Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA  47

Namna Tunaweza Kuendelea Kupendana Sana

Namna Tunaweza Kuendelea Kupendana Sana

“Tuendelee kupendana, kwa sababu upendo unatoka kwa Mungu.”—1 YO 4:7.

WIMBO 109 Tupendane Sana Kutoka Ndani ya Moyo

KIFUPI YA HABARI a

1-2. (a) Juu ya nini mutume Paulo alisema kama upendo njo sifa ‘kubwa zaidi’? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

 WAKATI mutume Paulo alikuwa nazungumuzia imani, tumaini, na upendo, alimazia kwa kusema hivi: “Jambo la mukubwa zaidi kati ya mambo hayo [ao zile sifa] ni upendo.” (1 Ko. 13:13) Juu ya nini Paulo alisema vile? Wakati wenye kuya hatutakuwa na lazima ya kuwa na imani katika ahadi za Mungu kuhusu ulimwengu mupya ao kuwa na tumaini kama zile ahadi zitatimia, kwa sababu zitakuwa zilishatimia. Lakini tutaendelea kuwa na lazima ya kumupenda Yehova na kuendelea kupenda watu. Na hata upendo wetu kwao utaendelea kuongezeka milele.

2 Juu tutaendelea kuwa na lazima ya upendo, tutazungumuzia maulizo tatu. Kwanza, juu ya nini tunapaswa kupendana? Pili, namna gani tunaweza kuonyeshana upendo? Tatu, namna gani tunaweza kuendelea kukomalisha upendo wetu kwa wengine?

JUU YA NINI TUNAPASWA KUPENDANA?

3. Ni sababu gani njo zinatuchochea kupendana?

3 Juu ya nini ni jambo ya maana tupendane? Kuko sababu mingi. Sababu moya ni kwamba upendo unatutambulisha kuwa Wakristo wa kweli. Yesu aliambia hivi mitume wake: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu—kama muko na upendo kati yenu.” (Yoh. 13:35) Zaidi ya ile, upendo unatusaidia tuendelee kuwa na umoja. Paulo alisema kama upendo “ni kifungo kikamilifu cha umoja.” (Kol. 3:14) Lakini kuko sababu ingine ya maana yenye inapaswa kutuchochea kupendana. Mutume Yohana aliandikia hivi waamini wenzake: “Yeyote mwenye anamupenda Mungu anapaswa pia kumupenda ndugu yake.” (1 Yo. 4:21) Wakati tunaonyeshana upendo, tunaonyesha kama tunamupenda Mungu.

4-5. Toa mufano wenye kuonyesha kama kuko uhusiano kati ya upendo wetu kwa Mungu na upendo wetu kwa wengine.

4 Kuko uhusiano gani kati ya upendo wetu kwa ndugu na dada zetu na upendo wetu kwa Mungu? Kwa mufano, wazia uhusiano wenye unakuwaka kati ya moyo wetu na viungo vingine vya mwili. Wakati munganga anatupima ku mukono juu ajue tension yetu, anaweza pia kujua hali ya moyo wetu. Ile mufano inatufundisha nini?

5 Sawa tu vile munganga anaweza kujua hali ya moyo wetu wakati anatupima tension, tunaweza pia kujua ikiwa upendo wetu kwa Mungu ni wenye nguvu kwa kuchunguza upendo wetu kwa wengine. Ikiwa tunatambua kama upendo wetu kwa waamini wenzetu umepunguka, ile inaweza kuonyesha kama upendo wetu kwa Mungu umepunguka pia. Lakini ikiwa tunazoea kuonyesha waamini wenzetu upendo, ile ni alama yenye kuonyesha kama upendo wetu kwa Mungu ni wenye nguvu.

