MAZUNGUMUZO YA BIBLIA PAMOJA NA JIRANI Ufalme wa Mungu
Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 1)
Habari inayofuata ni mufano wa mazungumuzo ambayo Shahidi wa Yehova fulani anaweza kuwa nayo pamoja na jirani yake. Kwa mufano, Shahidi fulani anayeitwa Richard anamukuta mwanaume anayeitwa Jon nyumbani kwake.
‘ENDELEA KUTAFUTA’ UELEWAJI
Richard: Jon, nimefurahia sana mazungumuzo ya kawaida yenye tunazoea kuwa nayo juu ya Biblia. * Tulipozungumuza wakati uliopita, ulitokeza ulizo juu ya Ufalme wa Mungu. Uliuliza sababu gani Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba Ufalme wa Mungu ulianza kutawala katika mwaka wa 1914.
Jon: Ndiyo, nilikuwa ninasoma kitabu chenu kimoja, na kilisema kwamba Ufalme wa Mungu ulianza kutawala katika mwaka wa 1914. Hilo liliniletea hamu ya kujua mengi kwa sababu munasema kwamba mambo yote munaamini yanategemea Biblia.
Richard: Hiyo ni kweli.
Jon: Sawa, nilisoma Biblia yote mimi mwenyewe. Lakini hakuna andiko niliona linataja mwaka wa 1914. Kwa hiyo nilifungua Biblia kwenye Internete na nikatafuta andiko lenye kuwa na mwaka wa “1914,” lakini mwaka huo haukupatikana nafasi yoyote katika maandiko.
Richard: Jon, ninakusifu kwa mambo mawili. Kwanza, ninakusifu kwamba umesoma Biblia nzima. Hilo linaonyesha kuwa unapenda kabisa Neno la Mungu.
Jon: Ni kweli. Hakuna kitabu kinachoweza kulinganishwa na Biblia.
Richard: Ninakubaliana na wewe. Tena, ninakusifu kuona namna unachunguza Biblia wakati unapenda kupata majibu ya maulizo yako. Unafanya kabisa-kabisa mambo Biblia inatutia moyo tufanye: ‘Endelea kutafuta’ uelewaji. * Ni vizuri kuona unajikaza kufanya vile.
Jon: Asante. Ninataka kuendelea kujifunza. Kwa kweli, nilitafuta tena zaidi na nikapata maelezo fulani juu ya mwaka wa 1914 katika kitabu hiki chenye tunajifunza. Kinazungumuzia ndoto yenye mufalme aliota—ndoto hiyo ilikuwa inahusu muti mukubwa uliokatwa na kuota tena ao kitu kama hicho.
Richard: Ni kweli. Huo ni unabii unaotajwa katika Danieli sura ya 4. Unahusu ndoto yenye Mufalme Nebukadneza wa Babiloni aliota.
Jon: Ndiyo, ni vile. Nilisoma unabii huo tena na tena. Lakini kusema kweli, kufikia sasa sijaona namna unabii huo unapatana na Ufalme wa Mungu ao mwaka wa 1914.
Richard: Jon, kwa kweli, hata nabii Danieli hakuelewa maana kabisa ya mambo hayo aliyoandika akiongozwa na roho ya Mungu!
Jon: Kweli?
Richard: Ndiyo. Hapa katika andiko la Danieli 12:8 anasema hivi: “Mimi nami nikasikia, lakini sikuweza kuelewa.”
Jon: Maana yake haiko mimi mwenyewe. Hilo linanitia moyo.
Richard: Ukweli ni kwamba, Danieli hakuelewa kwa sababu wakati wa Mungu wa kufunulia watu waziwazi maana kabisa ya unabii wa kitabu cha Danieli ulikuwa haujafika. Lakini leo, wakati wetu, tunaweza kuelewa unabii huo vizuri zaidi.
Jon: Sababu gani unasema vile?
Richard: Ona jambo lenye tunasoma katika mustari unaofuata. Danieli 12:9 inasema hivi: ‘Maneno hayo yamewekwa siri na kufungwa kwa muhuri mupaka wakati wa mwisho.’ Kwa hiyo, unabii huu mbalimbali ungeeleweka miaka mingi kisha hapo, katika kipindi cha “wakati wa mwisho.” Na kama tutakavyochunguza karibuni katika funzo letu la Biblia, mambo mbalimbali yanaonyesha kwamba tunaishi sasa katika kipindi hicho cha wakati. *
Jon: Sasa, unaweza kunifasiria unabii huo wa Danieli?
