Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 5

“Uone Mambo Maovu, Yenye Kuchukiza Yenye Wanafanya”

“Uone Mambo Maovu, Yenye Kuchukiza Yenye Wanafanya”

EZEKIELI 8:9

WAZO KUBWA: Wakaaji waasi-imani wa Yuda wanakuwa na mwenendo mupotovu ao mubaya sana na hali yao ya kiroho inaharibika

1-3. Yehova alipenda Ezekieli aone nini ku hekalu la Yerusalemu, na juu ya nini? (Ona maneno na picha ku mwanzo wa Sehemu ya 2.)

KWA SABABU yeye ni mutoto wa kuhani, Ezekieli anajua muzuri sana Sheria ya Musa. Kwa hiyo, anajua muzuri hekalu la Yerusalemu na ibada safi ya Yehova yenye inapaswa kufanywa kule. (Eze. 1:3; Mal. 2:7) Lakini sasa, mu mwaka wa 612 M.K.Y., mambo yenye kufanyika mu hekalu la Yehova inaweza kuchukiza kila Muyahudi muaminifu, na hata Ezekieli.

2 Yehova anapenda Ezekieli aone hali za mubaya sana zenye ziko ku hekalu na kisha aambie “wazee wa Yuda,” wahamishwa wenzake Wayahudi wenye kukusanyika mu nyumba yake, mambo yenye anaona. (Soma Ezekieli 8:1-4; Eze. 11:24, 25; 20:1-3) Kupitia roho takatifu, Yehova anamubeba Ezekieli (mu maono) kutoka mu nyumba yake kule Tel-abibu, karibu na muto Kebari mu Babiloni, makilometre mingi sana mangaribi mwa Yerusalemu. Yehova anamuleta ule nabii mu hekalu, ku mulango mukubwa wa kaskazini wa kiwanja cha ndani. Kuanzia pale, Yehova anamutembeza mu hekalu kupitia maono.

3 Sasa Ezekieli anaona hali ine za kuchukiza zenye kuonyesha namna hali ya kiroho ya taifa imeharibika kabisa. Ibada safi ya Yehova imekuwa mu hali gani? Na maono hii iko na maana gani kwetu leo? Acha tufuate Ezekieli mu safari yake. Lakini, mbele ya yote, tuone mambo yenye Yehova anataka waabudu wake wafanye.

“Mimi . . . Ni Mungu Mwenye Anataka Watu Washikamane Na Yeye Tu”

4. Yehova anataka waabudu wake wafanye nini?

4 Miaka 900 hivi mbele ya wakati wa Ezekieli, Yehova alionyesha waziwazi mambo yenye anataka waabudu wake wafanye. Mu amri ya pili ya zile amri kumi, aliambia Waisraeli hivi: * “Mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.” (Kut. 20:5) Kupitia maneno “watu washikamane na yeye tu,” Yehova alionyesha kama hangevumilia Waisraeli waabudu miungu ingine. Kama vile tuliona mu Sura ya 2 ya kitabu hiki, jambo la kwanza lenye ibada safi inaomba ni kwamba mupokeaji wa ibada yetu anapaswa kuwa Yehova. Waabudu wake wanapaswa kumutanguliza yeye kwanza mu maisha yao. (Kut. 20:3) Kwa kifupi, Yehova anataka waabudu wake waendelee kuwa safi kiroho kwa kuepuka kuchanga ibada safi na ibada ya uongo. Mu mwaka wa 1513 M.K.Y., Waisraeli walikubali kwa kupenda agano la Sheria. Kwa kufanya vile, walikubali kushikamana na Yehova tu. (Kut. 24:3-8) Yehova anaheshimiaka maagano yake, na anapenda pia watu wake wafanye vile.​—Kum. 7:9, 10; 2 Sa. 22:26.

5, 6. Juu ya nini Yehova tu njo mwenye Waisraeli walipaswa kushikamana naye?

5 Je, Yehova alikuwa na sheria ya kuomba Waisraeli washikamane na yeye tu? Ndiyo, kabisa! Yeye ni Mungu Mweza-Yote, Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi wa Ulimwengu Wote, na Chanzo cha uzima na Mutegemezaji wa uzima. (Zb. 36:9; Mdo. 17:28) Yehova alikuwa pia Mukombozi wa Israeli. Wakati aliwapatia zile amri kumi, alikumbusha watu hivi: “Mimi ni Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.” (Kut. 20:2) Ni wazi kwamba, Yehova tu njo alistahili kupewa nafasi ya kwanza mu mioyo ya Waisraeli.