6. Ikiwa upendo wetu kwa ndugu na dada zetu uko napunguka, juu ya nini tunapaswa kukamata ile jambo kwa uzito? (1 Yohana 4:7-9, 11)

6 Kama upendo wetu kwa ndugu na dada zetu uko napunguka, tunapaswa kukamata ile jambo kwa uzito. Juu ya nini? Juu inaweza kumaanisha kama tuko mu hatari ya kiroho. Mutume Yohana alionyesha wazi ile jambo wakati alisema kama “mutu mwenye hamupendi ndugu yake mwenye amemuona, hawezi kumupenda Mungu mwenye hajaonaka.” (1 Yo. 4:20) Ile inatufundisha nini? Yehova anatufurahia ikiwa tu ‘tunapendana.’—Soma 1 Yohana 4:7-9, 11.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUONYESHANA UPENDO?

7-8. Tunaweza kuonyeshana upendo mu njia gani mbalimbali?

7 Mu Neno ya Mungu tunapata tena na tena amri ya ‘kupendana.’ (Yoh. 15:12, 17; Ro. 13:8; 1 Te. 4:9; 1 Pe. 1:22; 1 Yo. 4:11) Lakini upendo ni sifa ya moyo ao sifa ya ndani, na hakuna mwanadamu mwenye anaweza kuona mambo yenye kuwa mu moyo wetu. Kwa hiyo, namna gani upendo wetu kwa wengine unaweza kuonekana? Kupitia maneno na matendo.

8 Tunaweza kuonyesha ndugu na dada zetu upendo mu njia mbalimbali. Hapa kuko mifano fulani: “Museme kweli mumoja na mwingine.” (Zek. 8:16) “Muendelee kuwa na amani mumoja na mwingine.” (Mk. 9:50) Mukuwe wa kwanza “katika kuonyeshana heshima.” (Ro. 12:10) “Mukaribishane.” (Ro. 15:7) “Muendelee . . . “kusameheana.” (Kol. 3:13) “Muendelee kubebeana mizigo mizito.” (Gal. 6:2) “Muendelee kufarijiana.” (1 Te. 4:18) “Muendelee . . . Kujengana.” (1 Te. 5:11) ‘Musali kwa ajili ya mutu na mwenzake.’—Yak. 5:16.

Tunaweza kusaidia namna gani muamini mwenzetu mwenye iko mu magumu? (Ona fungu ya 7-9)

9. Juu ya nini kufariji wengine ni njia ya maana ya kuonyesha kama tunawapenda? (Ona picha.)

9 Tuzungumuzie njia moja ya kuonyesha upendo yenye tulitaja mu fungo yenye kutangulia. Tutachunguza hii maneno ya Paulo: “Muendelee kufarijiana.” Juu ya nini kufariji wengine ni njia ya maana ya kuonyesha kama tunawapenda? Kulingana na kitabu fulani yenye kuzungumuzia mambo ya Biblia, neno “kufariji” yenye Paulo alitumia maana yake kusimama pembeni ya mutu ili kumutia moyo wakati iko napambana na majaribu ya nguvu. Kwa hiyo wakati tunafariji muamini mwenzetu mwenye iko mu magumu, tunamusaidia asimame na aendelee kutembea mu barabara ya uzima. Kwa hiyo, kila wakati wenye tunafariji ndugu ao dada yetu, tunaonyesha kama tunamupenda.—2 Ko. 7:6, 7, 13.

10. Kuko uhusiano gani kati ya kusikia huruma na kufariji?

10 Kuko uhusiano wa karibu sana kati ya kusikilia mutu huruma na kumufariji. Namna gani? Kama tunasikilia mutu huruma tutachochewa kumufariji na kujikaza kumusaidia. Kwa hiyo, kwanza tunasikia huruma na kisha tunafariji. Ona namna Paulo anaonyesha uhusiano wenye kuwa kati ya huruma ya Yehova na faraja yenye anatoa. Paulo anasema kama Yehova ni “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote.” (2 Ko. 1:3) Mu hii andiko Paulo anatumia maneno “rehema nyingi” ili kuzungumuzia hali ya kusikilia wengine huruma. Kwa hiyo, Mungu ni Baba ao Chanzo cha rehema nyingi kwa sababu sifa ya huruma inatoka kwake. Na ile huruma inamuchochea atufariji “katika majaribu yetu yote.” (2 Ko. 1:4) Sawa vile maji yenye kutiririka kutoka kwenye chemchemi inafanyaka mutu mwenye alikuwa na kiu ajisikie muzuri wakati anaikunywa, Yehova anafanyaka wale wenye kuwa na huzuni wajisikie muzuri na wafarijike. Kama Yehova, namna gani na siye tunaweza kusikilia wengine huruma na kuwafariji? Njia moja ya kufanya vile ni kukomalisha katika moyo wetu sifa zenye zinaweza kutusaidia tufariji wengine. Ni sifa gani?