Richard: Nitajikaza kufanya vile.
NDOTO YA NEBUKADNEZA
Richard: Ili kuanza, acha nieleze kwa kifupi mambo Mufalme Nebukadneza aliona katika ndoto yake. Kisha tutazungumuzia yanamaanisha nini.
Jon: Sawa.
Richard: Katika ndoto, Nebukadneza aliona muti mukubwa ambao ulifikia mupaka mbinguni. Kisha akasikia malaika wa Mungu anaamuru kwamba muti huo ukatwe. Lakini, Mungu alisema kwamba kisiki chake kiachwe katika udongo. Kisha kipindi cha “nyakati saba,” muti huo ungeota tena. * Kwanza unabii huo ulitimia juu ya Mufalme Nebukadneza mwenyewe. Hata ikiwa alikuwa mufalme mwenye nguvu zaidi, kama vile muti wenye kuonekana kuwa unafika mbinguni, alikatwa kwa “nyakati saba.” Unakumbuka mambo yaliyotokea?
Jon: Hapana, sikumbuke.
Richard: Hakuna shida. Biblia inasema kwamba Nebukadneza alirukwa na akili, inawezekana kwa miaka saba. Katika kipindi hicho, hakuwa na uwezo wa kutawala kama mufalme. Lakini nyakati hizo saba zilipoisha, Nebukadneza alirudiwa na akili na akaanza tena kutawala. *
Jon: Sawa, kufikia hapa ninaelewa mambo umesema. Lakini mambo hayo yote yanapatana namna gani na Ufalme wa Mungu na mwaka wa 1914?
Richard: Kwa kifupi, unabii huu uko na utimizo mbili. Ulitimizwa mara ya kwanza wakati utawala wa Mufalme Nebukadneza ulikatizwa. Ulitimizwa mara ya pili wakati utawala wa Mungu ulikatizwa. Kwa hiyo ni utimizo wa pili ndio unapatana na Ufalme wa Mungu.
Jon: Unajua namna gani kwamba unabii huo uko na utimizo wa pili unaopatana na Ufalme wa Mungu?
Richard: Sababu moja ni kwamba, tunapata maelezo katika unabii huo wenyewe. Kulingana na Danieli 4:17, unabii huo ulitolewa ‘kusudi watu wanaoishi wajue kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mutawala katika ufalme wa wanadamu na kwamba anamupa yeyote yule anayetaka ufalme huo.’ Umeona katika andiko hilo maneno “ufalme wa wanadamu”?
Jon: Ndiyo, andiko hilo linasema kwamba ‘Aliye Juu Zaidi ni Mutawala katika ufalme wa wanadamu.’
Richard: Ni vile kabisa. Unawaza ule “Aliye Juu Zaidi” ni nani?
Jon: Ninawaza andiko hilo linazungumuzia Mungu.
Richard: Unasema kweli. Kwa hiyo, maelezo hayo ndiyo yanatuonyesha kwamba unabii huo haumuhusu tu Nebukadneza. Ulihusu pia “ufalme wa wanadamu,” ni kusema, utawala wa Mungu juu ya watu. Na tunapochunguza mistari inayozunguka unabii huo tunaona kwamba wazo hilo linapatana na akili.
Jon: Unamaanisha nini?
WAZO KUBWA LA KITABU HICHO
Richard: Kitabu cha Biblia cha Danieli kinazungumuzia habari fulani tena na tena. Kitabu hicho kinazungumuzia mara nyingi kuwekwa kwa Ufalme wa Mungu chini ya utawala wa Mwana wake, Yesu. Kwa mufano, acha turuke sura mbili tukirudia nyuma. Tafazali, unaweza kusoma Danieli 2:44?
Jon: Sawa. Inasema hivi: ‘Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mupaka wakati usio na kipimo.’
Richard: Aksante kwa usomaji wako. Unawaza andiko hili linazungumuzia Ufalme wa Mungu?
Jon: Hmm. Sina uhakika.
Richard: Sawa, ona kwamba andiko hili linasema kuwa Ufalme huo “utasimama mupaka wakati usio na kipimo.” Maneno hayo yanahusu tu Ufalme wa Mungu, lakini hatuwezi kusema kwamba yanahusu serikali yoyote ya watu, sivyo?
Jon: Ninawaza ni vile kabisa.
