SURA YA TANO
Zabihu ya Ukombozi Ndiyo Zawadi ya Mungu Iliyo Nzuri Kuliko Zote
-
Zabihu ya ukombozi ni nini?
-
Zabihu hiyo ilitolewa namna gani?
-
Inaweza kukuletea faida gani?
-
Namna gani unaweza kuonyesha shukrani kwa ajili ya zabihu hiyo?
1, 2. (a) Ili zawadi iwe nzuri inaomba itimize nini? (b) Sababu gani zabihu ya ukombozi ndiyo zawadi nzuri zaidi unayohitaji?
NI ZAWADI gani nzuri zaidi ambayo umekwisha kupokea? Ili zawadi iwe nzuri si lazima iwe ya bei kali. Wala si feza ulizotoa ili kuinunua ndiyo zitaifanya iwe nzuri. Lakini, zawadi nzuri ni ile inayokuletea furaha ao kumaliza shida fulani uliyokuwa nayo.
2 Kuna zawadi nyingi ambazo unaweza kufurahia, lakini kuna moja tu iliyo nzuri zaidi kuliko zawadi zote. Ni ile ambayo Mungu alitolea wanadamu. Yehova ametupatia zawadi nyingi, lakini zawadi nzuri kuliko zote ni zabihu ya ukombozi, yaani, uzima ambao Mwana wake, Yesu Kristo alitoa. (Mathayo 20:28) Kama tutakavyojifunza katika sura hii, zabihu ya ukombozi ni zawadi ya maana zaidi unayohitaji, kwa sababu inaweza kukuletea furaha nyingi na kumaliza shida zako zote. Kwa kweli, zabihu ya ukombozi ndilo jambo kubwa ambalo Yehova alitufanyia ili kutuonyesha upendo wake.
ZABIHU YA UKOMBOZI NI NINI?
3. Zabihu ya ukombozi ni nini, na ili kuelewa kabisa maana ya fundisho hilo ni lazima tujue kwanza nini?
3 Kwa kifupi, zabihu ya ukombozi ni njia ambayo Yehova alitumia ili kuwaokoa wanadamu kutoka katika zambi na kifo. (Waefeso 1:7) Ili kuelewa maana ya fundisho hilo la Biblia, ni lazima tujue kwanza mambo yaliyotendeka katika bustani ya Edeni. Ikiwa tunajua kile Adamu alipoteza alipofanya zambi, tutajua kwa nini zabihu ya ukombozi ni zawadi nzuri sana kwetu.
4. Adamu alikuwa na uzima wa namna gani kwa kuwa alikuwa mukamilifu?
4 Yehova alipomuumba Adamu, alimutolea kitu cha maana kabisa, yaani, uzima mukamilifu. Hilo linamaanisha kama aliumbwa akiwa na mwili mukamilifu na akili yenye kukamilika; kwa hiyo, hangeweza kugonjwa, kuzeeka, wala kufa. Tena, kwa sababu alikuwa mutu mukamilifu, alikuwa na uhusiano wa pekee pamoja na Yehova. Biblia inasema kama Adamu alikuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Kwa hiyo, uhusiano wa Adamu pamoja na Yehova Mungu ulikuwa kama vile uhusiano wa mutoto pamoja na baba yake mwenye upendo. Yehova alikuwa akizungumuza na Adamu, alimupa kazi nzuri ya kufanya na alimuambia mambo aliyopenda afanye.—Mwanzo 1:28-30; 2:16, 17.
5. Biblia inamaanisha nini inaposema kama Adamu aliumbwa ‘kwa mufano wa Mungu’?
5 Adamu aliumbwa ‘kwa mufano wa Mungu.’ (Mwanzo 1:27) Hilo halimaanishi kama alikuwa kama Mungu. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 1, Yehova ni roho na hawezi kuonekana. (Yohana 4:24) Kwa hiyo, Yehova hana mwili kama wetu. Kuumbwa kwa mufano wa Mungu kunamaanisha kama Adamu aliumbwa akiwa na sifa kama zile za Mungu; kama vile upendo, haki, hekima na nguvu. Adamu aliumbwa kwa mufano wa Baba yake katika njia nyingine ya maana, aliumbwa na uhuru wa kuchagua. Hakuwa kama mashini inayofanya tu kazi bila kuwaza. Adamu angeweza kuamua, yaani, kuchagua kati ya mema na mabaya. Ikiwa angechagua kumutii Mungu, angeishi milele katika Paradiso duniani.