6 Yehova habadilikake. (Mal. 3:6) Sikuzote anataka tushikamane na yeye tu. Wazia sasa namna alipaswa kujisikia juu ya zile hali ine za kuchukiza zenye alionyesha Ezekieli mu maono.

Hali ya Kwanza: Alama ya Ibada ya Sanamu ya Wivu

7. (a) Wayahudi waasi-imani walikuwa wanafanya nini ku muingilio wa kaskazini wa hekalu, na ile ilifanya Yehova atende namna gani? (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Ni mu maana gani Yehova alikuwa na wivu? (Ona maelezo.)

7 Soma Ezekieli 8:5, 6. Ezekieli alipaswa kuchukizwa sana! Ku mulango mukubwa wa kaskazini wa hekalu, Wayahudi waasi-imani walikuwa wanaabudu alama ya ibada ya sanamu, ao sanamu. Pengine ile sanamu ilikuwa muti mutakatifu wenye kufananisha Ashera, mungu mwanamuke wa uongo, mwenye Wakanaani waliona kuwa bibi ya Baali. Kama ilikuwa vile ao hapana, wale Waisraeli waabudu-sanamu walivunja mapatano yao yenye walifanya na Yehova. Kwa kupatia sanamu ibada yenye Yehova tu njo alipaswa kupewa, walifanya Mungu asikie wivu; walichokoza kasirani yake; na alikuwa na haki ya kukasirika. * (Kum. 32:16; Eze. 5:13) Waza kidogo: Kwa zaidi ya miaka 400, hekalu lilionwa kuwa makao ya Yehova. (1 Fa. 8:10-13) Lakini sasa, kwa kuingiza ibada ya sanamu mu hekalu, wale waabudu-sanamu walimufanya Yehova ‘aende mbali sana na mahali pake patakatifu.’

8. Maono ya Ezekieli juu ya ile alama ya wivu iko na maana gani kwetu leo?

8 Maono hii ya Ezekieli juu ya ile alama ya wivu iko na maana gani kwetu leo? Bila shaka, wakaaji waasi-imani wa Yuda wanafanana na watu wa Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo. Watu wa Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo wanasema kama wanamuabudu Mungu, lakini Mungu hakubali ibada yao sababu wanaabudu sanamu. Kwa kuwa Yehova habadilikake, tunaweza kuwa hakika kwamba zile Dini zote Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo, ziko zinachokoza kasirani yake ya haki, kama vile wale wakaaji waasi-imani wa Yuda. (Yak. 1:17) Kusema kweli, Yehova iko mbali sana na aina hii ya ibada yenye kuharibika sana!

9, 10. Habari ya waabudu-sanamu wenye walikuwa wanaabudu mu hekalu inatupatia onyo gani?

9 Habari ya wale waabudu-sanamu wenye walikuwa wanaabudu mu hekalu inaweza kutupatia onyo gani? Kama tunapenda kushikamana na Yehova tu, tunapaswa ‘kukimbia ibada ya sanamu.’ (1 Ko. 10:14) Pengine unaweza kusema, ‘Siwezi kutumikisha hata siku moja sanamu ao mifano mu ibada yenye namutolea Yehova!’ Lakini kuko aina mingi za ibada ya sanamu, aina fulani haziko wazi kabisa kama zingine. Kitabu kimoja chenye kuzungumuzia Biblia kinafasiria hivi ibada ya sanamu: “Inaweza kusemwa kwamba ibada ya sanamu ni usemi wa mufano wenye kumaanisha mambo ingine, ni kusema, kitu chochote cha bei sana, cha lazima sana, ao uwezo fulani wenye unakuwa wa maana sana kwetu kuliko ushikamanifu wetu kwa Mungu.” Kwa hiyo, ibada ya sanamu inaweza kumaanisha vitu vya kimwili, feza, ngono, mambo ya kujifurahisha​—ni kusema, kitu chochote chenye kinaweza kukamata nafasi ya kwanza mu maisha yetu na hivyo kutufanya tusishikamane na Yehova tu. (Mt. 6:19-21, 24; Efe. 5:5; Kol. 3:5) Tunapaswa kuepuka kila aina ya ibada ya sanamu, sababu Yehova tu njo anapaswa kuchukua nafasi ya kwanza mu mioyo yetu na ni yeye tu njo tunapaswa kuabudu!​—1 Yo. 5:21.

