Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kristo—Nguvu za Mungu

Kristo—Nguvu za Mungu

“Kristo ni nguvu za Mungu.”1 KOR. 1:24.

1. Sababu gani mutume Paulo alisema kwamba “Kristo ni nguvu za Mungu”?

KUPITIA Yesu Kristo, Yehova alionyesha nguvu zake kwa njia za ajabu. Vitabu ine vya Injili vinatutolea mambo mengi yenye kutia nguvu imani yetu kuhusu miujiza fulani yenye Yesu alifanya. Wakati alikuwa duniani, Yesu alifanya miujiza mingi. Tunaweza kusoma habari fulani kuhusu miujiza hiyo katika Biblia. (Mt. 9:35; Lu. 9:11) Bila shaka, Yesu alionyesha nguvu za Mungu. Ndiyo sababu mutume Paulo alisema hivi: “Kristo ni nguvu za Mungu.” (1 Kor. 1:24) Lakini, miujiza ya Yesu inaweza kuwa na matokeo gani katika maisha yetu?

2. Miujiza ya Yesu inaweza kutufundisha nini?

2 Mutume Petro alisema kwamba Yesu alifanya miujiza ao “mambo ya ajabu.” (Mdo. 2:22) Miujiza yenye Yesu alifanya wakati alikuwa hapa duniani ilionyesha tu mambo makubwa zaidi yenye atafanya wakati wa Utawala wa Miaka Elfu. Miujiza hiyo ilionyesha mambo yenye Yesu atafanya katika dunia mupya ya Mungu! Pia, miujiza hiyo inatusaidia tuelewe vizuri zaidi sifa za Yesu na za Baba yake. Tuchunguze basi miujiza fulani ya Yesu, na tuone inaweza kuwa na matokeo gani katika maisha yetu ya sasa na ya wakati unaokuja.

MUUJIZA WENYE KUTUFUNDISHA UKARIMU

3. (a) Ni nini ilimuchochea Yesu afanye muujiza wake wa kwanza? (b) Huko Kana, namna gani Yesu alionyesha ukarimu?

3 Yesu alifanya muujiza wake wa kwanza kwenye karamu ya ndoa yenye ilifanyika Kana, huko Galilaya. Pengine watu wenye walifika walikuwa wengi zaidi kuliko wale wenye walialikwa. Iwe ni hivyo ao hapana, divai iliisha. Maria, mama ya Yesu, alikuwa kati ya watu wenye walialikwa. Bila shaka, kwa muda wa miaka mingi Maria alifikiria sana unabii wote wenye ulihusu mwana wake, mwenye angeitwa “Mwana wa Aliye Juu Zaidi.” (Lu. 1:30-32; 2:52) Je, aliamini kwamba mwana huyo alikuwa na nguvu fulani zenye alikuwa hajaonyesha? Jambo hilo lilionekana wazi kwenye karamu ya ndoa huko Kana. Maria na Yesu walisikilia huruma wale wenye walikuwa wameoana, na walipenda kuwasaidia ili wasipate haya. Yesu alijua kwamba wale wenye walikuwa wameoana walipaswa kuonyesha ukarimu watu wenye walialika. Kwa hiyo, aligeuza kwa njia ya muujiza litre 380 ya maji kuwa “divai nzuri.” (Soma Yohana 2:3, 6-11.) Je, Yesu alilazimishwa kufanya muujiza huo? Hapana. Alionyesha tu kwamba alihangaikia watu na kwamba alikuwa anamuiga Baba yake wa mbinguni kwa kuonyesha ukarimu.

4, 5. (a) Muujiza wa kwanza wa Yesu unatufundisha nini? (b) Muujiza wenye Yesu alifanya huko Kana, unatufundisha nini juu ya wakati unaokuja?

4 Kwa njia ya muujiza, Yesu alitoa divai nzuri kwa ajili ya watu wengi sana. Muujiza huo unatufundisha nini? Unatuhakikishia kwamba Yesu pamoja na Baba yake wanajitia pa nafasi ya wengine. Yehova na Mwana wake hawako wachoyo. Wazia sasa katika dunia mupya, namna Yehova atatumia nguvu zake kwa ukarimu ili kutayarisha karamu ya vyakula vitamu kwa ajili ya “vikundi vyote vya watu” katika dunia yote.—Soma Isaya 25:6.

5 Fikiria jambo hilo! Hivi karibuni Yehova atatutimizia mambo yenye tunahitaji kabisa. Kila mutu atakuwa na nyumba nzuri na chakula kizuri. Tunaweza kufurahi sana wakati tunafikiria vitu hivyo vizuri vyenye Yehova atatutolea kwa ukarimu katika dunia Paradiso.

