Habari Njema Juu ya Yesu
Hii mavideo yenye kufurahisha itakusaidia ujifunze mambo mingi juu ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu na Mwokozi wa wanadamu.
Epizode ya 1: Mwangaza wa Kweli wa Dunia
Banadamu bangeokolewa namna gani kutokana na zambi yenye Adamu aliingiza mu dunia? Masiya tu njo tumaini moya ya banadamu.
Epizode ya 2: “Huyu Ni Mwana Wangu”
Yohana Mubatizaji anatayarisha kukuya kwa Masiya. Ona matukio ya kushangaza yenye ilifanyika ku mwanzo wa utumishi wa Yesu hapa ku dunia!
Epizode ya 3: ‘Ni Miye’
Yesu alijitambulisha kuwa Masiya kwa Nikodemo, kwa mwanamuke Musamaria, na ku baakaaji ba Nazareti, lakini ni badogo tu njo benye balimukubali. Kisha kufanya muujiza wa kushangaza sana, alialika banaume benye kuvua samaki bamufuate.
Epizode ya 4: “Ni Juu ya Ile Njo Nilikuya”
Yesu anaonyesha uwezo wake wa kuponyesha batu na kufukuza pepo wachafu. Lakini batu fulani banapinga kazi yake na banapanga kumuua. Yesu anaonyesha huruma ya mingi, anafundisha kwa hekima, anafanya banafunzi, na anachagua mitume 12.
Epizode ya 5: “Bakashangazwa na namna yake ya kufundisha”
Kisha kuponyesha batu bamingi, Yesu anaanza kufundisha batu mu njia yenye hakuna hata mwalimu wao mwenye alishakafanya vile. Banashangala sana kuona namna anafundisha na mamlaka, anatoa mifano, na namna ya kuitumikisha mu maisha ya kila siku.
Epizode ya 6: “Weye Njo Ule Mwenye Anakuya?”
Yesu anatumia nguvu yake juu ya kufufua wafu. Miujuza yake na mafundisho yake ya hekima inaonyesha nia ya benye biko namusikiliza. Kupitia mifano, Yesu anafasiria habari za Ufalme.