10 Hali ya kwanza yenye Yehova alimuonyesha Ezekieli ilikuwa na “mambo ya mubaya, yenye kuchukiza.” Lakini, Yehova alimuambia hivi nabii wake muaminifu: “Utaona mambo ya kuchukiza ya mubaya hata zaidi.” Ni mambo gani ingeweza kuwa ya mubaya zaidi kuliko ile alama ya ibada ya sanamu ya wivu mu eneo la hekalu?

Hali ya Pili: Wazee 70 Wenye Kutolea Miungu ya Uongo Uvumba

11. Ni mambo gani ya kuchukiza yenye Ezekieli aliona kisha kuingia mu kiwanja cha ndani karibu na mazabahu ya hekalu?

11 Soma Ezekieli 8:7-12. Kisha kutoboa ukuta na kuingia mu kiwanja cha ndani karibu na mazabahu ya hekalu, Ezekieli anaona ku ukuta michoro ya kuchukiza ya “viumbe vyenye kutambaa na wanyama wenye kuchukiza na sanamu zote zenye kuchukiza.” * Ile michoro ku ukuta ilifananisha miungu ya uongo. Lakini, ya kuchukiza zaidi ni ile Ezekieli anaona sasa: “Wazee makumi saba (70) wa nyumba ya Israeli” wamesimama “katika giza” na wako wanatolea miungu ya uongo uvumba. Kulingana na Sheria, kuchoma uvumba wenye kutosha harufu ya muzuri kulifananisha sala zenye kukubaliwa zenye zilitolewa na waabudu waaminifu. (Zb. 141:2) Lakini, uvumba wenye wale wazee 70 walitolea miungu ya uongo ulikuwa harufu ya mubaya sana mbele ya Yehova. Sala zao zilikuwa kama harufu ya mubaya sana kwake. (Mez. 15:8) Wale wazee walijidanganya kwa kusema: “Yehova hatuone.” Lakini Yehova alikuwa anawaona, na alimuonyesha Ezekieli mambo yenye walikuwa wanafanya kabisa mu hekalu Lake!

Yehova anaona kila kitu cha kuchukiza chenye kufanyika “katika giza” (Ona fungu la 11)

12. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu hata “katika giza,” na ni nani zaidi wanapaswa kuweka mufano muzuri kuhusu ile jambo?

12 Habari ya Ezekieli juu ya wale wazee 70 wa Israeli wenye kutolea miungu ya uongo uvumba inaweza kutufundisha nini? Kama tunapenda Mungu asikilize sala zetu na ibada yetu ionekane kuwa safi mbele yake, tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu hata “katika giza.” (Mez. 15:29) Kila siku tukumbuke kama Yehova haiko kipofu, anaona kila kitu tunafanya. Tukijua kama Yehova anatuona, hatutafanya jambo lenye litamuchukiza wakati tuko peke yetu. (Ebr. 4:13) Zaidi sana wazee wa makutaniko wanapaswa kuonyesha mufano muzuri mu kufuata kanuni za Biblia. (1 Pe. 5:2, 3) Ndugu na dada mu kutaniko wanatazamia kwamba muzee mwenye kusimama mbele yao na mwenye kuwaongoza mu ibada ku mikutano anaishi kulingana na kanuni za Biblia hata “katika giza,” ni kusema, wakati pengine hakuna mwenye anamuona.​—Zb. 101:2, 3.

Hali ya Tatu: “Wanamuke . . . Wakimulia Mungu Tamuzi”

