Mazungumuzo ya Biblia Pamoja na Jirani—Je, Mungu Anawapa Watu Malipizi kwa Kuwaunguza Katika Moto wa Mateso?
Mazungumuzo ya Biblia Pamoja na Jirani—Je, Mungu Anawapa Watu Malipizi kwa Kuwaunguza Katika Moto wa Mateso?
MASHAHIDI WA YEHOVA wanafurahia kuzungumuzia Biblia pamoja na majirani wao. Je, una ulizo fulani ambalo umekwisha kujiuliza juu ya Biblia? Je, ungependa kujua mengi juu ya mambo ambayo Mashahidi wa Yehova wanaamini ao juu ya mambo fulani wanayofanya? Ikiwa jibu ni ndiyo, usisite kuuliza jambo hilo wakati utakutana na Shahidi wa Yehova. Atafurahi kuzungumuzia jambo hilo pamoja nawe.
Habari inayofuata ni mufano wa mazungumuzo ambayo Shahidi wa Yehova fulani anaweza kuwa nayo pamoja na jirani yake. Kwa mufano, Shahidi fulani anayeitwa Martin anamukuta mutu anayeitwa Antoine nyumbani kwake.
Je, Mungu Atawapa Watu Wabaya Malipizi?
Martin: Antoine, ninafurahi kukutana nawe tena.
Antoine: Ninafurahi pia.
Martin: Nilikuwa ninafikiria jambo fulani ambalo ulisema mara ya mwisho tulipoonana.
Antoine: Ni jambo gani?
Martin: Ulisema ulishangaa kusikia kama Mashahidi wa Yehova hawaamini moto wa mateso.
Antoine: Ndiyo, hilo lilinishangaza sana. Kwa kweli, ni vigumu kwangu kukubali kwamba hamuamini moto wa mateso.
Martin: Ninakushukuru sana kwa sababu unanifunulia mawazo yako. Kila mara ninafurahi sana kusikiliza mawazo ya watu wengine, na nimetambua kama watu wana mawazo mbalimbali juu ya moto wa mateso. Wewe unawaza moto wa mateso ni nini?
Antoine: Ninaamini kama wakati watu wabaya wanakufa, wanaenda katika moto wa mateso ili wateswe milele.
Martin: Watu wengi wanaamini hivyo. Acha nikuulize Antoine, umekwisha kukutana na hali fulani ngumu katika maisha yako?
Antoine: Ndiyo. Dada yangu aliuawa kumepita miaka 5.
Martin: Pole sana. Bila shaka unaendelea kumukumbuka.
Antoine: Ndiyo. Ninamukumbuka kila siku.
Martin: Nimetambua kama watu fulani ambao wameteswa na matendo ya watu wabaya wangependa kabisa watu hao waende katika moto wa mateso ili wapate malipizi kwa sababu ya matendo yao.
Antoine: Ni vile kabisa! Ninataka mutu aliyemuua dada yangu apate malipizi.
Martin: Mawazo yako yanaeleweka. Biblia inafundisha kama Mungu pia anakasirika sana anapoona watu wazuri wanatendewa vibaya—na anaahidi kama atawapa watu wabaya malipizi. Ona mambo ambayo andiko la Isaya 3:11 linasema: ‘Ole wake mutu muovu!—Musiba; kwa maana matendo yaliyotendwa kwa mikono yake mwenyewe atalipwa yeye!’ Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama Mungu atawapa watu wabaya malipizi.
Antoine: Lakini hilo litawezekana namna gani ikiwa hakuna moto wa mateso?
Martin: Ni ulizo nzuri. Kwa kifupi, jibu ni kwamba Mungu anawapa watu wabaya malipizi kwa kuwaharibu milele. Ona yale ambayo Biblia inasema katika andiko la 2 Wathesalonike 1:9. Tafazali, unaweza kusoma andiko hilo?
Antoine: Ndiyo. Linasema hivi: ‘Watu hao watahukumiwa azabu ya uharibifu wa milele kutoka mbele ya Bwana.’