Kutumia wakati wetu kwa ukarimu kunaonyesha kwamba tunaiga ukarimu wa Yesu (Ona fungu la 6)

6. Yesu alitumia nguvu zake za kufanya miujiza kwa faida ya nani, na namna gani tunaweza kumuiga?

6 Ni jambo lenye kupendeza kwamba, wakati Ibilisi alimujaribu Yesu ageuze majiwe ikuwe mikate, Yesu alikataa kutumia kwa faida yake mwenyewe uwezo wake wa kufanya miujiza. (Mt. 4:2-4) Lakini alitumia uwezo huo ili kutimiza mahitaji ya wengine. Namna gani tunaweza kuiga ukarimu wa Yesu? Yesu aliwatia moyo watumishi wa Mungu ‘wakuwe na mazoea ya kuwapa watu.’ (Lu. 6:38) Je, tunaweza kufanya hivyo kwa kualika wengine katika nyumba zetu ili kula chakula na kuzungumuzia mambo ya kiroho? Je, kisha mikutano, tunaweza kuonyesha ukarimu kwa kutumia wakati wetu ili kusaidia ndugu ao dada fulani mwenye kuwa na lazima ya musaada, kwa mufano, kumusikiliza ndugu wakati anarudilia hotuba yenye anapaswa kutoa? Ni musaada gani tunaweza kutolea watu katika mahubiri? Tunaonyesha kwamba tunaiga ukarimu wa Yesu kwa kuwatolea wengine musaada wa kimwili na wa kiroho kulingana na uwezo wetu.

‘WOTE WALIKULA NA KUSHIBA’

7. Ni hali gani itaendelea kuwa kadiri Shetani ataendelea kutawala ulimwengu huu?

7 Umasikini haukuanza leo. Yehova aliambia taifa la Israeli kwamba masikini wataendelea kupatikana katikati yao. (Kum. 15:11) Kisha miaka mingi, Yesu alisema waziwazi hivi: ‘Muna masikini pamoja nanyi sikuzote.’ (Mt. 26:11) Je, Yesu alimaanisha kwamba sikuzote masikini watakuwa katika dunia? Hapana, alimaanisha kwamba kadiri ulimwengu huu muovu wa Shetani utaendelea kuwa, masikini pia watakuwa. Kwa hiyo, tunatiwa moyo sana kuelewa kwamba miujiza yenye Yesu alifanya inaonyesha mambo mazuri sana yenye atafanya wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote. Wakati huo, tutakuwa na chakula mingi na tutatosheka kabisa!

8, 9. (a) Ni nini ilimuchochea Yesu akulishe watu wengi sana kwa njia ya muujiza? (b) Ni jambo gani linagusa moyo wako katika muujiza wa Yesu wa kukulisha watu wengi sana?

8 Mutunga-zaburi alisema hivi juu ya Yehova: ‘Unafumbua [unafungua] mukono wako na kutosheleza [kutimiza] tamaa ya kila kitu kilicho hai.’ (Zab. 145:16) ‘Kristo, nguvu za Mungu,’ alionyesha sifa ya Baba yake kwa kufungua kila mara mukono wake ili kutimiza tamaa za wafuasi wake. Hakufanya hivyo tu ili kuonyesha kwamba alikuwa na nguvu. Ni kwa sababu alihangaikia kabisa mahitaji ya wengine. Tuzungumuzie basi andiko la Mathayo 14:14-21. (Soma.) Wanafunzi wa Yesu walimukaribia na kumuambia kwamba watu wenye walikuwa wanamusikiliza hawana chakula. Hilo haliwezi tu kumaanisha kwamba wanafunzi walikuwa na njaa. Lakini linaonyesha kwamba walihangaikia kikundi cha watu wenye walikuwa na njaa, na wenye kuchoka sana kwa sababu walikuwa wametembea kwa miguu kutoka katika miji mingi ili kumufuata Yesu. (Mt. 14:13) Yesu alifanya nini?

9 Yesu alitumia mikate tano na samaki mbili ili kukulisha wanaume karibu 5000, bila kuhesabu wanawake na watoto! Wakati tunafikiria jambo hilo, je, hatuguswe moyo kuona namna Yesu alitumia nguvu zake za kufanya miujiza ili kuonyesha kwamba alipenda kabisa familia nzima-nzima? Vikundi vya watu ‘walikula na kushiba.’ Maneno hayo inaonyesha kwamba kulikuwa chakula mingi. Yesu hakuonjesha tu vikundi vya watu mukate, lakini aliwatolea chakula chenye kingeweza kuwasaidia wapate nguvu za kufanya safari yao ndefu ya kurudia nyumbani. (Lu. 9:10-17) Kisha watu hao kula, vitunga 12 vilibaki!