11. Kulingana na Wakolosai 3:12 na 1 Petro 3:8, tunapaswa kukomalisha sifa gani zingine ili tuendelee kuwa na upendo wenye unatuchochea kufariji wengine?

11 Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na upendo wenye utatuchochea ‘tuendelee kufarijiana’ kila siku? Tunapaswa kukomalisha sifa sawa vile kujitia pa nafasi ya wengine, kuwa na upendo wa kindugu, na fazili. (Soma Wakolosai 3:12; 1 Petro 3:8.) Zile sifa zitatusaidia namna gani? Wakati tunakuwa na huruma na hizi sifa zingine, tutakuwa na hamu sana ya kufariji wale wenye kuwa mu magumu. Sawa vile Yesu alisema “kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo. Mutu muzuri anatosha mambo ya muzuri katika hazina yake ya muzuri.” (Mt. 12:34, 35) Kufariji ndugu na dada wakati wako na lazima kabisa ya faraja ni njia ya muzuri sana ya kuonyesha kama tunawapenda.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUENDELEA KUPENDANA SANA?

12. (a) Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuwa waangalifu? (b) Tutazungumuzia sasa maulizo gani?

12 Siye wote tunapenda ‘kuendelea kupendana.’ (1 Yo. 4:7) Lakini ni jambo ya maana tukumbuke kama Yesu alionya hivi: “Upendo wa watu wengi utapoa.” (Mt. 24:12) Yesu hakukuwa nasema kama wanafunzi wake wengi wataacha kupendana. Hata vile, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusichochewe na roho ya kukosa upendo yenye kuwa mu hii ulimwengu. Tukiwa na ile wazo mu akili tuzungumuzie hii ulizo ya maana: Tunaweza kujua namna gani ikiwa upendo wetu kwa ndugu zetu uko wenye nguvu?

13. Nini njo inaweza kujaribu upendo wetu?

13 Njia moja ya kujua kama upendo wetu uko nguvu ni kuchunguza namna tunatendaka wakati tunakutana na hali fulani-fulani. (2 Ko. 8:8) Mutume Petro anazungumuzia moja kati ya zile hali. Anasema hivi: “Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.” (1 Pe. 4:8) Kwa hiyo, uzaifu na makosa ya wengine vinaweza kujaribu upendo wetu kwao.

14. Kulingana na 1 Petro 4:8, tuko na lazima ya aina gani ya upendo? Toa mufano.

14 Sasa tuchunguze kwa uangalifu maneno ya Petro. Sehemu ya kwanza ya mustari wa munane inaonyesha aina ya upendo yenye tunapaswa kuwa nayo, ni kusema, “upendo mwingi.” Neno “mwingi” yenye Petro alitumia inamaanisha neno kwa neno “kupanuka.” Sehemu ya pili ya ile andiko inaonyesha matokeo ya upendo mwingi: unafunika zambi za ndugu zetu. Ni sawa vile upendo ulikuwa nguo yenye inaweza kupanuka yenye tunakamata na mikono mbili na tunaanza kuikokota na inapanuka mupaka inafunika hapana zambi moya ao mbili, lakini “zambi nyingi.” ‘Kufunika’ ni namna ingine ya kusema kusamehe. Sawa tu vile nguo inaweza kufunika kasoro, upendo unaweza kufunika uzaifu na makosa ya wengine.