Martin: Unaona Antoine, watu wabaya hawana tumaini kwa sababu Mungu anawapa malipizi kwa kuwaharibu milele. Hawana tumaini la kuishi tena wakati ujao.
Antoine: Ninaelewa andiko hilo, lakini ninaona kama hilo si jambo la haki kwa sababu si watu wabaya tu ndio wanakufa. Hauone kama watu hao wanastahili malipizi makali zaidi?
Haki Ilimusukuma Mungu Afanye Nini?
Martin: Ninaona kama wewe ni mutu anayehangaikia sana haki.
Antoine: Ndiyo kabisa.
Martin: Ni vizuri kufanya hivyo. Mungu pia anahangaikia sana haki; ndiyo sababu alituumba tukiwa na uwezo wa kutofautisha mema na mabaya. Lakini, wakubwa wa dini wanafundisha kama Mungu anawapa watu malipizi kwa kuwaunguza katika moto wa mateso. Kwa kufundisha hivyo wanachochea watu wawaze kama Mungu hana haki hata kidogo.
Antoine: Sikuelewe vizuri.
Martin: Ili tuelewe vizuri, tuchukue mufano. Unajua habari ya Adamu na Eva inayozungumuziwa katika Biblia?
Antoine: Ndiyo. Mungu aliwaambia wasikule tunda la muti fulani, lakini hawakumutii.
Martin: Ni vile. Acha sasa tusome pamoja habari hiyo katika Biblia. Inapatikana katika andiko la Mwanzo 2:16, 17. Andiko hilo linasema hivi: ‘Yehova Mungu akamuwekea mutu amri hii: Matunda ya kila muti wa bustani unaweza kula mupaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.’ Sasa, Mungu alisema ni jambo gani lingetokea ikiwa Adamu angekula tunda la muti uliokatazwa?
Antoine: Alisema kama Adamu angekufa.
Martin: Ni vile. Waza kidogo: Kupitia zambi yake, Adamu aliwafanya watu wote wazaliwe wenye zambi. * Adamu alifanya zambi nzito, hata hivyo Mungu hakusema kama atapewa malipizi katika moto wa mateso, sivyo?
Antoine: Ndiyo.
Martin: Lakini ikiwa Adamu na Eva wangekuwa katika hatari ya kuteswa milele katika moto, hauone kama Mungu angewajulisha? Lingekuwa jambo la haki na la upendo kuwajulisha, sivyo?
Antoine: Inawezekana ni vile.
Martin: Tuone pia yale ambayo Mungu aliwaambia Adamu na Eva kisha wao kufanya zambi. Tafazali, unaweza kusoma andiko la Mwanzo 3:19?
Antoine: Ndiyo. Linasema hivi: ‘Kwa jasho la uso wako utakula mukate mupaka utakaporudia katika udongo, kwa kuwa ulitolewa katika huo. Kwa maana wewe ni mavumbi nawe utarudia mavumbini.’
Martin: Asante. Kulingana na maneno ya Mungu katika andiko hilo, Adamu alipaswa kuenda wapi kisha kufa kwake?
Antoine: Alipaswa kurudia katika mavumbi ya udongo.
Martin: Ni vile kabisa. Lakini, ili mutu arudie mahali fulani ni lazima mutu huyo awe alikuwa kwanza mahali hapo, sivyo?
Antoine: Ndiyo.
Martin: Sasa Adamu alikuwa wapi mbele Mungu amuumbe?
Antoine: Hakuwa fasi.
Martin: Hiyo ni kweli. Tena, wakati Mungu alimuhukumu, hakutaja hata kidogo moto wa mateso. Je, unawaza lingekuwa jambo la haki Mungu kumuambia Adamu kwamba atarudia katika udongo na huku anajua kama ataenda katika moto wa mateso?
Antoine: Hapana, halingekuwa jambo la haki.
Je, Shetani Ibilisi Anatimiza Mapenzi ya Mungu?
Martin: Kuna jambo lingine ambalo tunapaswa kufikiria juu ya fundisho la moto wa mateso.
Antoine: Ni jambo gani?
