Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | KUSALI KUNALETA FAIDA FULANI?

Sababu Gani Watu Wanasali?

Sababu Gani Watu Wanasali?

“Nilikuwa mutumwa wa michezo ya feza. Nilikuwa ninasali ili nipate ushindi wa utajiri mwingi. Lakini jambo hilo halikutokea hata siku moja.”—Samuel, * inchi ya Kenya.

“Kwenye masomo tulipaswa tu kurudilia sala zenye ­tulikuwa tumefundishwa na kuweka katika akili.”—Teresa, inchi ya Ufilipino.

“Ninasali wakati niko na magumu. Ninasali ili kuomba musamaha wa zambi na ili nikuwe Mukristo muzuri.”—Magdalene, inchi ya Ghana.

Maneno ya Samuel, Teresa, na Magdalene, yanaonyesha kama kuko sababu nyingi zenye zinafanya watu wasali, sababu fulani ni za muzuri kupita zingine. Sala za watu fulani zinatoka moyoni na zingine hazitoke moyoni kabisa. Hata hivyo, iwe watu fulani wanasali ili kuweza mashindano (examen) kwenye masomo, ao kusali ili kikundi cha muchezo chenye wanapenda kipate ushindi, ili wapate muongozo wa Mungu katika maisha yao ya familia ao kwa sababu zingine nyingi, mamilioni ya watu wanaona kuwa ni lazima kusali. Kwa kweli, uchunguzi mbalimbali unaonyesha kama hata watu fulani wenye hawana dini yoyote wanasali kwa ukawaida.

Unasali wakati fulani? Ikiwa jibu ni ndiyo, unasali kwa ajili ya mambo gani? Iwe uko na tabia ya kusali ao hapana, unaweza kujiuliza hivi: ‘Kusali kunaleta faida fulani? Kuko mutu fulani mwenye kusikiliza sala?’ Muandikaji mumoja alionyesha kama sala ni “aina fulani ya matunzo . . . kama vile kuzungumuza na samaki-rafiki.” Waganga fulani wako pia na mawazo kama hayo, wanaita sala kuwa “aina ingine ya matunzo.” Watu wenye kusali wanafanya zoezi fulani lenye halina maana, ao wanapata tu matunzo fulani kupitia zoezi hilo?

Hapana. Biblia inaonyesha kuwa sala iko na faida nyingi, haiko tu aina fulani ya matunzo. Tena, Biblia inatuonyesha kama kuko mutu mwenye anasikiliza sala zenye kutolewa kwa njia ya muzuri na kwa ajili ya mambo yenye kufaa. Jambo hilo ni kweli? Tuone mambo yenye kuhakikisha hilo.

^ fu. 3 Majina fulani yamebadilishwa.