Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UMUKARIBIE MUNGU

‘Endeleeni Kuomba, Nanyi Mutapewa’

‘Endeleeni Kuomba, Nanyi Mutapewa’

“Bwana, tufundishe jinsi ya kusali.” (Luka 11:1) Mwanafunzi mumoja wa Yesu ndiye alimuomba Yesu jambo hilo. Katika jibu lake, Yesu alizungumuzia mifano miwili ambayo inatufundisha namna ya kusali ili Mungu atusikilize. Ikiwa umekwisha kujiuliza kama Mungu anasikiliza sala zako, utapendezwa na jibu la Yesu.​—Soma Luka 11:5-13.

Mufano wa kwanza unakazia yule anayesali. (Luka 11:5-8) Katika mufano huo, mwanaume fulani anapokea mugeni usiku sana na hana chakula cha kumupatia. Kwa mwanaume huyo, iliomba kutenda bila kukawia. Ijapokuwa ilikuwa usiku sana, anaenda kwa rafiki yake ili kumukopesha mikate fulani. Kwanza, rafiki yake anakawia kuamuka kwa sababu alikuwa katika usingizi muzito pamoja na familia yake. Lakini bila haya, mwanaume huyo aliyepokea mugeni aliendelea kupiga hodi mupaka rafiki yake akaamuka mwishowe na akamupatia mikate fulani. *

Mufano huo wa Yesu unatufundisha nini juu ya sala? Yesu anatufundisha kwamba tunahitaji kudumu, ni kusema, kuendelea kuomba, kuendela kutafuta, na kupiga hodi. (Luka 11:9, 10) Sababu gani? Je, Yesu anamaanisha kwamba Mungu anakawia kusikiliza sala zetu? Hapana. Yesu anamaanisha kwamba tofauti na rafiki huyo aliyekawia, Mungu iko tayari kujibu sala zinazofaa za wale wanaomuomba kwa imani. Tunaonyesha imani kama hiyo kwa kudumu katika sala. Kwa kuendelea kuomba, tunaonyesha kwamba tunahitaji kabisa mambo tunayoomba na kwamba tunaamini kabisa kama Mungu anaweza kututolea mambo hayo, ikiwa yanapatana na mapenzi yake.​—Marko 11:24; 1 Yohana 5:14.

Mufano wa pili unakazia Yehova, ‘Musikiaji wa sala.’ (Zaburi 65:2) Yesu anauliza hivi: ‘Ni baba gani kati yenu ambaye, ikiwa mwana wake anaomba samaki, labda atamupa nyoka badala ya samaki? Ao ikiwa pia anaomba yai, atamupa nge?’ Jibu ni wazi: hakuna baba yeyote mwenye upendo anayeweza kuwapatia watoto wake vitu vya kuwaumiza. Kisha, Yesu anaeleza maana ya mufano huo kwa kusema hivi: Ikiwa baba wa kibinadamu wasio wakamilifu ‘wanawapa zawadi zilizo njema’ watoto wao, “je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu,” zawadi iliyo njema zaidi, wana wake walio duniani ambao wanamuomba? *​—Luka 11:11-13; Mathayo 7:11.

Mungu iko tayari kujibu sala zinazofaa za wale wanaomuomba kwa imani

Mufano huo unatufundisha nini juu ya Yehova ‘Musikiaji wa sala’? Yesu anatuomba tumuone Yehova kuwa Baba mwenye upendo aliye tayari kutimiza mahitaji ya watoto wake. Kwa hiyo, waabudu wa Yehova wanaweza kujisikia huru kumukaribia ili kumuelezea mahitaji ya moyo wao. Na wakijua kwamba anawatakia mema, wanaweza kuwa tayari kukubali jibu lake kwa sala zao, hata ikiwa jibu hilo ni tofauti na yale ambayo walitazamia. *

Tafazali, mwezi huu wa 4, soma maandiko haya katika Biblia:

Luka sura ya 7 mupaka sura ya 21

^ Mufano huo wa Yesu unaonyesha desturi na mazoea ya kawaida ya watu. Wayahudi waliona kukaribisha wageni kuwa daraka la maana zaidi. Familia ilipika mikate ya kutosha kwa ajili ya siku nzima, lilikuwa jambo la kawaida kukopa ikiwa mikate waliyopika iliisha. Pia, ikiwa walikuwa masikini, familia nzima ililala chini katika chumba kimoja.

^ Yesu alitumia mara nyingi maneno “hata zaidi” ili kuonyesha lililo ndogo mupaka lililo kubwa zaidi. Alitumia maneno hayo ili kukazia namna Mungu alivyo mwema zaidi kuliko wanadamu.

^ Ili kupata habari zingine juu ya namna tunaweza kusali ili Mungu atusikilize, soma sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.