15. Kama upendo wetu kwa ndugu na dada zetu uko wenye nguvu sana, tutaweza kufanya nini? (Wakolosai 3:13)

15 Upendo wetu unapaswa kuwa nguvu sana juu tuweze kusamehe makosa ya waamini wenzetu, hata kama wakati fulani ile inaomba kujikaza sana. (Soma Wakolosai 3:13.) Wakati tunasamehe wengine tunaonyesha kama upendo wetu uko nguvu na kama tunapenda kumufurahisha Yehova. Nini ingine inaweza kutusaidia tusikazie uzaifu na makosa ya wengine?

Sawa vile tu tunawekaka picha za muzuri na kuvuta za mubaya, tunafurahia kuchunga wakati wa muzuri wenye tulipitisha na waamini wenzetu na kuepuka kufikiria wakati wa mubaya (Ona fungu ya 16-17)

16-17. Ni nini itatusaidia tusikazie makosa ya kidogo-kidogo ya wengine? Toa mufano. (Ona pia picha.)

16 Kazia sifa za muzuri za ndugu na dada zako, hapana uzaifu wao. Kwa mufano wazia munakutana pamoya na ndugu na dada ili kujifurahisha. Munapitisha wakati ya muzuri pamoja, na ku mwisho munakamata picha pamoja. Juu haujue kama ile picha ya kwanza itatoka muzuri, unakamata picha mbili zingine. Sasa uko na picha tatu. Lakini mu picha moya unaona kama ndugu fulani alifunga sura. Sasa utafanya nini na ile picha? Utavuta ile picha juu ungali na picha zingine mbili kwenye kila mutu iko nacheka, kutia ndani ule ndugu.

17 Zile picha ziko sawa vile mambo yenye tunachunga mu akili. Mara mingi tunachungaka mu akili wakati za muzuri zenye tulipitisha pamoya na ndugu na dada zetu. Lakini wazia wakati moya kati ya zile, ndugu ao dada alisema ao kufanya jambo fulani yenye haukufurahia. Utafanya nini juu ya ile? Hauone kama ni muzuri uivute mu akili sawa vile ulivuta ile picha moya? (Mez. 19:11; Efe. 4:32) Sawa vile hatupoteze kitu kama tunavuta picha moya ya mubaya, hatupoteze kitu kama tunasahau wakati moya ya mubaya yenye tulipitisha pamoja na ndugu na dada yetu, juu tuko na wakati zingine za mingi za muzuri zenye tumepitisha pamoja naye. Na zile njo tunapaswa kuweka mu akili na kuzifurahia.

JUU YA NINI UPENDO NI WA LAZIMA SANA LEO

18. Mu hii habari tumezungumuzia nini kuhusu upendo?

18 Juu ya nini tunapenda kuendelea kupendana sana? Sawa vile tuliona, wakati tunaonyesha ndugu na dada zetu upendo, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova. Tunaonyesha namna gani kama tunapenda waamini wenzetu? Njia moya ya kufanya vile ni kwa kuwafariji. Tutaweza ‘kuendelea kufarijiana’ ikiwa tuko na huruma. Namna gani tunaweza kuendelea kupendana sana? Kwa kufanya yetu yote ili kusamehe makosa ya wengine.

19. Juu ya nini ni jambo ya maana sana kuonyeshana upendo, zaidi sana leo?

19 Juu ya nini ni jambo ya maana sana leo kuonyeshana upendo? Ona sababu yenye Petro alitoa. Alisema: “Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo, . . . mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi.” (1 Pe. 4:7, 8) Kadiri mwisho wa huu ulimwengu muovu unaendelea kukaribia, tunaweza kutazamia nini? Yesu alitabiri hivi juu ya wanafunzi wake: “Mutachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.” (Mt. 24:9) Juu tuweze kupambana na ile chuki tunapaswa kuendelea kuwa na umoja kati yetu. Kama tunafanya vile Shetani hataweza kututenganisha juu tunaunganishwa na upendo, wenye ni “kifungo kikamilifu cha umoja.”—Kol. 3:14; Flp. 2:1, 2.

WIMBO 130 Tusameheane

a Kuliko wakati mwingine wowote, leo ni jambo ya maana sana kuonyesha ndugu na dada zetu upendo. Juu ya nini? Na namna gani tunaweza kuonyesha upendo zaidi?