Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 2

Utangulizi wa Sehemu ya 2

Juu ya nini Yehova alileta garika ao mvua kubwa na kuharibu ulimwengu wa ile wakati? Ku mwanzo wa historia ya watu, Shetani alianzisha uasi juu ya Yehova. Watu fulani sawa vile Adamu, Eva, na mutoto wao Kaini, walichagua kuwa upande wa Shetani. Wengine sawa vile Abeli na Noa, walichagua kuwa upande wa Yehova. Watu mingi walianza kufanya mambo ya mubaya sana mupaka Yehova akaamua kuharibu ule ulimwengu wa watu wabaya. Hii sehemu itatusaidia tujifunze namna Yehova anajisikia juu ya mambo yenye tunachagua kufanya. Itatusaidia tena tujifunze kama Yehova hataruhusu hata kidogo mambo ya mubaya ishinde mambo ya muzuri.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 3

Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu

Juu ya nini muti moja ya mu bustani ya Edeni ilikuwa ya pekee? Juu ya nini Eva alikula tunda ya ile muti?

SOMO LA 4

Aliua Mudogo Wake Juu ya Kasirani

Mungu aliitika zabihu ya Abeli lakini alikataa zabihu ya Kaini. Wakati Kaini aliona vile, alikasirika sana na akafanya jambo la mubaya sana.

SOMA LA 5

Safina ya Noa

Wakati malaika wenye walifanya zambi walikuja ku dunia na kuoa wanamuke, walizaa watoto wenye walikuwa na nguvu sana. Mambo ya mubaya ilienea fasi yote. Lakini Noa alikuwa tofauti​​—alipenda Mungu na alimutii.

SOMO LA 6

Watu Munane Waliokoka Garika

Mvua ilinyesha mu siku 40 muchana na usiku. Noa na familia yake walibakia ndani ya safina zaidi ya mwaka moja. Kisha, Mungu aliwaambia watoke katika safina.