Sifa ya Wema Ni ya Lazima Sana Machoni pa Mungu
Sifa ya Wema Ni ya Lazima Sana Machoni pa Mungu
KIJANA mumoja huko Japon aliguswa moyo na wema ambao mwanaume fulani mwenye kuzeeka alimuonyesha. Mwanaume huyo aliyekuwa misionere alipitisha miaka mingi bila kufika katika inchi hiyo ya Asia na hakuzoea tena kuzungumuza Kijapani. Lakini, kila juma alimutembelea kijana huyo nyumbani ili kujifunza naye Biblia. Kwa kicheko cha kirafiki na tabia ya wema, mwanaume huyo muzee alijibu kwa uvumilivu maulizo mengi ya mwanafunzi huyo kijana aliyetaka kujua mengi.
Kijana huyo hawezi kusahau hata kidogo wema ambao misionere huyo alimuonyesha. Aliwaza hivi: ‘Ikiwa Biblia inaweza kumufanya mutu awe mwema na mwenye upendo, kwa kweli ninapaswa kujifunza Biblia.’ Hilo lilimuchochea ajifunze kitabu hicho kilichokuwa kigeni kwake. Ni kweli, mara nyingi wema unagusa moyo zaidi kuliko maneno.
Ni Sifa Inayotoka kwa Mungu
Kwa kawaida, tunawaonyesha wema watu wa jamaa yetu kwa sababu wema unamaanisha upendo unaotokana na uhusiano wa jamaa. * Hata hivyo, wema ni sifa inayotoka kwa Mungu. Yesu alisema kama Baba yake wa mbinguni ni mwema kuelekea wale wanaomupenda na wale ‘wasio na shukurani.’ Yesu aliwatia moyo wafuasi wake wamuige Mungu katika njia hiyo. Alisema hivi: ‘Muwe wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mukamilifu.’—Luka 6:35; Mathayo 5:48; Kutoka 34:6.
Kwa sababu watu waliumbwa kwa mufano wa Mungu, wanaweza kuonyesha sifa hiyo. (Mwanzo 1:27) Kwa kweli, tunaweza kumuiga Mungu kwa kujifunza kuwaonyesha wengine wema. Biblia inaonyesha kama wema ni sehemu ya tunda la roho takatifu ya Mungu, ao nguvu yake ya utendaji. (Wagalatia 5:22) Kwa hiyo, mutu anaweza kuwa na sifa hiyo na kuionyesha wengine anapojifunza juu ya Mungu, Muumbaji wetu, na kumukaribia.
Sifa ya wema ni sehemu ya utu wetu na ni ya lazima sana machoni pa Mungu, ndiyo maana Mungu anatuambia tuwe wema sisi kwa sisi. (Waefeso 4:32) Tena tunakumbushwa hivi: ‘Musisahau ukaribishaji-wageni,’ ao wema kuelekea wageni.—Waebrania 13:2.
Kwa sababu katika dunia ya leo watu si wema na hawana shukurani, je, inawezekana tuwaonyeshe wengine wema, na hata wageni? Ni nini kinachoweza kutusaidia kufanya hivyo? Na, sababu gani tunapaswa kuzungumuzia sifa hiyo?
Ni Sifa ya Lazima Machoni pa Mungu
Jambo la kupendeza ni kwamba, kisha kusema kama tunapaswa kuwa wema, hata kuelekea wageni, mutume Paulo aliendelea kusema hivi: “Kupitia huo watu wengine, bila wao wenyewe kujua, waliwakaribisha malaika.” Wewe unaweza kujisikia namna gani ikiwa unapata pendeleo la kuwakaribisha malaika nyumbani kwako? Katika andiko hilo, Paulo alianza kwa kusema kama watu wengine waliwakaribisha malaika “bila wao wenyewe kujua.” Alipenda kusema kama ikiwa tuna tabia ya kuwaonyesha wengine wema, hata wageni ao watu tusiowajua, tunaweza kupata baraka ambazo hatukutazamia.
Biblia nyingi zilizo na maelezo pembeni zinapatanisha maneno ya Paulo na habari ya Abrahamu na Loti iliyo katika kitabu cha Mwanzo Sura ya 18 na 19. Malaika waliwafikia Abrahamu na Loti kama vile wageni waliokuwa na ujumbe wa lazima sana. Walimuletea Abrahamu ujumbe ulioonyesha kama Mungu atatimiza ahadi yake ya kumupatia mutoto, lakini walimuletea Loti ujumbe wa uharibifu uliokaribia sana wa miji ya Sodoma na Gomora.—Mwanzo 18:1-10; 19:1-3, 15-17.
Ukisoma maandiko yanayotajwa hapa juu, utaona kama Abrahamu na Loti waliwaonyesha wema wapita-njia ambao hawakuwa wanajua. Kwa kweli, wakati wa zamani, kuwakaribisha wasafiri na wapita-njia—iwe marafiki, watu wa jamaa, ao wageni—ilikuwa desturi na kila mutu alipaswa kufanya hivyo. Sheria ya Musa iliwaomba Waisraeli wahangaikie mahitaji ya wageni waliokuwa katika inchi yao. (Kumbukumbu la Torati 10:17-19) Hata hivyo, ni wazi kama Abrahamu na Loti walifanya zaidi ya jambo lililoombwa na sheria. Walijikaza sana kuwaonyesha wageni wema, na walibarikiwa kwa kufanya hivyo.
