Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Kumutumainia Yehova Kuliniletea Usalama wa Kweli

Kumutumainia Yehova Kuliniletea Usalama wa Kweli

WAKATI watu wananiuliza kuhusu maisha yangu, mara mingi ninawaambiaka “niko muzigo mu mikono ya Yehova!” Ninamaanisha kama, sawa vile tu ninabebaka muzigo wangu kila fasi kwenye ninapenda, ninapenda Yehova na tengenezo yake wafanye vile juu yangu, ni kusema waniambie fasi ya kuenda na wakati wa kufanya vile. Nilikubali migao yenye ilikuwa nguvu, na wakati fulani ilikuwa hatari. Lakini nilijifunza kama kumutumainia Yehova njo kunaletaka usalama wa kweli.

NAMNA NILIANZA KUMUTUMAINIA YEHOVA

Nilizaliwa mu 1948 mu kijiji ya kidogo ya kusini-mangaribi mwa Nigeria. Mu ile kipindi, baba yangu mudogo Moustapha na kaka yangu Wahabi, walibatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Wakati nilikuwa na miaka 9, baba yangu alikufa. Nilivunjika moyo sana. Wahabi aliniambia kama tunaweza tena kumuona baba wakati wa ufufuo. Ile mawazo yenye kutia moyo ilinichochea kujifunza Biblia. Nilibatizwa mu 1963. Ndugu zangu wengine tatu walibatizwa pia.

Mu 1965, nilienda kwa ndugu yangu Wilson mu muji wa Lagos na nilifurahia kupitisha wakati pamoya na mapainia wengine wa kawaida mu kutaniko ya Igbobi. Furaha yao na bidii yao ilinichochea, na mu 1968 miye pia nikakuwa painia.

Ndugu fulani wa ku Beteli, Albert Olugbebi, alifanya mukutano wa pekee pamoya na siye vijana. Na mu ile mukutano, alionyesha kama kulikuwa lazima ya mapainia wa pekee mu sehemu ya kaskazini ya Nigeria. Ningali nakumbuka hii maneno yenye kuchochea ya Ndugu Olugbebi: “Muko vijana na munaweza kutumia wakati wenu na nguvu yenu kwa ajili ya Yehova. Mashamba iko wazi.” Juu nilipenda sana kuiga roho ya kujitolea ya nabii Isaya, nilijaza fomu.—Isa. 6:8.

Mu Mwezi wa 5, 1968, niliwekwa kuwa painia wa pekee mu muji wa Kano, kaskazini mwa Nigeria. Ile ilikuwa wakati wa vita ya Biafran (1967-1970). Ile vita iliua watu wengi na kuletea watu wengi mateso kaskazini mwa Nigeria, kisha ikahamia mashariki mwa Nigeria. Ndugu fulani mwenye alikuwa na nia ya muzuri alijaribu kunisadikisha nisiende kule. Lakini nilimuambia hivi: “Aksanti kwa kunihangaikia, lakini kama Yehova anapenda nimutumikie mu ule mugao, niko hakika kama atakuwa pamoya na miye.”

KUMUTUMAINIA YEHOVA MU ENEO YENYE KUWA MU HALI YA MUBAYA KWA SABABU YA VITA

Hali ilikuwa mubaya sana mu muji wa Kano. Vita ya wenywe kwa wenyewe ilifanya watu wengi wateseke mu ule muji. Mu mahubiri, wakati fulani tulikuwa nakutana na maiti ya watu wenye walikuwa wameuawa mu ile vita. Hata kama mbele ya pale kulikuwa makutaniko mingi mu ile eneo, ndugu wengi walikuwa wamekimbia vita. Kulibakia wahubiri wenye hawakufika hata 15, na walikuwa na woga sana na wenye kuvunjika moyo. Wale ndugu na dada walifurahi sana wakati siye mapainia wa pekee sita, tulifika. Tuliwatia moyo na walijisikia muzuri zaidi. Tuliwasaidia warudilie tena mambo ya kiroho na waanze tena kutuma ripoti ku tawi na kutuma ombi za vichapo.