6. Adamu alipoteza nini alipokosa kumutii Mungu, na hilo liliwaletea watoto wake nini?
6 Kwa hiyo, Adamu alipokosa kumutii Mungu, alihukumiwa kifo; alipoteza kitu cha maana sana. Alipoteza uzima wake mukamilifu na faida zote za uzima huo. (Mwanzo 3:17-19) Jambo la huzuni ni hili: Adamu alipotezea pia watoto wake uzima mukamilifu. Neno la Mungu linasema hivi: ‘Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ (Waroma 5:12) Kwa kweli, sisi wote tumeriti zambi kutoka kwa Adamu. Biblia inasema kama Adamu ‘alijiuzisha’ pamoja na watoto wake katika utumwa wa zambi na kifo. (Waroma 7:14) Kwa sababu Adamu na Eva walikosa kumutii Mungu kwa makusudi, walipoteza mambo yote. Lakini, sisi watoto wao tuna tumaini gani?
7, 8. Ukombozi unamaanisha mambo gani mawili?
7 Yehova aliwaokoa wanadamu kupitia zabihu ya ukombozi. Ukombozi unamaanisha nini? Ukombozi unamaanisha mambo mawili. Kwanza, ni bei inayolipwa ili kukomboa ao kurudisha kitu fulani. Unaweza kulinganishwa na bei inayolipwa ili kukomboa ao kumurudisha mutu aliyekamatwa katika vita. Pili, ukombozi ni bei inayofunika, ao kulipia garama ya kitu fulani. Ni sawa na bei ambayo mutu analipa anapoharibisha kitu fulani. Kwa mufano, ikiwa mutu anaharibisha kitu fulani, anaweza kuombwa alipe hesabu fulani ya feza inayolingana kabisa na bei ya kitu alichoharibisha.
8 Namna gani ingewezekana kulipia kitu cha lazima sana ambacho Adamu aliharibu na hivyo kukomboa wanadamu kutoka katika zambi na kifo? Acheni tujifunze juu ya zabihu hiyo ya ukombozi na namna wewe unavyoweza kufaidika nayo.
NAMNA YEHOVA ALIVYOTOA ZABIHU YA UKOMBOZI
9. Ni zabihu ya ukombozi ya namna gani iliyoombwa?
9 Kwa sababu Adamu alipoteza uzima mukamilifu, mwanadamu asiyekamilika hangeweza kuukomboa. (Zaburi 49:7, 8) Kitu kilichohitajiwa ni bei ya ukombozi inayolingana na bei ya kile kilichopotezwa. Hilo linapatana na kanuni hii ya haki inayopatikana katika Neno la Mungu: “Uzima kwa uzima.” (Kumbukumbu la Torati 19:21, La Sainte Bible en Swahili de la R. D. Congo) Basi, ni nini ingeweza kulipia uzima mukamilifu ambao Adamu alipoteza? Kilichoombwa ni zabihu ya ukombozi “inayolingana” na uzima mwingine mukamilifu wa kibinadamu.—1 Timotheo 2:6.
10. Namna gani Yehova alitoa zabihu ya ukombozi?
10 Namna gani Yehova alitoa zabihu ya ukombozi? Alimutuma mumoja wa wana wake hapa duniani. Lakini Yehova alichagua na kumutuma tu Mwana wake muzaliwa-pekee, mupendwa wake. (1 Yohana 4:9, 10) Mwana huyo alikubali bila kunungunika kuacha makao yake ya mbinguni. (Wafilipi 2:7) Kama tulivyojifunza katika Sura ya 2, Yehova alifanya muujiza; alihamisha uzima wa Mwana wake na kuutia katika tumbo la uzazi la Maria. Kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu, Yesu alizaliwa mwanadamu mukamilifu na hakuriti zambi hata kidogo.—Luka 1:35.
Yehova alitoa Mwana wake muzaliwa-pekee ili awe zabihu ya ukombozi kwa ajili yetu
11. Namna gani mutu mumoja angeweza kuwa zabihu ya ukombozi kwa ajili ya watu wengi?
11 Namna gani mutu mumoja angeweza kuwa zabihu ya ukombozi kwa ajili ya wanadamu wengi? Ungali unakumbuka, namna gani wanadamu hao wote walipata kuwa wenye zambi? Usisahau kama Adamu alipofanya zambi, alipoteza 1 Wakorintho 15:45) Hivyo, Yesu alichukua mahali pa Adamu ili atuokoe. Kwa kumutii Mungu katika mambo yote na kutoa uzima wake mukamilifu, Yesu alilipa kile kilichohitajiwa kwa ajili ya zambi ya Adamu. Kwa kufanya hivyo, Yesu aliwapa watoto wa Adamu tumaini.—Waroma 5:19; 1 Wakorintho 15:21, 22.
jambo la lazima sana, yaani, uzima mukamilifu. Kwa hiyo, watoto wake hawangeweza kuriti uzima huo mukamilifu. Waliriti tu zambi na kifo. Yesu, ambaye Biblia inaita “Adamu wa mwisho,” alikuwa na uzima mukamilifu wa kibinadamu, na hakufanya zambi hata kidogo. (12. Yesu alionyesha nini kwa kuvumilia mateso makali?