Richard: Ona unabii mwingine katika kitabu cha Danieli unaozungumuzia Ufalme wa Mungu. Ni unabii wenye kuwa katika Danieli 7:13, 14. Unabii huo unasema hivi juu ya mutawala wa wakati unaokuja: ‘Akapewa utawala na heshima na ufalme, ili vikundi vyote vya watu, vya mataifa na luga vimutumikie yeye. Utawala wake ni utawala unaodumu mupaka wakati usio na kipimo ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake ni ufalme ambao hautaharibiwa.’ Kuna jambo fulani katika unabii huu ambalo tayari unajua?
Jon: Unabii huo unazungumuzia ufalme.
Richard: Hilo ni kweli. Na haiko tu ufalme wowote. Ona kwamba andiko hili linasema kuwa Ufalme huo utakuwa na mamlaka juu ya “vikundi vyote vya watu, vya mataifa na luga.” Kwa maneno mengine, Ufalme huo ungetawala juu ya dunia yote.
Jon: Sikuwa nafikiria kuwa hiyo ndiyo maana ya andiko hilo, lakini unasema kweli. Andiko hilo linasema hivyo kabisa.
Richard: Tena, ona mambo mengine unabii huo unasema: ‘Utawala wake ni utawala unaodumu mupaka wakati usio na kipimo ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake ni ufalme ambao hautaharibiwa.’ Unakubali sasa kwamba unabii huu unapatana na unabii ambao tunatoka kusoma katika Danieli 2:44?
Jon: Ndiyo, unapatana.
Richard: Acha tujikumbushe kwa kufupi mambo tulizungumuzia huko mbele. Unabii katika Danieli sura ya 4 ulitolewa ili watu wajue kwamba “Aliye Juu Zaidi ni Mutawala katika ufalme wa wanadamu.” Maneno hayo yenyewe yanaonyesha waziwazi kwamba unabii huo ulikuwa na utimizo mukubwa zaidi ya utimizo moja uliohusu Nebukadneza. Na katika kitabu chote cha Danieli, kuna unabii mbalimbali juu ya kuwekwa kwa Ufalme wa Mungu chini ya utawala wa Mwana wake. Je, unafikiri ni sawa tumalizie kwa kusema kwamba unabii huu ulio katika Danieli sura ya 4 unahusu pia Ufalme wa Mungu?
Jon: Ninafikiri hivyo. Lakini sijaona namna gani unapatana na mwaka wa 1914.
“NYAKATI SABA ZIPITE”
Richard: Sawa, acha tuzungumuzie tena Mufalme Nebukadneza. Alifananishwa na muti katika utimizo wa kwanza wa unabii huo. Utawala wake ulikatizwa wakati muti huo ulikatwa na kuachwa kwa nyakati saba, ni kusema, wakati alirukwa na akili kwa kipindi fulani cha wakati. Kipindi hicho cha nyakati saba kiliisha wakati Nebukadneza alirudiwa na akili na kurudilia utawala wake. Katika utimizo wa pili wa unabii huo, utawala wa Mungu ungekatizwa kwa kipindi fulani cha wakati, lakini si kwa sababu Mungu alishindwa katika njia fulani.
Jon: Unamaanisha nini?
Richard: Wakati wa zamani, wafalme wa Israeli waliotawala Yerusalemu walisemwa kuwa wanakaa kwenye “kiti cha ufalme cha Yehova.” * Wafalme hao waliwakilisha Mungu katika kutawala watu wake. Kwa hiyo, utawala wa wafalme hao ulikuwa kabisa unafananisha utawala wa Mungu. Kisha wakati fulani, wengi kati ya wafalme hao walimuasi Mungu na wengi kati ya watu waliotawaliwa nao walifuata mufano wao mubaya. Kwa sababu ya uasi wa Waisraeli, Mungu aliwaruhusu Wababiloni wawashinde katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, hakuna mufalme mwengine aliyewakilisha Yehova katika Yerusalemu. Kwa njia hiyo, ilionekana kwamba utawala wa Mungu unakatizwa. Ungali unanifuata?
Jon: Ndiyo.
Richard: Kwa hiyo, mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu ulionyesha mwanzo wa nyakati saba, ao wakati ambapo utawala wa Mungu ungekatizwa. Kwenye mwisho wa nyakati hizo saba, Mungu angeweka mutawala mupya ili kumuwakilisha, mara hii, mutu fulani wa mbinguni. Na ni wakati huo ndipo unabii mwingine mbalimbali tulisoma katika Danieli ungetimizwa. Sasa ulizo la maana ni hili: Nyakati hizo saba ziliisha wakati gani? Ikiwa tunaweza kujibia ulizo hilo, tutajua wakati gani Ufalme wa Mungu ulianza kutawala.