Siye mapainia wa pekee tulianza kujifunza luga ya Hausa. Wakati watu wa mu ile eneo walisikia ujumbe wa Ufalme mu luga yao, wengi wao walitusikiliza. Lakini watu wa mu dini yenye ilikuwa imeenea mu ile muji hawakufurahia kazi yetu ya kuhubiri. Kwa hiyo, tulipaswa kuwa waangalifu sana. Siku moya mwanaume fulani alitukimbiza na kisu miye na mwenzangu. Jambo ya kufurahisha ni kwamba tulimushinda mbio na vile njo tuliponyoka. Hata kama kulikuwa hatari, Yehova alitusaidia ‘tuishi katika usalama’na hesabu ya wahubiri ikaanza kuongezeka. (Zb. 4:8) Leo, mu muji wa Kano muko wahubiri zaidi ya 500 wenye kuwa mu makutaniko 11.

KUPAMBANA NA UPINZANI KATIKA NIGER

Niko painia wa pekee katika Niamey, Niger

Kisha kutumikia mu muji wa Kano kwa miezi kidogo, Mwezi wa 8, 1968, nilitumwa Niamey, muji mukubwa wa Jamuhuri ya Niger pamoya na mapainia wengine wa pekee wawili. Bila kukawia tulitambua kama Niger, yenye kuwa mangaribi mwa Afrika, iko kati ya inchi zenye kuwa na kifukutu zaidi mu dunia. Zaidi ya kujikaza kuzoea kifukufu, tulipaswa pia kujifunza Kifaransa. Hata kama tulikuwa na ile magumu, tulimutumainia Yehova na tulianza kuhubiri mu muji mukubwa pamoya na wahubiri kidogo wenye walikuwa naishi mu ule muji. Mu wakati kidogo tu karibu kila mutu mu Niamey mwenye alijua kusoma alipata kitabu ya kusaidia kujifunza Biblia, ni kusema kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele. Na hata watu walikuwa nakuya kututafuta juu tuwapatie kitabu!

Bila kukawia, tulitambua kama wakubwa wa serikali hawakufurahia Mashahidi wa Yehova. Mu Mwezi wa 7, 1969, tulikusanyika kwa mara ya kwanza mu inchi kwa ajili ya mukusanyiko wa muzunguko, na watu karibu 20 walihuzuria. Tulikuwa nangoya kwa hamu ubatizo wa wahubiri wapya wawili. Lakini siku ya kwanza ya mukusanyiko, polisi walifika na kusimamisha programu. Walikamata mapainia wa pekee na mwangalizi wa muzunguko na kuwapeleka ku biro ya polisi. Kisha kutuuliza maulizo, walituambia turudie siku yenye kufuata. Juu tulitambua kama hali inaweza kuwa mubaya, tulifanya mipango ya kutoa hotuba ya ubatizo mu nyumba ya mutu fulani na tukabatiza kwa uficho wale wahubiri mu mutoni.

Kisha majuma fulani, serikali ilitufukuza miye na mapainia wengine wa pekee tano. Walitupatia saa 48 ya kutoka mu inchi. Na siye wenyewe njo tulipaswa kutafuta namna ya kufanya vile. Tulitii na mara moya tukaenda ku biro ya tawi ya Nigeria kwenye tulipewa migao ya mupya.

Nilitumwa mu kijiji fulani ya Nigeria yenye kuitwa Orisunbare, kwenye nilipata matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri pamoya na kikundi kidogo ya wahubiri wenye walikuwa naishi kule. Lakini kisha miezi sita biro ya tawi iliniomba nirudie Niger miye peke. Ku mwanzo nilishangaa na nilikuwa na wasiwasi kidogo. Lakini nilikuwa na hamu ya kuonana tena na ndugu wa Niger!