13. Ni mambo gani Ezekieli aliona wanamuke wako wanafanya ku mulango mukubwa wa hekalu?

13 Soma Ezekieli 8:13, 14. Kisha kumuonyesha zile hali mbili za mambo ya kuchukiza, Yehova anamuambia tena hivi Ezekieli: “Utaona mambo ya kuchukiza ya mubaya hata zaidi yenye wanafanya.” Nabii Ezekieli anaona nini sasa? “Kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa kaskazini wa nyumba ya Yehova,” anaona “wanamuke wamekaa wakimulia mungu Tamuzi.” Tamuzi, mungu moja wa Mesopotamia, anaitwa Dumuzi mu maandishi ya Wasumeri na inawaziwa kwamba alikuwa bwana wa Ishtari, mungu mwanamuke wa uzazi. * Inaonekana kulia kwa wale wanamuke Waisraeli ilikuwa sehemu ya desturi fulani ya dini yenye kuhusiana na kifo cha Tamuzi. Kwa hiyo, kwa kumulia Tamuzi mu hekalu la Yehova, wale wanamuke walikuwa wanafanya desturi ya kipagani mahali pa kufanyia ibada safi. Lakini, ibada hii ya uongo haingekubaliwa juu tu ilitolewa mu hekalu la Yehova. Njo maana, kulingana na mawazo ya Yehova, wale wanamuke waasi-imani walikuwa wanafanya “mambo ya kuchukiza”!

14. Mawazo ya Yehova juu ya mambo yenye wale wanamuke waasi-imani walikuwa wanafanya inaweza kutufundisha nini?

14 Mawazo ya Yehova juu ya mambo yenye wale wanamuke walikuwa wanafanya inaweza kutufundisha nini? Kama tunapenda ibada yetu iendelee kuwa safi, hatupaswe hata kidogo kuchanga ibada safi na desturi za kipagani. Kwa hiyo, hatupaswe kufanya jambo fulani lenye kuhusiana na sikukuu zenye zilianzishwa na wapagani. Je, ni jambo la maana kujua namna zilianzaka? Ndiyo! Leo, desturi zenye kuhusiana na sikukuu fulani, kama vile Noeli na Pasaka, zinaweza kuonekana kuwa haziko za mubaya. Lakini, tusisahau kama Yehova aliona na macho yake mwanzo wa desturi za kipagani zenye zimegeuka kuwa sikukuu za leo. Yehova hakubali zile desturi juu tu watu walianza kuzifanya tangu zamani sana ao juu wamezichanga na ibada safi.​—2 Ko. 6:17; Ufu. 18:2, 4.

Hali ya Ine: Wanaume 25 Wenye ‘Kuinamia Jua’

15, 16. Wale wanaume 25 walikuwa wanafanya nini mu kiwanja cha ndani cha hekalu, na juu ya nini matendo yao ilimuchukiza sana Yehova?

15 Soma Ezekieli 8:15-18. Yehova anaanza kufasiria hali ya ine, ya mwisho, kwa kutumia maneno hii yenye Ezekieli amezoea kusikia: “Utaona mambo ya kuchukiza ya mubaya hata zaidi kuliko haya.” Pengine nabii Ezekieli alijiuliza: ‘Ni nini inaweza kuwa ya mubaya zaidi kupita ile yenye nilishaona?’ Sasa Ezekieli iko mu kiwanja cha ndani cha hekalu. Pale, ku muingilio wa mulango mukubwa wa hekalu, anaona wanaume 25 wenye kuinamia “jua kuelekea mashariki” juu ya kuiabudu. Wale wanaume wanamukasirikisha Yehova mubaya sana, tena sana. Juu ya nini tunasema vile?

16 Fikiria hali hii: Hekalu la Mungu lilijengwa likiwa na muingilio wenye kuangalia mashariki. Waabudu walikuwa wanaingia mu hekalu wakiangalia upande wa mangaribi, migongo yao ikielekea jua lenye kutokea upande wa mashariki. Lakini mu maono hii, “migongo” ya wale wanaume 25 “ilielekea hekalu” na nyuso zao ziliangalia mashariki juu waweze kuabudu jua. Kwa kufanya vile, walimugeuzia Yehova migongo yao, sababu ile hekalu ilikuwa “nyumba ya Yehova.” (1 Fa. 8:10-13) Wale wanaume 25 walikuwa waasi-imani. Walifanya sawa vile Yehova hakuwake, na walivunja amri yenye iko mu Kumbukumbu la Torati 4:15-19. Walimukasirisha kabisa Mungu mwenye tunapaswa kushikamana na yeye tu!

Yehova tu njo waabudu wake wanapaswa kushikamana naye

17, 18. (a) Habari ya waabudu wa jua wenye walikuwa wanaabudu mu hekalu inaweza kutufundisha nini? (b) Waisraeli waasi-imani waliharibisha urafiki gani, na namna gani walifanya vile?

