Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ADRESI YA JW.ORG

Tumia Biblia ya Funzo

Tumia Biblia ya Funzo

Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya (ya funzo) iko na vifaa vya funzo, kutia ndani:

  • Utangulizi wa kila Kitabu cha Biblia, na pia video ya utangulizi

  • Wazo kubwa, ao maelezo makubwa ya kila kitabu

  • Maandishi ya funzo kuhusu kila andiko

  • Maelezo ya chini kuhusu maneno ao misemwa

  • Maelezo ya pembeni kwenye ukurasa

  • Media (picha na video)

  • Liste ya maneno ya Biblia

  • Nyongeza zenye kuwa na karte, picha, na habari zingine za kusaidia kutafuta habari

  • Usomaji wa kusilikiza tu wa kila sura

  • Maandiko katika tafsiri zingine za Biblia

Sehemu ya funzo ya kitabu cha Mathayo ilitolewa katika Kiingereza Mwezi wa 10, 2015. Vitabu vingine vya Biblia vitaongezwa wakati vinamalizika.

Tumia misaada hii ili kuzoea Biblia ya Funzo:

  • Kupata kitabu na sura ya Biblia

  • Tumia vyombo vya kujifunza kwa ajili ya sura ya Biblia

  • Angalia picha na video za kitabu cha Biblia

  • Tumia maelezo kuhusu kitabu, maneno ya Biblia, na nyongeza

Kupata Kitabu na Sura ya Biblia

Uende kwenye VICHAPO > BIBLIA na ufinye Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya (ya funzo) jalada ao fungua maandishi.

Ukurasa wa Habari Zenye Ziko Ndani unaonyesha vitabu vya Biblia vyenye vinapatikana, na ukurasa huo uko na rangi ya blue. Unaunganishwa pia na habari zingine, kutia ndani maana ya maneno ya Biblia, nyongeza, na media (picha na video).

  • Finya kwenye Mosaïque ili kuona mambo yenye kuwa katika Biblia ya Funzo. Ni hivyo inaonekana.

  • Finya Liste ili kuona mambo yenye kuwa katika Biblia ya funzo, Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo upande moja na Maandiko ya Kiebrania upande mwengine.

Finya kwenye kitabu cha Biblia. Ukurasa wenye utatokea uko na liste ya sura, maelezo kwa kifupi ya kitabu cha Biblia, na mahali pa kufinya ili kupata mambo mengine mawili yenye kufuata:

  • Utangulizi wa kitabu cha Biblia, na video ya utangulizi.

  • Maelezo kwa kifupi ya kitabu cha Biblia. Tofauti na sehemu Yaliyomo ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, yenye inaonyesha liste kulingana na sura, Biblia ya Funzo inaonyesha vichwa ao habari kubwa zenye kuzungumuziwa katika kila kitabu cha Biblia.

Chagua sura yenye unapenda kujifunza.

Liste yenye kuwa juu ya kila mwanzo wa ukurasa inaonyesha kitabu na sura. Tumia liste hii ili kuchagua kitabu ao sura ingine ya Biblia, ao mambo mengine ya Biblia ya Funzo, kama vile maana ya maneno ya Biblia.

Tumia Vyombo vya Kujifunza kwa Ajili ya Sura ya Biblia

Maandishi ya sura inaonekana katika namna mbili: ya Kusoma kwenye mukono wa kushoto wa ecran, na ya Kujifunza kwenye mukono wa kuume. (Maagizo: Kwenye chombo ndogo, sehemu ya Kujifunza inafichama, lakini inaonekana kama unafinya kwenye mustari wa andiko, alama ya maelezo ya chini, herufi ya maelezo ya pembeni, ao kama unafinya sehemu Afficher.)

Habari zenye kufuata zinaeleza kwa kifupi namna ya kupata mambo mengine ya sehemu ya kujifunza:

  • Finya sura ao mustari katika sehemu ya Kujifunza, ili kuona habari za kujifunza na andiko.

  • Finya alama ya maelezo ya chini ili kuona maelezo ya chini na maneno ao misemwa ya maelezo hayo.

  • Finya herufi katika maelezo ya pembeni ili kupata maelezo mengi katika sehemu ya Kujifunza na uone maandishi ya andiko lenye kuhusika.

  • Ili usikilize sura hiyo, anza kwenye mustari fulani, finya maandishi ya andiko, kisha ufinye alama ya kusikiliza.

  • Ili kusikiliza sehemu hiyo kuanzia mwanzo wa sura, finya Soma ao Lecture.

  • Kwenye Andiko Lenye Kutajwa, finya Soma ao Lecture ili usikilize andiko lenye kutajwa tu.

  • Finya Tua ili kusimamisha andiko lenye unasikiliza.

  • Finya Découverte ili kufungua sehemu hiyo ya Kujifunza na uonyeshe maelezo yote, maelezo ya chini, maandiko ya pembeni, na picha na video ya sura hiyo. (Sehemu hiyo inaonekana mara moja wakati unafungua sura fulani.)

  • Finya Comparaison Biblique ili upate sehemu hiyo kwenye sehemu ya Funzo na uone namna gani namna andiko hilo linatafsiriwa katika Biblia zingine.

  • Finya Reference Marginale (maandiko ya pembeni) ili sehemu hiyo ionekane kwenye sehemu ya Funzo na kuonyesha liste ya maandiko yote yenye kupatikana pembeni ya ukurasa wa sura hiyo.

  • Ili sehemu ya Funzo ionekane kwenye chombo ndogo, ni vizuri kufinya sehemu Afficher.

  • Ili kuficha sehemu ya Funzo kwenye chombo ndogo, finya sehemu Cacher.