Nilirudia Niamey. Siku yenye ilifuata mufanyabiashara fulani wa kutoka Nigeria alitambua kama nilikuwa Shahidi, na akaanza kuniuliza maulizo juu ya Biblia. Nilijifunza naye Biblia na akaacha kuvuta tumbako na kunywa sana, kisha akabatizwa. Nilifurahia kuhubiri pamoya na ndugu na dada mu maeneo mbalimbali ya Niger, na kuona namna, kadiri miaka ilikuwa napita, pole kwa pole watu walikuwa nakubali kweli. Wakati nilifika, mu Niger mulikuwa Mashahidi 31 na wakati niliondoka walikuwa 69.

“HATUJUE MENGI JUU YA KAZI YA UFALME MU GUINÉE”

Ku mwisho-mwisho wa mwaka wa 1977, nilirudia Nigeria ili kupata mazoezi. Ku mwisho wa majuma tatu ya mazoezi, Ndugu Malcolm Vigo, muratibu wa Halmashauri ya Tawi alinisomea barua kutoka ku tawi ya Sierra Leone. Ndugu wa Sierra Leone walikuwa natafuta ndugu mwenye hayaoa mwenye afya ya muzuri, mwenye kuwa painia, na mwenye kujua kuzungumuza Kiingereza na Kifaransa juu akuwe mwangalizi wa muzunguko katika Guinée. Ndugu Vigo aliniambia kama nilikuwa nazoezwa kwa ajili ya ule mugao. Alinifasiria waziwazi kama haikukuwa mugao wa mwepesi. Alinishauria hivi: “Ufikiri muzuri mbele ya kuitika.” Mara moya nilijibia hivi: “Juu Yehova njo ananituma kule, nitaenda.”

Nilienda Sierra Leone na nikakutana na ndugu ku biro ya tawi. Ndugu moya wa mu Halmashauri ya Tawi aliniambia hivi: “Hatujue mengi juu ya kazi ya Ufalme mu Guinée.” Hata kama tawi ya Sierra Leone njo ilikuwa nasimamia kazi ya kuhubiri mu inchi jirani ya Guinée, ilikuwa nguvu kupashana habari na wahubiri wa mu ile inchi kwa sababu ya muvurugo mu mambo ya politike wenye ulikuwa kule. Walikuwa wamejikaza mara mingi kutuma mujumbe mu inchi ya Guinée lakini hawakuweza kufanya vile. Kwa hiyo, nilitumwa Conakry, muji mukubwa wa Guinée ili nijaribu kupata ruhusa kwa wakubwa wa serikali ya kubakia kule.

“Juu Yehova njo ananituma kule, nitaenda”

Wakati nilifika Conakry, nilienda ku ambasade ya Nigeria na nilionana na ambasadere. Nilimuambia kama nilipenda kuhubiria mu inchi ya Guinée. Aliniambia nisibakie kule juu ningeweza kuwa mu hatari ya kufungwa ao hata kutendewa mubaya. Aliniambia hivi: “Rudia Nigeria na uhubiri kule.” Nilimujibu: “Naazimia kabisa kubakia.” Kwa hiyo, akaandikia waziri wa mambo ya ndani wa Guinée barua juu anisaidie, na waziri akanipokea muzuri.

Kisha wakati kidogo, nilirudia ku biro ya tawi ya Sierra Leone na kujulisha ndugu uamuzi wa waziri. Ndugu walifurahi sana kuona vile Yehova alibariki safari yangu. Serikali iliniruhusu kubakia Guinée!

Mu kazi ya muzunguko katika Sierra Leone

Kuanzia mwaka wa 1978 mupaka 1989, nilikuwa mwangalizi wa muzunguko katika Guinée, Sierra Leone, na mwangalizi wa badala katika Liberia. Ku mwanzo, nilikuwa nagonjwa-gonjwa. Wakati fulani niligonjwea mu maeneo ya mbali. Lakini ndugu walifanya yao yote ili kunipeleka ku hopitali.