17 Habari ya waabudu wa jua inaweza kutufundisha nini? Kama tunapenda ibada yetu iendelee kuwa safi, tunapaswa kumuomba Yehova uelewaji na hekima. Usisahau kama, “Yehova Mungu ni jua,” na Neno lake ni “mwangaza” wa njia zetu. (Zb. 84:11; 119:105) Yehova anatupatia hekima kupitia Neno lake na vichapo vyenye kutegemea Biblia vya tengenezo lake. Ile hekima inatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri kusudi tukuwe na maisha ya furaha leo na tupate uzima wa milele wakati wenye kuja. Lakini kama tunaanza kutafuta hekima ya dunia juu ya kujua namna ya kuishi, itakuwa kumugeuzia Yehova migongo yetu. Kufanya vile kutamuhuzunisha sana, kutamufanya akuwe na huzuni sana mu moyo wake. Hatupendi kumutendea vile Mungu wetu! Maono ya Ezekieli ni onyo kwetu: Tunapaswa kuepuka wale wenye kugeuzia kweli migongo yao, ni kusema, waasi-imani.​—Mez. 11:9.

18 Kama vile tuliona, Ezekieli aliona na macho yake hali ine za kuchukiza za ibada ya sanamu na ibada ya uongo yenye kuonyesha namna hali ya kiroho ya wakaaji waasi-imani wa Yuda ilikuwa imeharibika sana. Wale Waisraeli waliharibisha urafiki wao pamoja na Mungu juu walikuwa na uchafu wa kiroho. Lakini kwenye kuko uchafu wa kiroho hakukosake mwenendo muchafu. Njo maana hatushangae kuona kwamba, Waisraeli waasi-imani walifanya matendo ya mubaya ya kila rangi, yenye iliharibisha urafiki wao pamoja na Mungu na hata pia na wanadamu wenzao. Tuone sasa namna Ezekieli, akiongozwa na roho ya Mungu, anaeleza mwenendo mupotovu ao mubaya sana wa wakaaji waasi-imani wa Yuda.

Mwenendo Wenye Hauko Safi​—“Mwenendo Muchafu Katikati Yako”

19. Kulingana na Ezekieli, watu wenye walifanya agano na Yehova walikuwa wanafanya mambo gani ya mubaya sana?

19 Soma Ezekieli 22:3-12. Taifa liliharibika kuanzia ku viongozi mupaka ku watu wa kawaida. “Wakubwa,” ao viongozi, walitumia mamlaka yao juu ya kumwanga damu yenye haina kosa. Karibu watu wote walitenda kama viongozi wao kwa kuvunja Sheria ya Mungu. Mu familia, watoto walitendea wazazi wao “kwa zarau,” na ngono kati ya watu wa jamaa moja ilienea sana. Mu inchi, Waisraeli wenye kuasi walikuwa wanapunja mukaaji mugeni na kutesa mutoto mwenye hana baba na mujane. Wanaume Waisraeli walikuwa wanachafua bibi za majirani wao. Watu walikuwa na pupa sana: Waliomba rushwa ao kata-midomo, walipunja wengine, na walitafuta faida ya juu sana mu mambo ya kukopeshana. Yehova alihuzunika sana kuona namna watu wenye alifanya nao agano walikanyanga-kanyanga sheria zake kimakusudi na namna walishindwa kuelewa kwamba Yehova aliwapatia zile sheria juu aliwapenda! Mwenendo wao mubaya ulimuletea Yehova uchungu sana. Njo maana Yehova alituma Ezekieli awaambie hivi wale watu wenye mwenendo mubaya: “Umenisahau kabisa.”

Kwa kuchochewa na Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo, dunia inaendelea kuzama mu jeuri na mwenendo mupotovu (Ona fungu la 20)

20. Juu ya nini tunaweza kusema kwamba maneno ya Ezekieli kuhusu mwenendo muchafu wa wakaaji wa Yuda iko na maana kwetu leo?