12 Biblia inaeleza mateso ambayo Yesu alivumilia mbele ya kufa. Alipigwa mijeledi, akatundikwa kinyama, na kufa kwa maumivu makali kwenye muti wa mateso. (Yohana 19:1, 16-18, 30; Nyongeza, ukurasa wa 204-206) Kwa nini ilikuwa lazima Yesu ateseke sana hivyo? Katika sura nyingine ya kitabu hiki, tutaona kuwa Shetani alitilia shaka kuwa hakuna mutumishi wa Yehova anayeweza kubaki mwaminifu akijaribiwa. Kwa kuvumilia kwa uaminifu mateso makali, Yesu alijibu mashitaka hayo ya Shetani. Yesu alionyesha wazi kama mwanadamu mukamilifu aliye na uhuru wa kuchagua anaweza kubaki mwaminifu kwa Mungu hata Shetani afanye nini. Kwa kweli, Yehova alifurahia sana uaminifu wa Mwana wake mupendwa!—Methali 27:11.
13. Zabihu ya ukombozi ililipwa namna gani?
13 Zabihu ya ukombozi ililipwa namna gani? Tarehe 14 mwezi wa Nisani, mwaka wa 33, Mungu aliacha Mwana wake mukamilifu asiye na zambi auawe. Hivyo, Yesu alitoa uzima wake mukamilifu wa kibinadamu kuwa zabihu “mara moja kwa wakati wote.” (Waebrania 10:10) Siku ya tatu baada ya kifo chake, Yehova alimufufua kuwa kiumbe cha kiroho. Yesu aliporudi mbinguni, alimupa Mungu bei ya uzima wake mukamilifu wa kibinadamu kuwa zabihu ya ukombozi kwa ajili ya watoto wa Adamu. (Waebrania 9:24) Yehova alikubali bei ya zabihu ya Yesu kuwa ukombozi uliohitajiwa ili kuwakomboa wanadamu.—Waroma 3:23, 24.
NAMNA UNAVYOWEZA KUFAIDIKA NA ZABIHU YA UKOMBOZI
14, 15. Tunapaswa kufanya nini ili ‘tusamehewe zambi zetu’?
14 Ijapokuwa hatukamiliki, tunaweza kufaidika sana na zabihu ya ukombozi. Acheni tuzungumuzie namna tunavyoweza kufaidika leo na pia wakati ujao na zawadi hiyo ya Mungu iliyo nzuri kuliko zawadi zingine zote.
15 Tunaweza kusamehewa zambi. Kwa sababu tumeriti kutokamilika, si vyepesi kufanya yaliyo sawa. Tunafanya zambi kwa maneno na kwa matendo. Hata hivyo, kupitia zabihu ya ukombozi ya Yesu, tunaweza ‘kusamehewa zambi zetu.’ (Wakolosai 1:13, 14) Lakini, ili Mungu atusamehe tunapaswa kutubu kwelikweli. Tena, tunapaswa kumulilia Yehova kwa unyenyekevu na kumuomba atusamehe kwa kuwa tunaamini zabihu ya ukombozi ya Mwana wake.—1 Yohana 1:8, 9.
16. Ni nini inayotusaidia kumuabudu Mungu kwa zamiri safi, na kuwa na zamiri safi kunatuletea faida gani?
16 Tunaweza kuwa na zamiri safi mbele za Mungu. Zamiri yenye kumuhukumu mutu inaweza kumufanya akose tumaini na ajisikie kama hafai kitu. Lakini kupitia zabihu ya ukombozi, tunasamehewa zambi zetu, kwa hiyo, kwa fazili, Yehova anatuwezesha tumuabudu tukiwa na zamiri safi hata ikiwa sisi ni watu wasio wakamilifu. (Waebrania 9:13, 14) Tunaweza kuzungumuza na Yehova bila woga. Tunaweza kumukaribia katika sala bila kujihukumu. (Waebrania 4:14-16) Kuendelea kuwa na zamiri safi kunatufanya tuwe na amani ya akili, tuwe na furaha na kujisikia kuwa watu wenye kuheshimika.
