Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari za hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Ikiwa ni hivyo, jaribu kujibu maulizo haya:

Tunaweza kufanya mambo gani ine ili kuimba muzuri zaidi?

Tunaweza kusimama na kuinua juu kitabu chetu cha nyimbo. Tunapaswa kupumua muzuri. Wakati tunafungua sana kinywa chetu, tunaweza kuimba kwa sauti kubwa.​—w17.11, uku. 5.

Ni mambo gani yenye yanatugusa moyo juu ya mahali kwenye miji ya makimbilio ilipatikana katika Israeli na barabara za kuenda katika miji hiyo?

Kulikuwa miji sita ya makimbilio mahali mbalimbali katika inchi, na kulikuwa barabara za muzuri za kuenda katika miji hiyo. Kwa hiyo, mutu angeweza kupata kimbilio haraka na kwa njia yenye kufaa.​—w17.11, uku. 14.

Sababu gani zawadi ya Mungu ya zabihu ya ukombozi kupitia Yesu ndiyo zawadi ya muzuri zaidi yenye tunaweza kupata?

Inatimiza tamaa yetu ya kuendelea kuishi na inatimiza uhitaji wetu wa kukombolea kutoka katika zambi na kifo. Kwa sababu anapenda wazao wa Adamu, Mungu alitoa Yesu kwa ajili yetu wakati tulikuwa tungali watenda zambi.​—wp17.6, uku. 6-7.

Namna gani andiko la Zaburi 118:22 lilionyesha mbele ya wakati kufufuliwa kwa Yesu?

Watu walikataa kuwa Yesu ni Masiya na wakamuua. Ili afikie kuwa ‘jiwe kubwa la pembeni,’ alipaswa kufufuliwa.​—w17.12, uku. 9-10.

Kizazi chenye kiliongoza kwa Masiya, kilipitishwa tu kupitia haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza?

Wakati fulani kizazi chenye kiliongoza kwa Yesu kilipitishwa kupitia muzaliwa wa kwanza, lakini haikukuwa hivyo sikuzote. Daudi hakukuwa muzaliwa wa kwanza wa Yese; lakini Masiya alitokea katika kizazi cha Daudi.​—w17.12, uku. 14-15.

Ni kanuni gani fulani za mambo ya matunzo zenye kupatikana katika Biblia?

Chini ya Sheria, watu wenye walikuwa na magonjwa fulani walitengwa ili wasikuwe pamoja na wengine. Watu walipaswa kunawa kisha kugusa maiti. Sheria iliomba mavi ya wanadamu izikwe. Watoto walipaswa kutahiriwa siku ya munane kisha kuzaliwa; ilikuwa muzuri kufanya hivyo kwa sababu ya uwezo wa damu wa kuganda.​—wp18.1, uku. 7.

Sababu gani haiko mubaya kwa Mukristo kujipenda kwa kadiri fulani?

Tunapaswa kupenda majirani wetu kama vile tunajipenda sisi wenyewe. (Mk. 12:31) Bwana wanapaswa ‘kuwapenda wake [ao, bibi] zao kama miili yao wenyewe.’ (Efe. 5:28) Lakini, kujipenda kunaweza kupita mipaka.​—w18.01, uku. 23.

Tunaweza kukamata hatua gani fulani ili kukomaa kiroho?

Tunapaswa kusoma Neno la Mungu, kutafakari juu ya Neno hilo, na kutumikisha mambo yenye tunajifunza. Tunapaswa pia kufanya akili yetu na moyo wetu vikuwe tayari kufuata muongozo wa roho takatifu na kukubali musaada wa wengine na kuwaonyesha shukrani.​—w18.02, uku. 26.

Sababu gani unajimu na kutabiri matukio haviwezi kutusaidia kujua wakati wenye kuja?

Kuko sababu nyingi, lakini sababu kubwa ni kwamba Biblia inakataza mazoea hayo yote.​—wp18.2, uku. 4-5.

Tunapaswa kuwa na mawazo gani juu ya kukubali mualiko kwa ajili ya chakula?

Ikiwa tunakubali mualiko, tunapaswa kujikaza kutimiza maneno yetu. (Zab. 15:4) Hatupaswe kuvunja mualiko bila sababu. Inawezekana kwamba mutu mwenye ametualika ametumika sana ili kutayarisha chakula.​—w18.03, uku. 18.

Namna gani ndugu wenye kuwa na madaraka wanaweza kumuiga Timotheo?

Timotheo alihangaikia sana watu na aliweka mahitaji yao ya kiroho pa nafasi ya kwanza. Alitumika kwa bidii katika utumishi mutakatifu na alitumikisha mambo yenye alijifunza. Aliendelea kujizoeza na kutegemea roho ya Yehova. Wazee wa kutaniko na watu wengine wanaweza kuiga mufano wake.​—w18.04, uku. 13-14.