake na amani, havitakuwa na mwisho.”​—Isaya 9:6, 7.

  • “Akapewa utawala, heshima, na ufalme, ili vikundi vya watu, mataifa, na vikundi vya luga, wote wamutumikie. Utawala wake . . . hautapitilia mbali.”​—Danieli 7:14.

  • “Ufalme wa ulimwengu umekuwa Ufalme wa Bwana wetu [Mungu] na wa Kristo wake.”​—Ufunuo 11:15.

Ili kutimiza sala ya Yesu ya mufano, Ufalme wa Mungu utatimiza kwa ukamili mapenzi ya Mungu ku dunia. Katika ule ufalme, wanadamu wote watajifunza namna ya kutunza dunia hivi kwamba ikuwe muzuri tena na kujaa viumbe vyenye kuishi.

Zaidi ya yote, Ufalme wa Mungu utafundisha raia wake. Raia wote watafundishwa kanuni zilezile. Hakutakuwa migawanyiko. Andiko la Isaya 11:9 linasema hivi: “Hawatatokeza jambo lolote lenye kuumiza . . . kwa maana dunia hakika itajaa ujuzi juu ya Yehova kama vile maji yanafunika bahari.”

Wakaaji wa dunia wataishi wote kwa umoja na amani, jambo lenye Umoja wa Mataifa ungependa kutimiza. Andiko la Zaburi 37:11 linasema kama watu “watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.” Ile wakati, hatutazungumuzia tena maneno kama vile “uvunjaji wa sheria,” “kuchafuliwa kwa hewa,” “umaskini,” na “vita”. Lakini, mambo hayo itafanyika wakati gani? Kwa kweli, ni wakati gani Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia? Utafanya vile namna gani? Na namna gani unaweza kupata baraka za ule ufalme? Tuzungumuzie basi jambo hilo.