Martin: Kwa kawaida, watu wanasema “musimamizi” wa moto wa mateso ni nani? Wanasema ni nani anayewatesa watu walio katika moto huo?
Antoine: Wanasema ni Ibilisi.
Martin: Lakini, Ibilisi ndiye adui wa kwanza wa Mungu. Ikiwa Mungu anawatupa watu katika moto wa mateso ili Shetani awatese, hauone kwamba ingeonekana kama Mungu na Shetani wanatumika pamoja?
Antoine: Hmm. Nilikuwa bado sijafikiria jambo hilo.
Martin: Ili kuelewa vizuri, tuchukue mufano—wewe ni muzazi, sivyo?
Antoine: Ndiyo, nina mutoto mwanaume. Ana miaka 15.
Martin: Wazia kama mutoto wako anakuwa muasi sana na anafanya mambo mengi ya kukuumiza. Wewe utafanya nini?
Antoine: Nitajaribu kumusaidia abadilike.
Martin: Niko hakika kama utajaribu kufanya hivyo mara nyingi.
Antoine: Ndiyo.
Martin: Wazia kama unajikaza sana kumusaidia lakini anakataa kukusikiliza. Mwishowe, utatambua kama itaomba umupatie malipizi.
Antoine: Ndiyo.
Martin: Lakini, utafanya nini ukitambua kama kuna mutu fulani mubaya aliyemufundisha mutoto wako kufanya mambo hayo yote mabaya na aliyemushawishi akatae kukusikiliza?
Antoine: Nitamukasirikia sana mutu huyo.
Martin: Sasa ninataka kujua mawazo yako juu ya jambo hili: Kisha kujua kama mutu huyo ni mubaya, mwenye mwenendo muovu na alishawishi mutoto wako ili akugeuke, je, unaweza kumuendea mutu huyohuyo na kumuomba akusaidie kumupatia mutoto wako malipizi?
Antoine: Hapana. Huo unaweza kuwa upumbavu kabisa.
Martin: Sasa, hauone kama ingekuwa upumbavu kabisa ikiwa Mungu angemuomba Shetani Ibilisi awapatie malipizi watu ambao Shetani mwenyewe alishawishi?
Antoine: Ndiyo.
Martin: Sasa, ikiwa Mungu anataka watu wabaya wapate malipizi, unawaza kama Shetani, ambaye ni adui wa kwanza wa Mungu, anaweza kutimiza mapenzi ya Mungu kwa kuwatesa watu wabaya katika moto?
Antoine: Nilikuwa bado sijafikiria jambo hilo!
Yehova Atamaliza Ubaya Wote
Martin: Hata hivyo, uwe hakika kama Mungu atawapa malipizi watu wabaya ambao hawatake kubadilika. Tunaweza kusoma andiko la mwisho litakalokusaidia uelewe vizuri jambo hilo. Ni andiko la Zaburi 37:9. Tafazali, unaweza kulisoma?
Antoine: Sawa. Linasema hivi: ‘Watenda-maovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomutumaini Yehova ndio watakaoimiliki dunia.’
Martin: Asante. Umeona ni nini ambayo Yehova Mungu atawatendea wafanya zambi?
Antoine: Andiko linasema atawakatilia mbali.
Martin: Ni kweli. Kuwakatilia mbali kunamaanisha kuwaharibu milele. Lakini watu wazuri, ni kusema ‘wale wanaomutumaini Yehova,’ wataishi milele hapa duniani. Lakini inawezekana ujiulize maulizo fulani. Kwa mufano, sababu gani Mungu hawazuie kwanza watu wasifanye zambi? Na ikiwa anataka kabisa kuwapa watu wabaya malipizi, sababu gani anakawia?
Antoine: Hayo ni maulizo mazuri.
Martin: Nitafurahi kukuonyesha majibu ya Biblia wakati tutazungumuza tena. *
Antoine: Nitakuchunga kwa hamu.
[Maelezo ya chini]
^ Soma Waroma 5:12.
^ Ili kupata habari zingine, usome sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.