20 Juu ya nini tunaweza kusema kwamba maneno ya Ezekieli kuhusu mwenendo mupotovu ao mubaya sana wa wakaaji wa Yuda iko na maana kwetu leo? Mwenendo mupotovu wa wakaaji waasi-imani wa Yuda unafanana na mwenendo mupotovu wenye uko mu dunia yenye tunaishi ndani leo. Viongozi wa guvernema wametumia mubaya mamlaka yao na wametesa sana watu wa kawaida. Viongozi wa dini​—zaidi sana, wale wa Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo—​wamebariki vita za mataifa zenye zimeua mamilioni ya watu. Viongozi wa dini wamepunguza uzito wa kanuni za Biblia zenye kuwa safi na wazi kuhusu ngono. Ile imefanya mwenendo wa watu mu dunia uendelee kuharibika sana. Bila shaka, Yehova anaweza kuambia Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo mambo yenye aliambiaka wakaaji waasi-imani wa Yuda: “Umenisahau kabisa.”

21. Habari juu ya mwenendo muchafu wa wakaaji wa Yuda ya zamani inaweza kutufundisha nini?

21 Habari juu ya mwenendo mupotovu wa wakaaji wa Yuda ya zamani inaweza kutufundisha nini, sisi watu wa Yehova? Kama tunapenda kumuabudu Yehova namna anakubali, tunapaswa kuendelea kuwa na mwenendo safi mu mambo yote. Haiko mwepesi kufanya vile mu dunia hii yenye kuharibika. (2 Ti. 3:1-5) Lakini, tunajua mawazo ya Yehova juu ya aina zote za mubaya za mwenendo mupotovu ao mubaya sana. (1 Ko. 6:9, 10) Tunatii kanuni za Yehova kuhusu mwenendo juu tunamupenda na juu tunapenda kanuni zake. (Zb. 119:97; 1 Yo. 5:3) Kama tunakuwa na mwenendo muchafu, ile itaonyesha kama hatumupende Mungu wetu mutakatifu na musafi. Hatupendi kumupatia Yehova sababu ya yeye kusema hivi juu yetu: “Umenisahau kabisa.”

22. (a) Kisha kuchunguza maelezo ya Yehova juu ya wakaaji wa Yuda ya zamani, unaazimia kufanya nini? (b) Tutazungumuzia nini mu sura ya kufuata?

22 Kuchunguza maelezo ya Yehova juu ya hali ya kiroho yenye kuharibika ya wakaaji wa Yuda na juu ya mwenendo wao mupotovu ao mubaya sana kumetupatia somo za maana sana. Kwa kweli tunatiwa moyo kuendelea kushikamana na Yehova tu sababu yeye njo anastahili ibada yetu. Juu tufikie kufanya vile, tunapaswa kuepuka kila aina ya ibada ya sanamu na kuendelea kuwa na mwenendo safi. Sasa, Yehova alitendea namna gani watu wake wenye hawakukuwa washikamanifu? Wakati nabii Ezekieli alimaliza kuona mambo yenye ilikuwa inatendeka mu hekalu, Yehova alimuambia waziwazi hivi: “Nitatenda katika kasirani kali.” (Eze. 8:17, 18) Tunapenda kujua mambo yenye Yehova alitendea wakaaji wa Yuda wenye hawakukuwa washikamanifu, sababu kuko hukumu ingine yenye kufanana na ile yenye itapata dunia yenye kuharibika. Sura ya kufuata itazungumuzia namna hukumu za Yehova juu ya Yuda zilitimia.

^ fu. 4 Mu kitabu cha Ezekieli, neno “Israeli” linatumiwa mara mingi juu ya kumaanisha wakaaji wa Yuda na wa Yerusalemu.​—Eze. 12:19, 22; 18:2; 21:2, 3.

^ fu. 7 Kutumiwa kwa neno “wivu” kunaonyesha kama Yehova anaona uaminifu kwake kuwa jambo la maana sana. Tunaweza kuwazia namna bwana anaweza kusikia wivu sana wakati bibi yake haiko muaminifu kwake. (Mez. 6:34) Kama vile ule mwanaume, Yehova iko na haki ya kukasirika wakati watu wake wanaonyesha kama hawako waaminifu kwa kuabudu sanamu. Kitabu kimoja kinasema: “Wivu wa Mungu . . . unatokana na utakatifu Wake. Sababu Yeye peke yake njo Mutakatifu . . . , Hatavumilia ushindani.”​—Kut. 34:14.

^ fu. 11 Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “sanamu zenye kuchukiza” linahusiana na neno lingine la Kiebrania lenye kumaanisha “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

^ fu. 13 Hakuna musingi wowote wa kweli kabisa wenye kuonyesha kama Tamuzi ni jina lingine la Nimrodi.