17. Kwa sababu Yesu alikufa kwa ajili yetu, tunaweza kupata baraka gani?
Waroma 6:23 linasema: ‘Mushahara ambao zambi inalipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu anatoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.’ Katika Sura ya 3, tulizungumuzia baraka ambazo tutapata katika Paradiso duniani wakati ujao. (Ufunuo 21:3, 4) Tutapata baraka hizo zote, pia uzima wa milele na afya kamilifu, kwa sababu Yesu alikufa kwa ajili yetu. Ili kupata baraka hizo, tunapaswa kuonyesha kama sisi ni wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya zabihu ya ukombozi.
17 Tuna tumaini la kupata uzima wa milele katika Paradiso duniani. Andiko laNAMNA GANI UNAWEZA KUONYESHA SHUKRANI YAKO?
18. Sababu gani tunapaswa kumushukuru Yehova juu ya zabihu ya ukombozi?
18 Sababu gani tunapaswa kumushukuru Yehova sana juu ya zabihu ya ukombozi? Zawadi ni ya lazima sana ikiwa mutoaji amefanya yote awezayo ili kuitoa. Tunaguswa moyo sana tunapoona kama rafiki anatutolea zawadi kwa sababu anatupenda kabisa. Zabihu ya ukombozi ndiyo zawadi inayopita zingine zote, kwa sababu Mungu alijinyima mambo mengi ili kuitoa. Andiko la Yohana 3:16 linasema hivi: ‘Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee.’ Zabihu ya ukombozi ndilo jambo kubwa linaloonyesha kama Yehova anatupenda. Inaonyesha pia kama Yesu anatupenda sana, kwa kuwa alikubali, bila kunungunika, kutoa uzima wake. (Yohana 15:13) Hivyo, zawadi hiyo inapaswa kutusadikisha kama Yehova na Mwana wake wanamupenda kila mumoja wetu.—Wagalatia 2:20.
Kujifunza zaidi juu ya Yehova kunaonyesha shukrani yetu juu ya zawadi ya Mungu ya ukombozi
19, 20. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya zawadi ya ukombozi?
19 Basi, namna gani unaweza kuonyesha shukrani yako juu ya zawadi hiyo ya Mungu? Kwanza, jikaze kujifunza zaidi juu ya Yehova, Mutoaji Mukubwa wa zawadi hiyo. (Yohana 17:3) Kujifunza Biblia kupitia kitabu hiki kutakusaidia umujue zaidi. Kadiri unavyoendelea kumujua Yehova, ndivyo utamupenda zaidi. Na upendo huo utakuchochea ufanye mambo yanayomupendeza.—1 Yohana 5:3.
20 Onyesha kama unaamini zabihu ya ukombozi ya Yesu. Biblia inasema hivi: ‘Yule anayemuamini Mwana ana uzima wa milele.’ (Yohana 3:36) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamuamini Yesu? Imani kama hiyo haionyeshwi kwa maneno tu. Andiko la Yakobo 2:26 linasema kama “imani bila matendo imekufa.” Ndiyo, imani ya kweli inaonyeshwa kwa “matendo.” Tunaweza kuonyesha kama tunamuamini Yesu kwa kujikaza kumuiga kupitia maneno yetu na matendo yetu.—Yohana 13:15.
21, 22. (a) Sababu gani tunapaswa kuhuzuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu unaofanywa kila mwaka? (b) Sura ya 6 na ya 7 itazungumuzia jambo gani?
21 Huzuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu unaofanywa kila mwaka. Mangaribi ya Nisani 14, mwaka wa 33, Yesu alianzisha mwazimisho ambao Biblia inaita “Mulo wa jioni wa Bwana.” (1 Wakorintho 11:20; Mathayo 26:26-28) Unaitwa pia Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Yesu alianzisha mwazimisho huo ili mitume wake na Wakristo wote wa kweli waendelee kukumbuka kama kupitia kifo chake, alitoa nafsi yake ao uzima wake kuwa zabihu ya ukombozi. Juu ya mwazimisho huo, Yesu aliamuru hivi: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Kutii amri hiyo ya Yesu juu ya Ukumbusho kunatusaidia kukumbuka upendo mwingi ambao Yehova na Yesu walionyesha kwa kututolea zabihu ya ukombozi. Tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya zabihu hiyo kwa kuhuzuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu unaofanywa kila mwaka. *
22 Kwa kweli, zabihu ya ukombozi ambayo Yehova alitutolea ni zawadi ya lazima sana. (2 Wakorintho 9:14, 15) Hata watu ambao wamekufa wanaweza kufaidika na zawadi hiyo. Sura ya 6 na ya 7 itazungumuzia jambo hilo.
^ fu. 21 Ili kupata habari zaidi juu ya Chakula cha Jioni cha Bwana, soma Nyongeza, ukurasa wa 206-208.