Sehemu ya Découverte

Sehemu hii inaanza na maelezo kwa kifupi ya kitabu cha Biblia kuhusu sura fulani. Kama maelezo hayo yako na sehemu ndogo-ndogo, finya alama (+) ili kuonyesha sehemu zingine ao alama (-) ili kuzificha.

Kisha, kwenye kila andiko la sura utaona:

  • Maandishi ya funzo: Habari za funzo kuhusu andiko hilo.

  • Media: Picha na video zenye kuhusiana na andiko hilo. Finya picha ao maelezo yake ili kufungua Gallérie Media ili upate habari nyingi zaidi.

  • Maelezo ya Chini: Habari zingine kuhusu maneno ao misemwa katika andiko.

  • Maandiko ya Pembeni: Maandiko ya pembeni yanaunganishwa na maneno ao misemwa katika andiko. Finya alama (+) ili kupata habari zaidi kuhusu andiko. Finya alama (-) ili kuficha andiko.

Katika sehemu ya Kusoma, finya namba ya andiko, alama ya maelezo ya chini, ao herufi ya maandiko ya pembeni ili habari ionekane katika sehemu ya Funzo.

Comparaison Biblique

Sehemu ya Comparaison Biblique inaonyesha namna andiko linatafsiriwa katika Biblia mbalimbali. Andiko andiko lingine katika sehemu ya Kusoma ili kuona namna linatafsiriwa katika Biblia zingine.

Maandiko ya Pembeni Kwenye Ukurasa

Sehemu hii inaonyesha maandiko yote ya pembeni ya sura hiyo, ikigawanywa katika sehemu tatu:

  1. Habari Ileile: Maandiko ya habari ileile katika kitabu kingine ao sura ingine ya Biblia.

  2. Mitajo (citation): Maandiko mengine ya Biblia yenye kutajwa katika sura hiyo.

  3. General (Kwa ujumla): Maandiko ya pembeni yenye haiko habari ileile ao mitajo. Inaweza kuwa maandiko mengine kuhusu mutu uleule ao mahali palepale, musemwa uleule, utimizo wa unabii fulani, ao maelezo kuhusu kanuni fulani.

Katika kila sehemu hizo, finya alama ya (+) ili kuonyesha maandiko yote ya pembeni kuhusu andiko fulani, ao alama (-) ili kuyaficha.

Kisha ufinye mahali pa rangi mbalimbali ili kutia rangi maandiko yote ya pembeni. Kufanya hivyo kunaweza kusaidia kwa mufano kama unapenda kujua mahali kwenye muandishi fulani wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo alitaja Maandiko ya Kiebrania.

Angalia Picha na Video za Kitabu cha Biblia

Gallérie Media ni picha zote na video zenye kuhusiana na kila kitabu cha Biblia. Picha hizo na video zinaonekana kwa utaratibu muzuri.

Fuata njia hizi ikiwa uko katika Gallérie Media:

  • Finya picha katika sehemu ya Funzo.

  • Kwenye ukurasa wa Habari Zenye Kuwa Ndani ao liste, chagua Media. Finya picha ao kiunganisho cha kitabu ya Biblia.

Gallérie Media iko na sehemu tatu:

  1. Finya Mukuki wa kushoto ao wa kuume ili uone picha ao video yenye kufuata ao yenye ilishapita.

  2.  

    Kwenye chombo ndogo, finya Onyesha Mafasirio ya Picha ili kuona mafasirio hayo.

  3. Finya mukuki wa kushoto ao wa kuume ili kuona picha ndogo zingine. Finya picha ndogo ili kuona picha ao video yenye kuhusika.

Ukisha kuchagua picha, unaweza kuinenepesha ao kuipunguza, ao kutumia alama zingine kwenye ecran zenye zinaweza kufanya kazi hiyo.

Kama unachagua video, unaweza kuiendesha, kutua ao kuitazama ikiwa kubwa.

Tumia Maelezo kwa Kifupi ya Kitabu cha Biblia, Maelezo ya maneno, ao Nyongeza

Kuko namna mbili ya kufanya hivyo:

  • Finya kiunganisho cha andiko kwenye sehemu ya Funzo.

  • Chagua moja ya habari hizo kutoka ukurasa wa Habari Zenye Kuwa Ndani ao kwenye liste.

Maelezo kwa kifupi juu ya kitabu cha Biblia inaonekana. Tumia alama (+) kuona sehemu yote alama (-) kama haupendi kuona habari zote.

Maelezo ya maneno ni liste ya maneno yenye kutumiwa katika Biblia na maana yake. Ukifanya sehemu hiyo katika sehemu ya Funzo, itakupeleka mara moja kwenye maneno hayo.

Kama unatumia ukurasa wa Habari Zenye Kuwa Ndani ao liste, finya herufi kwenye liste ili upate habari ya kwanza yenye kuanza na herufi hiyo kisha utafute habari yenye unapenda.

Nyongeza fulani za Biblia ziko na namna mbili ya kuonyesha habari—picha moja (picha ya ukurasa yenye inapatana na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya) ao maandishi na picha tofauti.

  • Ona habari kupitia picha. Finya picha ili kuifungua katika Image Viewer. Unaweza kutumia mukuki kushoto ao kuume ili kunenepesha picha ao kuipunguza ao kutumia sehemu zingine kwenye ecran ili kufanya hivyo.

  • Angalia habari hiyo kama maandishi yenye picha tofauti. Mufumo huo utakusaidia kufinya kiunganishi cha Andiko ao maandiko mengine na kuona maandishi yake katika sehemu ya Funzo.