Wakati fulani niligonjwa malaria ya nguvu na manyoka ya mu tumbo. Wakati nilipona nilipata habari kama ndugu walikuwa walishaanza kuzungumuza juu ya fasi kwenye watanizika. Hata kama nilipambana na zile hali za nguvu, hakuna siku nilifikiria kuacha mugao wangu. Na ninaendelea kuwa hakika kama usalama wa kweli na wenye kudumu unatoka kwa Mungu mwenye anaweza kutufufua.

MIYE NA BIBI YANGU TUNAMUTUMAINIA YEHOVA

Siku ya ndoa yetu mu 1988

Mu 1988, nilikutana na Dorcas, dada painia, munyenyekevu, na wa kiroho sana. Tulifunga ndoa, na tukaanza kutumika pamoya mu muzunguko. Dorcas amekuwa bibi mwenye upendo na mwenye kujitoa kabisa. Ili kutembelea makutaniko, tulikuwa natembea kwa muguu safari za murefu, za kufikia hata kilometre 25; tulifanya zile safari tukiwa tumebeba mizigo yetu. Ili kutembelea makutaniko ya mbali sana, tulitumia njia yoyote ya kusafiri yenye ilipatikana. Na tulisafiri mu barabara zenye kujaa matope na zenye kuwa na mashimo.

Dorcas ni mwenye uhodari sana. Kwa mu- fano, wakati fulani tulipaswa kuvuka mitoni yenye kuwa na mamba. Mu safari fulani yenye tulifanya kwa siku tano, vilalo vya mbao vyenye vilikuwa juu ya mutoni vilikuwa vimevunjika. Tulipaswa kutumia mutumbwi. Wakati Dorcas alisimama ili kutoka mu mutumbwi, alianguka mu maji ya murefu. Siye wote hatukujua kuogelea na mu ile mutoni mulikuwa mamba. Jambo ya kufurahisha ni kwamba, vijana fulani walishuka ndani ya ile maji na wakamuokoa. Kwa wakati fulani miye naye tulilota ndoto za kuogopesha kwa sababu ya ile tukio. Lakini tuliendelea na mugao wetu.

Watoto wetu, Jahgift na Eric, wamekuwa zawadi kutoka kwa Yehova

Ku mwanzo-mwanzo wa mwaka wa 1992, tulishangaa kujua kama Dorcas iko na mimba. Ile ingekuwa mwisho wa utumishi wetu wa wakati wote? Tulijiambia hivi: “Yehova ametupatia zawadi.” Kwa hiyo tuliamua kupatia mutoto wetu mwanamuke jina Jahgift (maana yake zawadi kutoka kwa Yehova). Miaka ine kisha Jahgift kuzaliwa, mudogo yake mwanaume, Eric, alizaliwa. Watoto wetu wote wawili wamekuwa zawadi kutoka kwa Yehova. Jahgift alitumikia kwa wakati fulani ku biro ya kutafsiri katika Conakry, na Eric ni mutumishi wa huduma.

Hata kama Dorcas aliacha kutumikia kama painia wa pekee, aliendelea kutumikia kama painia wa kawaida, hata wakati alikuwa nakomalisha watoto wetu. Kwa musaada wa Yehova, niliendelea kuwa mu utumishi wa pekee wa wakati wote. Kisha watoto wetu kukomaa, Dorcas alianza tena kutumikia kama painia wa pekee. Sasa miye na Dorcas tuko wamisionere katika Conakry.

MWENYE ANATOA USALAMA WA KWELI

Siku zote nimeenda kwenye Yehova anapenda niende. Mara kwa mara miye na bibi yangu tumeona namna anatulinda na namna anatubariki. Kumutumainia Yehova kumefanya tusikuwe na mahangaiko mingi yenye wale wenye wanatumainia vitu vya kimwili wako nayo. Kupitia mambo yenye tumejionea, miye na Dorcas tumejifunza kama usalama wa kweli unatoka kwa Yehova, “Mungu wa wokovu wetu.” (1 Ny. 16:35) Niko hakika kama uzima wa wale wote wenye kumutumainia, ‘utafungwa salama katika mufuko wa uzima karibu na Yehova.’—1 Sa. 25:29.