10. Hivi karibuni, kutakuwa badiliko gani kuhusu umasikini?

10 Leo, mahitaji ya lazima ya mamilioni ya watu haitimizwe kwa sababu ya utawala mubaya wa wanadamu. Hata ndugu na dada fulani hawana chakula cha kutosha, ni kusema, ‘hawashibe’ kabisa. Lakini, hivi karibuni, wanadamu wenye kumutii Mungu wataishi katika dunia yenye haina ukosefu wa haki na umasikini. Ikiwa ungekuwa na nguvu, je, ungewatimizia wanadamu mahitaji yao? Mungu Mweza-Yote iko na nguvu na anatamani kufanya hivyo. Ndiyo, mateso itaisha hivi karibuni!—Soma Zaburi 72:16.

11. Sababu gani uko hakika kwamba hivi karibuni Kristo atatumia nguvu zake katika dunia yote, na hilo linakuchochea kufanya nini?

11 Wakati Yesu alikuwa hapa duniani, alifanya miujiza katika eneo ndogo kwa kipindi cha miaka tatu na nusu tu. (Mt. 15:24) Kwa sababu Yesu ni Mufalme mwenye utukufu, wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu, atasaidia wanadamu katika dunia yote. (Zab. 72:8) Miujiza ya Yesu inatuhakikishia kwamba iko na uwezo na anatamani kutumia mamlaka yake hivi karibuni ili kutufanyia mambo mazuri. Hata kama hatuwezi kufanya miujiza, tunaweza kusaidia watu waelewe unabii wenye kupatikana katika Neno la Mungu lenye liliongozwa na roho yake. Unabii wa Biblia unatuhakikishia kwamba mambo mazuri iko mbele yetu. Sisi Mashahidi wa Yehova wenye kujitoa kwake, tunajua mambo mazuri ya wakati unaokuja; kwa hiyo, tunapaswa kuwatangazia watu mambo hayo. (Rom. 1:14, 15) Wakati tunafikiri sana juu ya mambo hayo, hilo litatuchochea kutangazia wengine habari njema juu ya Ufalme wa Mungu.—Zab. 45:1; 49:3.

YESU ANAZUIA NGUVU ZA ASILI ZA DUNIA

12. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kwamba Yesu anaelewa vizuri kabisa namna dunia iliumbwa?

12 Wakati Mungu aliumba dunia na vitu vyote vyenye kuwa ndani, Yesu, Mwana wake muzaliwa-pekee, ndiye alikuwa pembeni yake kama “stadi [fundi] wa kazi.” (Met. 8:22, 30, 31; Kol. 1:15-17) Ndiyo sababu Yesu anaelewa vizuri kabisa namna dunia iliumbwa. Anajua namna ya kutumia nguvu za asili za dunia kama vile volkano, matetemeko ya inchi, upepo mukubwa, zoruba, radi, mvua, na anajua namna ya kuzuia nguvu hizo.

Ni jambo gani linakufurahisha juu ya namna Yesu alitumia nguvu zake za kufanya miujiza? (Ona fungu la 13, 14)

13, 14. Toa mufano wenye kuonyesha namna Kristo anaweza kutumia uwezo wake ili kuzuia nguvu za asili.

13 Wakati alikuwa duniani, Yesu alizuia nguvu za asili. Kwa kufanya hivyo, alionyesha kwamba yeye ni “nguvu za Mungu.” Tuchunguze namna Yesu alizuia upepo mukali wenye ulionekana kuwa unatia uzima wa wanafunzi wake katika hatari. (Soma Marko 4:37-39.) Mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia anasema hivi: “Neno la Kigiriki [lenye kutafsiriwa ‘zoruba ya upepo’ kwenye Marko 4:37] linatumiwa ili kuzungumuzia kimbunga ao upepo mukubwa sana. Halimaanishe upepo wa kawaida tu . . . lakini ni upepo mukali wenye kufuatana na mingurumo ya radi, mawingu mweusi, mvua kubwa, na wenye kuangusha kila kitu chenye hakisimame muzuri.” Mathayo anataja zoruba hiyo kuwa ‘musukosuko mukubwa.’—Mt. 8:24.

14 Fikiria hali hii: Kristo ni mwenye kuchoka kwa sababu alihubiri sana. Zoruba inafanya mashua iyumbeyumbe sana, na kuingiza maji ndani. Hata kama zoruba inafanya makelele na mashua inayumba-yumba sana, Yesu anaendelea kulala usingizi. Anapumuzika kwa sababu amechoka. Wanafunzi wake wenye kuogopa wanamuamusha na kulalamika hivi: “Tuko karibu kuangamia [kukufa]!” (Mt. 8:25) Yesu anaamuka na anaambia upepo na bahari hivi: “Nyamaza! Utulie!” Na upepo mukubwa ukatulia. (Mk. 4:39) Kwa kweli, Yesu anaamuru upepo na bahari vitulie. Ni nini inatokea? ‘Kukakuwa utulivu mukubwa.’ Yesu anaonyesha kwamba iko na nguvu!

