Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 63

Yesu Anatoa Mashauri Kuhusu Kukwaza Wengine na Kuhusu Zambi

Yesu Anatoa Mashauri Kuhusu Kukwaza Wengine na Kuhusu Zambi

MATAYO 18:6-20 MARKO 9:38-50 LUKA 9:49, 50

  • MASHAURI KUHUSU KUKWAZA MWENGINE

  • IKIWA NDUGU ANATENDA ZAMBI

Yesu ametoka kutoa mufano ili kuonyesha namna wanafunzi wake wanapaswa kujiendesha. Wanapaswa kujiona kama watoto wadogo, watu wa hali ya chini na wenye hawatafute cheo. Wanafunzi wanapaswa ‘kupokea watoto hao wadogo kwa sababu ya jina lake na kwa kufanya hivyo wanamupokea Yesu pia.’—Matayo 18:5.

Hivi karibuni, mitume wamekuwa wanabishana ili kujua ni nani ndiye mukubwa zaidi, kwa hiyo pengine wanaona kuwa Yesu amewakemea kupitia maneno yake. Sasa, mutume Yohana anaanza kuzungumuzia jambo lingine lenye limetoka kufanyika. Anasema hivi: “Tuliona mutu fulani akifukuza pepo wachafu kwa kutumia jina lako, na tulijaribu kumuzuia, kwa sababu yeye hakufuate pamoja na sisi.”—Luka 9:49.

Je, Yohana anaona mitume kuwa ni wao tu ndio wamepewa mamlaka ya kuponyesha wengine ao kufukuza pepo wachafu? Ikiwa ni hivyo, namna gani mwanaume huyo Muyahudi amepata uwezo wa kufukuza roho waovu? Inawezekana Yohana anaona kuwa mwanaume huyo hapaswe kufanya miujiza kama hiyo kwa sababu haiko anaenda pamoja na Yesu na mitume wake.

Yohana anashangaa wakati Yesu anasema hivi: “Musijaribu kumuzuia, kwa maana hakuna mutu mwenye atafanya kazi yenye nguvu kwa musingi wa jina langu mwenye ataweza haraka kusema jambo lolote la mubaya juu yangu. Kwa maana kila mutu mwenye hatupinge iko upande wetu. Na kila mutu mwenye anawapatia kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wa Kristo, kwa kweli ninawaambia ninyi, hatapoteza zawabu yake hata kidogo.”—Marko 9:39-41.

Kwa kweli, wakati huu mwanaume huyo hana lazima ya kuwa pamoja na Kristo ili akuwe upande wake. Kutaniko la Kikristo halijaanzishwa, kwa hiyo hata kama mwanaume huyo hasafiri pamoja na Yesu hilo halimaanishe kuwa yeye ni mupinzani ao anategemeza dini ya uongo. Inaonekana wazi kuwa mwanaume huyo anaonyesha imani katika jina la Yesu, na mambo yenye Yesu anasema yanaonyesha kuwa mwanaume huyo hatapoteza zawadi yake.

Kwa upande mwingine, itakuwa mubaya sana ikiwa mwanaume huyo anakwazika kwa sababu ya maneno na matendo ya mitume. Yesu anasema hivi: “Kila mutu mwenye anamukwaza mumoja wa hawa wadogo wenye kuwa na imani, ingekuwa muzuri zaidi kwake ikiwa jiwe la kusagia lenye linazungushwa na punda lingewekwa kwenye shingo yake na atupwe katika bahari.” (Marko 9:42) Kisha, Yesu anasema kuwa wanafunzi wake wanapaswa kuondoa hata kitu fulani cha maana sana kama vile mukono, muguu, ao jicho ikiwa kitu hicho kinafanya wakwazike. Ni muzuri zaidi kuwa bila kitu chenye tunapenda sana na kuingia katika Ufalme wa Mungu kuliko kushikamana na kitu hicho na kuenda katika Gehena (Bonde la Hinomu). Inawezekana mitume wamekwisha kuona bonde hilo karibu na Yerusalemu mahali kwenye uchafu unaunguzwa, kwa hiyo wanaweza kuelewa kuwa Gehena inafananisha uharibifu wa milele.

Yesu anatoa onyo hili: “Mufanye angalisho musizarau mumoja wa hawa wadogo, kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika wao mbinguni sikuzote wanaangalia uso wa Baba yangu mwenye kuwa mbinguni.” Ni kwa kiasi gani “wadogo” hao ni wa maana sana mbele ya Baba yake? Yesu anazungumuzia mwanaume mumoja mwenye iko na kondoo 100 lakini anapoteza kondoo moja. Mwanaume huyo anaacha kondoo 99 ili kutafuta ule mumoja mwenye amepotea, na wakati anamupata, anamufurahia kuliko wale 99. Yesu anaongeza hivi: “Baba yangu mwenye kuwa mbinguni hapendi hata mumoja wa hawa wadogo aangamie.”—Matayo 18:10, 14.

Pengine Yesu anafikiria mabishano ya mitume wake ya kutaka kujua ni nani angekuwa mukubwa zaidi kati yao, wakati anatoa shauri hili: “Mukuwe na chumvi ndani yenu, na muendelee kuwa na amani mumoja na mwengine.” (Marko 9:50) Chumvi inafanya chakula kikuwe kitamu zaidi. Chumvi ya mufano inafanya mambo yenye mutu anasema yakuwe mwepesi zaidi kukubaliwa na kwa hiyo inaweza kusaidia kulinda amani, jambo lenye mabishano hayawezi kufanya.—Wakolosai 4:6.

Wakati fulani, magumu yanaweza kutokea, na Yesu anaonyesha namna ya kuyamaliza. Anasema hivi: “Kama ndugu yako anatenda zambi, uende ufunue kosa lake kati yako na yeye peke yake. Kama anakusikiliza, umemupata ndugu yako.” Utafanya nini ikiwa hasikilize? Yesu anatoa shauri hili: “Chukua pamoja na wewe mutu mumoja ao wawili zaidi, ili kila jambo lihakikishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili ao watatu (3).” Ikiwa hilo halimalize tatizo, wanapaswa kuambia “kutaniko,” ni kusema, wazee wenye wanaweza kukamata uamuzi. Sasa ikiwa mukosaji hapendi tu kusikiliza? Yesu anasema, “Akuwe kwako kama mutu wa mataifa na kama mukusanya-kodi,” watu wenye Wayahudi hawangefanya nao urafiki.—Matayo 18:15-17.

Wazee wa kutaniko wanapaswa kufuata Neno la Mungu. Ikiwa wanaona kuwa mutenda-zambi iko na kosa na ni lazima kumupatia nizamu, hukumu yao ‘imekwisha kufungwa mbinguni.’ Lakini wakati wanaona kuwa mutu hana kosa, hukumu yao itakuwa ‘imekwisha kufunguliwa mbinguni.’ Muongozo huo utakuwa wa maana kisha tu kutaniko la Kikristo kuanzishwa. Katika mazungumuzo hayo ya maana sana, Yesu anasema hivi: “Mahali kwenye watu wawili ao watatu (3) wanakusanyika pamoja katika jina langu, mimi niko pale katikati yao.”—Matayo 18:18-20.