Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

INCHI ZA AFRIKA ZILIZO KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA

Ripoti moja ya Shirika la UNICEF kuhusu inchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara inasema kwamba ni “watoto 38 tu juu ya 100 walio na miaka chini ya 5 ndio wana cheti cha kuzaliwa.” Lakini Elke Wisch, musimamizi wa Shirika la UNICEF katika eneo la kusini na la magaribi mwa Afrika alisema kwamba “kuandikisha watoto wanaozaliwa ni kwa lazima ili wapate matunzo na wasome, ni kwa lazima pia kwa mayatima ili wariti mali ya wazazi wao.”

ITALIA

Kulingana na uchunguzi fulani, vijana wengi wa Italia wanaogopa sana kuonewa na vijana wengine kupitia Internete. Vijana 72 juu ya 100 kati ya vijana walio na miaka 12 mupaka 17 wanasema kwamba wanaogopa sana kuonewa hivyo. Hesabu ya vijana hao wanaoogopa kuonewa kupitia Internete inapita hesabu ya wale wanaoogopa dawa za kulewesha (55 juu ya 100), wale wanaoogopa kutendewa vibaya kingono na watu wazima (44 juu ya 100), ao wale wanaoogopa kupata ugonjwa unaoambukizwa kingono (24 juu ya 100).

JAPANI

Kama gazeti moja la Japani (The Japan Times) lilivyoripoti, hesabu ya vijana wakubwa wa Japani wanaokataa kupandishwa cheo kwenye kazi inaongezeka. Vijana 40 juu ya 100 wanachukia mwenendo mubaya na mazoea mabaya ambayo yameenea sana. Wafanyakazi wengi wanajisikia kuwa hawawezi kutoa maoni yao ao kuongea kwa uhuru na wakubwa wao wa kazi. Wafanyakazi wa zamani walishikamana na wakubwa wao wa kazi, leo wafanyakazi vijana 60 juu ya 100 wanashikamana na kazi yao na wakati huohuo wakingojea kupata kazi nyingine nzuri zaidi.

BRAZILI

Kuanzia mwaka wa 1980 mupaka mwaka wa 2010, karibu watu 800 000 waliuawa kwa bunduki katika inchi ya Brazili. Watu zaidi ya 450 000 waliouawa walikuwa na miaka kati ya 15 na 29. Uchunguzi uliofanywa juu ya watu waliouawa hivi karibuni unaonyesha kwamba mara nyingi watu wanauana kwa sababu ya mabishano ya nyumbani, kutoelewana na majirani, wivu, ao mabishano kati ya watu wanaotembeza motokari.