15. Namna gani Mungu Mweza-Yote ameonyesha kwamba iko na uwezo wa kuzuia nguvu za asili?

15 Yehova mwenyewe ndiye alimupatia Yesu nguvu; kwa hiyo, tuko hakika kwamba Mungu Mweza-Yote iko na uwezo mwingi sana wa kuzuia nguvu za asili. Tufikirie mifano fulani. Mbele ya Garika kuanza, Yehova alisema hivi: ‘Baada ya siku 7 nitanyesha mvua duniani siku 40 muchana na usiku.’ (Mwa. 7:4) Vilevile kwenye Kutoka 14:21, tunasoma hivi: “Yehova akaanza kuifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wenye nguvu wa mashariki.” Na kwenye Yona 1:4, tunasoma hivi: ‘Yehova mwenyewe akavumisha [akaleta] upepo mukubwa baharini, kukawa na tufani [zoruba] kubwa baharini; nayo meli [mashua] ikawa karibu kuvunjika.’ Ni jambo lenye kutia moyo sana kujua kwamba katika dunia mupya, sikuzote Yehova atazuia nguvu za asili.

16. Sababu gani tunatiwa moyo kujua kwamba Muumbaji wetu pamoja na Mwana wake muzaliwa wa kwanza wako na uwezo wa kuzuia nguvu za asili?

16 Wakati tunafikiri sana juu ya nguvu za ajabu sana za Muumbaji wetu na za “stadi [wake] wa kazi,” hilo linatusaidia kuwa na tumaini. Wakati wa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu, wanadamu wote wataishi katika usalama. Mambo kama vile upepo mukubwa, tsunamis, volkano, zoruba, ao matetemeko ya inchi haitaua tena watu ao kuwaumiza. Hatutaogopa tena mambo hayo kwa sababu “hema la Mungu [litakuwa] pamoja na wanadamu”! (Ufu. 21:3, 4) Tunaweza kuwa hakika kwamba, katika Utawala wa Miaka Elfu,Yesu atatumia nguvu za Mungu ili kuzuia nguvu za asili.

TUMUIGE MUNGU NA YESU LEO

17. Ni njia gani moja tunaweza kutumia ili kuiga Mungu na Kristo leo?

17 Bila shaka, Yehova na Yesu wanaweza kuzuia misiba yenye kuletwa na mambo kama vile mvua, upepo mukali, volkano, na zoruba. Sisi wanadamu hatuna nguvu ya kufanya hivyo; lakini tuko na uwezo kwa kadiri fulani. Namna gani tunaweza kutumia uwezo huo? Njia moja ni kutumia shauri lenye kupatikana kwenye Methali 3:27. (Soma.) Wakati ndugu na dada zetu wanapatwa na musiba, tunaweza kuwatia moyo na kuwategemeza kimwili, kiakili, na kiroho. (Met. 17:17) Kwa mufano, tunaweza kuwasaidia wakati wanapatwa na misiba ya asili. Ona maneno ya shukrani yenye dada mumoja mujane alisema kisha upepo mukubwa kuharibu nyumba yake. Alisema hivi: “Ninashukuru sana kuwa katika tengenezo la Yehova, si kwa sababu tu ya musaada wa kimwili wenye nimepokea, lakini kwa sababu ya musaada wa kiroho pia.” Ona pia maneno ya dada mwengine mwenye hajaolewa na mwenye aliona kuwa hana tena tumaini lolote na mwenye kuvurugika kisha upepo mukubwa kuharibu nyumba yake. Kisha kupokea musaada, alisema hivi: “Ninashindwa kueleza! Ninakosa maneno ya kutumia ili kueleza kabisa namna ninajisikia . . . Aksanti, Yehova!” Tunafurahi kwa sababu tuko kati ya ndugu na dada wenye kuhangaikia kabisa mahitaji ya wengine. Ni jambo lenye kufurahisha sana kuona namna Yehova na Yesu Kristo wanatuhangaikia kabisa sisi watumishi wa Mungu.

18. Ni nini inakufurahisha juu ya jambo lenye lilimuchochea Yesu afanye miujiza?

18 Wakati alikuwa anahubiri hapa duniani, Yesu alionyesha kwamba yeye ni “nguvu za Mungu.” Lakini, ni nini ilimuchochea? Hakutumia hata kidogo nguvu zake ili kushangaza wengine ao kwa faida yake mwenyewe. Lakini, miujiza yenye alifanya ilionyesha kwamba anapenda wanadamu. Tutazungumuzia jambo hilo katika habari yenye kufuata.