Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kujua Kama Mungu Anakuhangaikia Kutakuletea Faida Gani?

Kujua Kama Mungu Anakuhangaikia Kutakuletea Faida Gani?

Mungu aliumba mwili wetu na uwezo wa ajabu wa kupona. Wakati mutu mwenye kuwa na afya ya muzuri anajikata kidonda, anajikwaruza ao kujiumiza, “mwili wake unaanza kutumia uwezo wa ajabu wa kuponyesha vidonda, vikubwa na vidogo.” (Johns Hopkins Medicine) Mara moja mwili unafanya jambo fulani ili kuzuia damu kuvuya, kupanua mishipa ya damu, kuponyesha kidonda, na kufanya ngozi ikuwe nguvu.

FIKIRIA JAMBO HILI: Ikiwa Muumbaji aliumba mwili wetu na uwezo wa kuponyesha kidonda, tunaweza kuwa na imani katika ahadi yake ya kutusaidia pia tupone vidonda vyetu vya moyoni. Muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: “Anaponyesha wenye kuvunjika moyo; anafunga vidonda vyao.” (Zaburi 147:3) Lakini ikiwa unateseka moyoni kwa sababu ya mambo fulani yenye yanakupata sasa ao yalikupata zamani, namna gani unaweza kuwa hakika kama Yehova atafunga vidonda vyako​—leo na wakati wenye kuja?

MAMBO YENYE BIBLIA INATUFUNDISHA KUHUSU UPENDO WA MUNGU

Mungu anaahidi hivi: “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia.” (Isaya 41:10) Mutu mwenye anajua kama Yehova anamuhangaikia, iko na amani ya akili na nguvu ya kupambana na majaribu mengi. Mutume Paulo aliita amani hiyo ya moyoni “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” Paulo aliongeza hivi: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.”​—Wafilipi 4:4-7, 9, 13.

Maandiko yanatusaidia tukuwe na imani katika ahadi za Yehova kuhusu wakati wenye kuja wa wanadamu. Kwa mufano, andiko la Ufunuo 21:4, 5 linatuambia mambo yenye atafanya na sababu gani tunaweza kuwa hakika kama atayafanya:

  • “Atapanguza kila chozi” katika macho ya watu. Yehova atamaliza mateso yetu yote na mahangaiko, hata yale wengine wanaweza kuona kuwa ni ya kidogo sana.

  • “Mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme” katika utukufu wa mbinguni, ni kusema, Mufalme Mweza-Yote wa viumbe vyote atatumia nguvu na mamlaka yake ili kuzuia mateso na kutupatia musaada wenye tuko nao lazima.

  • Yehova anatuhakikishia kama ahadi zake ni za ‘uaminifu na za kweli.’ Hilo linamaanisha kuwa, atalinda sifa yake ya kuwa Mungu mwenye kutimiza ahadi zake.

“‘Atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.’ Na Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme akasema: ‘Angalia! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Tena anasema: ‘Andika, kwa maana maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’”​—Ufunuo 21:4, 5.

Ulimwengu pamoja na Biblia vinafunua sifa za Baba yetu wa mbinguni. Uumbaji unatupatia mualiko wa kimya-kimya wa kumukaribia Mungu, lakini Biblia inafanya mualiko huo ukuwe wazi. Inasema hivi: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Andiko la Matendo 17:27 linasema: “Haiko mbali sana na kila mumoja wetu.”

Kadiri unachukua wakati wa kumujua Mungu, utakuwa na imani zaidi kuwa ‘anakuhangaikia.’ (1 Petro 5:7) Kuwa na imani hiyo katika Yehova kutakuletea faida gani?

Fikiria mufano wa Toru, mwenye kuishi katika inchi ya Japani. Alikomalishwa na mama Mukristo, lakini akajiingiza katika kikundi cha watu wenye jeuri chenye kuitwa yakuza, Mafia wa Japani. Anasema, “Niliamini kama Mungu ananichukia, na nilijisikia kama kufa kwa watu wenye walikuwa karibu na mimi, zaidi sana wale wenye nilikuwa ninapenda sana, ni malipizi yenye nilikuwa ninapata.” Toru anasema kama kuwa katika kikundi hicho na kuwa na mawazo hayo ya mubaya, kulimufanya “akuwe na moyo mugumu na akose huruma.” Kuhusu shabaha yake, anakumbuka, “nilipenda nikufe kijana kisha kuua mutu mwenye kujulikana kuliko mimi na kwa hiyo kujifanyia jina.”

Lakini, wakati Toru na bibi yake, Hannah, walijifunza Biblia, Toru alifanya mabadiliko makubwa katika maisha yake na katika namna yake ya kuona mambo. Hannah anasema, “Nilijionea mimi mwenyewe namna bwana yangu alikuwa anafanya mabadiliko.” Sasa, Toru anasema kwa uhakika: “Kuko kabisa Mungu mwenye anahangaikia kila mumoja wetu. Hapendi mutu yeyote akufe, na iko tayari kusamehe wale wote wenye wanatubu kikweli makosa yao. Anasikiliza mambo yenye hatuwezi kuambia mutu mwengine yeyote na yenye wengine hawawezi kuelewa. Hivi karibuni, Yehova atamaliza matatizo yote, mateso, na maumivu. Hata leo, anatusaidia katika njia yenye hatuwazie kabisa. Anatupenda na anatusaidia wakati tuko katika hali ya chini.”​—Zaburi 136:23.

Kama vile mufano wa Toru unaonyesha, kujua kama Mungu iko na uwezo wa kumaliza magumu na kupanguza kila chozi, na kama atafanya hivyo hivi karibuni, hakutupatie tu tumaini la kweli kwa ajili ya wakati wenye kuja, lakini kunatusaidia pia tukuwe na maisha ya muzuri leo. Ndiyo, hata katika ulimwengu wenye kujaa mateso, namna Mungu anakuhangaikia kwa upendo, inaweza kukuletea faida.