Abrahamu alibarikiwa kwa kupata mutoto kwa sababu ya matendo yake ya wema, sisi pia tumebarikiwa kupitia matendo yake. Namna gani? Abrahamu na mutoto wake Isaka walitimiza daraka la lazima katika kusudi la Mungu. Walikuwa watu wa maana zaidi katika kizazi cha Yesu Masiya. Na uaminifu wao ulionyesha mbele ya wakati namna Mungu angewaokoa watu kwa sababu ya upendo na wema wake.—Mwanzo 22:1-18; Mathayo 1:1, 2; Yohana 3:16.
Habari hizo zinaonyesha yale Mungu anataka watu wake wafanye na kama sifa ya wema ni ya lazima sana machoni pake. Tunapaswa kuonyesha wema kwa sababu ni sifa ya lazima machoni pa Mungu.
Kuonyesha Wema Kunatusaidia Kumujua Mungu Vizuri Zaidi
Biblia ilisema kama katika siku zetu watu wengi wangekuwa ‘wasio na shukurani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili.’ (2 Timotheo 3:1-3) Kwa kweli, kila siku unakutana na watu wa namna hiyo. Lakini, hiyo si sababu ya kukosa kuwaonyesha wengine wema. Wakristo wanakumbushwa hivi: ‘Musimulipe yeyote uovu kwa uovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.’—Waroma 12:17.
Tunaweza pia kujikaza sana ili kuwaonyesha wengine wema kwa moyo wetu wote. Biblia inasema hivi: ‘Kila mutu ambaye anapenda anapata kumujua Mungu,’ na namna moja ya kuwa na upendo ni kuwaonyesha wengine wema. (1 Yohana 4:7; 1 Wakorintho 13:4) Kwa kweli, kwa kuwaonyesha watu wema, tunaweza kumujua Mungu vizuri, na hilo litafanya tuwe na furaha zaidi. Kulingana na tafsiri fulani, katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu alisema hivi: ‘Heri walio wema—kwa sababu wataonyeshwa wema. Heri walio safi moyoni—kwa sababu watamuona Mungu.’—Mathayo 5:7, 8.
Matendo 20:35) Ndiyo, jambo nzuri unaloweza kufanya unapovunjika moyo ni kuwaonyesha wengine wema.
Tuzungumuzie mufano wa Aki, kijana mwanamuke, ambaye ni mama wa watoto wawili. Kisha kifo cha mama yake kilichotokea kwa kushitukia, alivunjika moyo sana. Mara kwa mara alianza kujisikia vibaya, kwa hiyo alilazimika kuonana na muganga. Kisha, familia moja ilihamia karibu na kwake. Wao pia walitoka tu kufiwa na baba yao aliyefanya aksida, na mama yao alibaki peke yake na watoto tano wadogo. Aki aliwasikilia huruma sana na alijikaza sana ili kufanya urafiki na mama huyo na watoto wake. Alifanya yote aliyoweza ili kusaidia familia hiyo—aliwatolea chakula, nguo ambazo yeye na familia yake hawakuhitaji tena, na mambo mengine—kufanya hivyo kulimusaidia aanze kujisikia vizuri. Aliona kama maneno haya ya Biblia ni ya kweli: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (‘Kumukopesha Yehova’
Hatuhitaji kuwa na feza nyingi, uwezo fulani ao nguvu ya kimwili ili kuonyesha wengine wema. Kumuonyesha mutu sura ya kicheko, kumuambia neno lenye kufariji, kumusaidia, kumutolea zawadi, ao kumupitisha mutu mbele yetu tunapokuwa kwenye mustari, kunaweza kumufanya ajisikie vizuri. Wakati haujue jambo la kufanya ao la kusema katika hali fulani, sema ao fanya jambo fulani nzuri. Kijana ambaye tulizungumuzia mwanzoni mwa habari hii aliguswa moyo sana na wema wa misionere mwenye kuzeeka kuliko maneno aliyosema. Si jambo la kushangaza kwamba Mungu anawaomba waabudu wake ‘wapende [wema]’!—Mika 6:8.
Mezali moja inasema kama “wema hauoze.” Mezali hii inaonyesha kama tendo moja la wema linaweza kutimiza mambo mengi. Wakati mutu anayeonyesha wema anachochewa na nia nzuri na upendo kwa Mungu, wema huo unaweza kufurahisha moyo wake yeye mwenyewe na moyo wa mutu anayeonyeshwa wema. Hata kama watu hawafurahie tendo lako la wema, hilo halimaanishe kama haukufanya kitu. Machoni pa Mungu tendo hilo ni la lazima sana. Biblia inatuhakikishia kama kuwaonyesha wengine wema ni ‘kumukopesha Yehova.’ (Methali 19:17) Sababu gani usitafute nafasi ya kuwaonyesha wema watu unaokutana nao?
[Maelezo ya chini]
^ Kamusi The Oxford English inaonyesha kama maana ya kwanza-kwanza ya neno “wema” ni ‘uhusiano wa jamaa; uhusiano wa karibu; upendo unaotokana na uhusiano huo.’
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 20]
Wakati haujue jambo la kufanya ao la kusema katika hali fulani, sema ao fanya jambo fulani nzuri
[Picha katika ukurasa wa 19]
Abrahamu alibarikiwa kwa sababu ya wema wake
[Picha katika ukurasa wa 20]
Kuwaonyesha wengine wema ni kama ‘kumukopesha Yehova’