Ona video zinazopatikana

Jibu ya Sala za Mwanamuke Moja Kipofu

Jibu ya Sala za Mwanamuke Moja Kipofu

 Yanmei ni Shahidi wa Yehova, na anaishi Asia. Siku moya, alimusaidia Mingjie *, mwanamuke moja kipofu, kuvuka barabara. Mingjie akamuambia : “Aksanti sana ! Mungu akubariki!” Wakati alisikia ile maneno, Yanmei akamuuliza ule mwanamuke kipofu kama angependa, wakati ingine, wazungumuzie Biblia pamoja. Kisha wakati, Mingjie alimuambiaka dada yetu kama ile ilikuwa jibu ya sala zake. Kila siku, alikuwa anaomba Mungu amuongoze ku dini ya kweli. Lakini juu ya nini alikuwa anasali vile?

 Mu mwaka 2008, mumoja wa marafiki vipofu wa Mingjie alimualikaka ku kanisa yenye ilikuwa musaada vilema. Wakati misa iliisha, Mingjie akaenda kuuliza Padiri kama aliwasomea kitabu gani. Wakati Padiri alimujibu kama ni Neno ya Mungu Biblia, Mingjie akapenda sana kuisoma. Akapata Biblia ya luga ya Kishinwa yenye kuwa mu maandishi ya vipofu, na akasoma buku zote 32 mu miezi sita. Wakati alikuwa anasoma, Mingjie akajua kama mafundisho ya Utatu Mutakatifu (yenye alifundishwa ku misa) haikukuwa mafundisho ya Biblia, na akajua pia jina ya Mungu: Yehova.

 Hata vile, watu wa kanisa ya Mingjie walimuvunja moyo. Alifikia kujua kama hawakukuwa wanatumikisha mambo yenye Biblia inafundisha. Kwa mufano, chakula yenye ilipigiwa ile siku walikuwa wanaipatia wale wenye hawako vipofu, kisha chakula yenye ilibakia tena yenye ililala njo walipatia vipofu. Ile ilifanya Mingjie aanze kutafuta dini zingine karibu yake. Njo maana, alikuwa anaomba Mungu amusaidie kupata dini ya kweli.

 Namna Yanmei alimutendea kwa upendo, ilimugusa moyo sana. Mingjie alikubali waanze kujifunza Biblia. Kisha siku moya akahuzuria ku mukutano fulani wa Mashahidi wa Yehova. Mingjie anaeleza hivi: “Siwezi kusahau ile mukutano. Ndugu na dada walinisalimia na shauku. Ile ilinigusa sana. Hata niko kipofu, ile haifanye nikuwe tofauti na wengine, na niliona kama watu wote wanapendana.”

 Mingjie aliendelea kujifunza kumujua Yehova na akazoea kuhuzuria ku mikutano. Alikuwa anapenda kuimba nyimbo zetu, hata kama ilikuwa nguvu kwake kuimba juu nyimbo zilikuwa hazijakuwa mu maandishi ya vipofu ya luga ya Kishinwa. Lakini kutaniko ilimusaidia kuandika mu maandishi ya vipofu kitabu yote ya wimbo. Ile kazi ilimukamata saa 22 ili kuandika nyimbo 151! Mu Mwezi wa 4, 2018 Mingjie akakuwa muhubiri na akaanza kuhubiri karibu masaa 30 kila mwezi.

Kuandika kitabu mu maandishi ya vipofu haiko mwepesi

 Ili kumusaidia atayarishe maulizo ya ubatizo, Yanmei alirekodi sehemu ya kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova kwenye kunapatikana maulizo ya ubatizo na maandiko ya Biblia. Mu Mwezi wa 7, 2018 Mingjie alibatizwa. Anasema hivi: “Upendo wenye ndugu na dada walinionyesha ku ile mukusanyiko, ilinigusa sana. Nililia kwa furaha, juu nilikuwa sasa ndani ya dini ya kweli !” (Yohana 13:34, 35). Mingjie ni painia, anaonyesha wengine upendo wengine kama vile yeye alionyeshwa upendo.

^ Majina imebadilishwa.