Jon: Ninaelewa. Maana yake nyakati saba ziliisha katika mwaka wa 1914?
Richard: Ndiyo, ni vile kabisa!
Jon: Lakini tunajua vile namna gani?
Richard: Wakati wa huduma yake hapa duniani, Yesu alionyesha kwamba nyakati saba zilikuwa hazijaisha. * Kwa hiyo, zinapaswa kuwa kipindi kirefu sana cha wakati. Nyakati hizo saba zilianza mamia ya miaka mbele Yesu akuje hapa duniani, na ziliendelea kwa muda fulani kisha yeye kurudia mbinguni. Kumbuka tena kwamba maana ya unabii huo wa Danieli haingekuwa wazi mbele ya “wakati wa mwisho.” * Jambo la kupendeza ni kwamba, mwishoni mwa miaka kati ya 1801 na 1900, wanafunzi wa Biblia wenye moyo mweupe walichochewa kuchunguza kwa uangalifu sana unabii huo na unabii mwingine mbalimbali. Walianza kutambua kwamba nyakati saba zingeisha katika mwaka wa 1914. Na matukio mengi ya dunia kuanzia hapo na kuendelea yanahakikisha kwamba mwaka wa 1914 ndio mwaka Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni. Huo ndio mwaka ambao dunia hii iliingia katika siku zake za mwisho, ao wakati wa mwisho. Sasa, ninajua kwamba si vyepesi kwako kuelewa mara moja hizi habari nyingi mupya . . .
Jon: Ndiyo. Nitasoma habari hii tena na tena ili niielewe vizuri.
Richard: Usiogope. Mimi pia iliniomba wakati murefu ili nielewe unabii huo na utimizo wake. Lakini kufikia sasa, ninatumaini mazungumuzo yetu yamekusaidia kuona kwamba mambo Mashahidi wa Yehova wanaamini juu ya Ufalme wa Mungu yanategemea Biblia.
Jon: Kweli kabisa. Nimependezwa sikuzote na namna munategemea Biblia ili kueleza imani yenu.
Richard: Na ninaona kwamba wewe pia unapenda kufanya hivyo. Lakini kama vile nilikuambia, habari hizi ni nyingi na ni vigumu kuzielewa zote mara moja. Inawezekana ungali na maulizo fulani. Kwa mufano, tumetambua kwamba nyakati saba zinahusu Ufalme wa Mungu na zilianza katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Lakini, namna gani tunajua kwa uhakika kabisa kwamba nyakati hizo saba ziliisha katika mwaka wa 1914? *
Jon: Ndiyo, ninajiuliza pia vile.
Richard: Biblia yenyewe inatusaidia kujua urefu wa nyakati hizo saba. Unaweza kupenda tuzungumuzie habari hiyo wakati nitakuja tena?
Jon: Hilo ni wazo nzuri.
Una ulizo fulani juu ya habari za Biblia ambalo umekwisha kujiuliza? Unapenda kujua mengi juu ya mambo Mashahidi wa Yehova wanaamini ao juu ya mambo fulani wanayofanya? Ikiwa jibu ni ndiyo, usisite kuuliza ulizo hilo wakati utakutana na Shahidi wa Yehova. Atafurahi kuzungumuzia mambo hayo pamoja na wewe.
^ fu. 5 Kupitia programu yao ya kujifunza Biblia na watu nyumbani bila kulipa, Mashahidi wa Yehova wanazungumuza kwa ukawaida juu ya Biblia pamoja na jirani zao.
^ fu. 21 Soma sura ya 9 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza pia kupata kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.
^ fu. 63 Katika unabii wake juu ya siku za mwisho, Yesu alisema hivi: ‘Yerusalemu [linalowakilisha utawala wa Mungu] litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mupaka nyakati zilizowekwa za mataifa zitimie.’ (Luka 21:24) Kwa hiyo kipindi cha kukatizwa kwa utawala wa Mungu kilikuwa kinaendelea wakati wa Yesu na kingeendelea mupaka siku za mwisho.
^ fu. 67 Soma ukurasa wa 215-218 wa kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Unaweza pia kupata kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.
Sehemu ya pili ya mazungumuzo haya itazungumuzia maandiko ya Biblia yanayotusaidia kuelewa urefu wa zile nyakati saba.