Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Muzee wa Siku Akaketi’

‘Muzee wa Siku Akaketi’

Umukaribie Mungu

‘Muzee wa Siku Akaketi’

BIBLIA inasema kama ‘hakuna mwanadamu ambaye amemuona Mungu wakati wowote.’ (Yohana 1:18) Mungu ana utukufu mwingi sana hivi kwamba hakuna mwanadamu anayeweza kumuona na kuendelea kuishi. (Kutoka 33:20) Hata hivyo, wakati fulani alichagua wanaume fulani ili kuwaonyesha maono ya mbinguni. Nabii Danieli alikuwa mumoja kati ya wanaume hao. Mambo aliyoona yalimufanya amuogope Mungu na amuheshimu sana. Maono ya Danieli yanapaswa pia kutuchochea tumuogope Mungu na kumuheshimu sana. Ona namna Danieli alivyoeleza mambo ambayo alipata pendeleo la kuona. *​—Soma Danieli 7:9, 10.

‘Muzee wa Siku.’ Ni Danieli tu ndiye anayetumia maneno ‘Muzee wa Siku;’ maneno hayo yanamaanisha “mutu aliye na miaka mingi.” (Danieli 7:9, 13, 22) Yehova ana miaka ngapi? Hana mwanzo wala mwisho kwa sababu yeye ni ‘Mufalme wa umilele.’ (1 Timotheo 1:17; Yuda 25) Umilele wa Mungu unatuhakikishia kama ana hekima isiyo na mipaka, kwa sababu Biblia inalinganisha uzee na hekima. (Ayubu 12:12) Hatuwezi kuelewa vizuri umilele wa Mungu kwa sababu akili yetu ina mipaka. Pia, hatuwezi kutumainia kuelewa vizuri kabisa hekima ya Mungu isiyoweza kulinganishwa.​—Waroma 11:33, 34.

Ona kwamba Muzee wa Siku ‘aliketi.’ Kwa sababu gani? Maandiko yanayotangulia na yanayofuata andiko hilo yanatusaidia kuelewa vizuri, kwa sababu yanatumia maneno kama vile “mahakama” na “hukumu.” (Danieli 7:10, 22, 26) Kwa hiyo, katika maono hayo, Yehova alikaa ili kuhukumu. Kuhukumu nani? Mataifa ya dunia, ambayo yanafananishwa na wanyama katika maono ya Danieli. * (Danieli 7:1-8) Yehova ni Muamuzi wa namna gani?

‘Mavazi yake yalikuwa meupe kama seluji, na nywele za kichwa chake zilikuwa kama sufu safi.’ Rangi nyeupe inamaanisha haki na usafi. Kwa kawaida sufu (manyoya ya kondoo) ni nyeupe. Kwa hiyo, nywele zilizo kama sufu zinapaswa kuwa nyeupe. Je, unaweza sasa kufikiria akilini mambo ambayo Danieli aliona? Je, unaona akilini yule Muamuzi aliye na nywele nyeupe na anayevaa kanzu nyeupe sana? Maneno hayo ya mufano yanatuhakikishia kama hukumu za Yehova ni zenye haki na zenye hekima. Yeye ni Muamuzi ambaye tunapaswa kutumainia sana na kuheshimu.

‘Kulikuwa na maelfu elfu walioendelea kumutumikia, na elfu kumi mara elfu kumi walioendelea kusimama mbele zake.’ Watumishi hao walio mbinguni ni nani? Biblia inasema kama malaika ni “wahudumu wa [Mungu].” (Zaburi 104:4) Malaika wa Mungu, ambao ni wengi sana, wana kazi kubwa ya ‘kutenda neno lake’ na ‘kufanya mapenzi yake.’ (Zaburi 103:20, 21) Hilo linaonyesha kama hekima ya Mungu haina mipaka, sivyo? Ni nani mwengine anayeweza kupanga vizuri majeshi ya malaika na kuwatolea kazi kwa wakati usio na mipaka isipokuwa Mungu tu?

Maono ya Danieli yanatuchochea tumutumainie Yehova, Muzee wa Siku. Hukumu zake ni zenye haki na hekima yake ni yenye kutumainika. Sababu gani usijifunze mengi juu ya namna unavyoweza kumukaribia Mungu mwenye hekima yote?

Tafazali, mwezi huu wa 10, soma Maandiko haya katika Biblia:

Danieli sura ya 4-12 mupaka Hosea sura ya 1-14

[Maelezo ya chini]

^ Danieli hakumuona Mungu kabisa; ilikuwa maono tu. Anapoeleza mambo aliyoona, Danieli anatumia maneno ya mufano yanayomupa Mungu sura ya kibinadamu. Hatupaswe kuchukua maneno hayo neno kwa neno, yanatusaidia tu kumuelewa Mungu vizuri zaidi.

^ Ili kupata maelezo mengine juu ya maono ya Danieli ambamo aliona wanyama, usome sura ya 9 ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 18]

Yeye ni Muamuzi ambaye tunapaswa kutumainia sana na kuheshimu