Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | SHETANI ANAKUWAKA KABISA?

Shetani Anakuwaka?

Shetani Anakuwaka?

Sanamu katika muji wa Madrid, Hispania, inayomuonyesha Shetani kuwa malaika mubaya, aliyeasi

“Nilikomalia katika inchi ya El Salvador. Wakati nilikosa utii, mama alikuwa ananiambia, ‘Shetani atakuja kukukamata!’ Na nilikuwa ninajibia, ‘Acha akuje!’ Nilimuamini Mungu, lakini sikumuamini Shetani.”—ROGELIO.

Wewe pia uko kama kijana Rogelio? Kati ya mawazo yenye kufuata, ni wazo gani unaona kuwa lenye kufaa?

  • Shetani hakuwake; ni alama tu ya ubaya.

  • Shetani anakuwaka, lakini hahangaikie watu.

  • Shetani ni kiumbe wa roho mwenye nguvu anayechochea sana watu.

Kila wazo kati ya mawazo hayo, watu fulani wanaliamini, labda mamilioni ya watu. Lakini, ni jambo la maana kabisa kujua ni wazo gani lililo la kweli? Kwa kweli, ikiwa Shetani hakuwake, watu wanaokubali kama anakuwaka wanadanganyika. Ikiwa Shetani anakuwaka lakini hahangaikie watu, watu wengi wanakuwa waangalifu ao wanaogopa bila sababu. Hata hivyo, ikiwa Shetani ni kiongozi mudanganyifu, basi yeye ni hatari sana kuliko vile watu wengi wanawazia.

Tuone basi namna Maandiko Matakatifu yanajibia maulizo haya: Shetani ni nini ao ni nani—ni alama ya ubaya ao ni mutu wa roho? Ikiwa Shetani ni mutu, iko hatari kwako? Ikiwa iko hatari, namna gani unaweza kujilinda?