Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UMUKARIBIE MUNGU

Mungu Anajaza ‘Mioyo Yetu kwa Ukamili’

Mungu Anajaza ‘Mioyo Yetu kwa Ukamili’

Je, Yehova anatuhangaikia kabisa, ao hahangaike juu ya mateso ambayo wanadamu wanapata duniani? Jibu la Biblia kwa ulizo hilo ni lenye kufariji. Kwa kweli, Mungu anawahangaikia wanadamu, na anataka wawe na furaha katika maisha. Kila siku anawaruhusu wanadamu wafaidike na wema wake mwingi, hata wale wasiokuwa na shukrani kwake. Tuchunguze maneno ya mutume Paulo.​—Soma Matendo 14:16, 17.

Akizungumuza na watu ambao hawakuwa waabudu wa Mungu katika muji wa Listra, Paulo alisema hivi: ‘Katika vizazi vilivyopita yeye aliwaruhusu mataifa yote waendelee kutembea katika njia zao, ijapokuwa, kwa kweli, hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamufu.’ Maneno hayo ya Paulo yalikuwa na maana gani kwa wasikilizaji wake?

Watu wa Listra walielewa kwa urahisi maana ya maneno hayo ya Paulo. Waliishi katika eneo la walimaji ambalo lilikuwa na mbolea na maji mengi. Lakini, kama Paulo alivyowakumbusha, Mungu ndiye anayefanya mvua inyeshe na ndiye anayeleta majira yenye kuzaa matunda. Kwa hiyo, kila mara walipopata mavuno mengi na kula chakula kizuri, walikuwa wanafaidika na wema wa Mungu.

Maneno ambayo Paulo aliwaambia watu wa Listra yanatufundisha mambo mengi ya maana juu ya Yehova Mungu.

Yehova anatupatia uhuru wa kuchagua. Ona kwamba Yehova aliwaruhusu watu wa mataifa “waendelee kutembea katika njia zao.” Kitabu kimoja kilicho na maagizo kwa ajili ya watafsiri wa Biblia kinasema kwamba maneno hayo yanaweza kumaanisha “kutembea kama wanavyopenda” ao “kufanya mambo ambayo wanafikiri kuwa mazuri zaidi.” Yehova hamulazimishe mutu yeyote amuabudu. Alituumba tukiwa na uhuru wa kuchagua, ni kusema, uwezo wa kujichagulia namna yetu ya kuishi.—Kumbukumbu la Torati 30:19.

Yehova anataka tumujue. Paulo alieleza kwamba Yehova hakujiacha “mwenyewe bila ushahidi.” Kitabu ambacho tulitaja hapo juu kinasema kwamba maneno hayo yanaweza kutafsiriwa “amewaonyesha watu waziwazi yeye ni Mungu wa aina gani.” Uumbaji mbalimbali wa Mungu unaonyesha waziwazi “sifa zake ambazo hazionekani,” kutia ndani wema wake, hekima yake, nguvu zake, na upendo wake. (Waroma 1:20) Katika Biblia, Yehova amefunua mambo mengi juu yake mwenyewe. (2 Timotheo 3:16, 17) Hilo linaonyesha wazi kwamba anataka tumujue, sivyo?

Kila siku Mungu anawaruhusu wanadamu wafaidike na wema wake, hata wale wasiokuwa na shukrani kwake

Yehova anataka tuwe na furaha. Paulo anasema kwamba Yehova anajaza ‘mioyo yetu kikamili kwa chakula na uchangamufu.’ Hata mutenda-zambi ambaye hamujue Yehova anaweza kula chakula na kutosheka na kupata furaha katika maisha kwa kiasi fulani. Hata hivyo, Mungu anataka tuwe na furaha ya kweli na ya milele. Tunaweza kupata furaha hiyo ikiwa tu tunajifunza kweli juu yake na kuishi kulingana na kweli hiyo.​—Zaburi 144:15; Mathayo 5:3.

Sisi wote tunafaidika na wema wa Yehova kila siku. Sababu gani usijifunze mengi zaidi juu ya namna unaweza kuonyesha shukrani yako kwa Mungu ambaye anajaza moyo wako ‘kikamili kwa chakula na uchangamufu’?

Tafazali, mwezi huu wa 7, soma maandiko haya katika Biblia:

Matendo sura ya 11 mupaka sura ya 28