Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Samaki-Kasuku—Anatengeneza Muchanga?

Samaki-Kasuku—Anatengeneza Muchanga?

NI NINI kinatengeneza muchanga? Muchanga unatengenezwa na vitu mbalimbali. Lakini kitu chenye kuzungumuziwa katika habari hii kinaweza kukushangaza. Ni samaki mwenye kusaga matumbawe (majiwe laini ya baharini yanayotokana na mukusanyo wa wanyama wadogo wa baharini) na kuigeuza kuwa muchanga. Samaki huyo anaitwa samaki-kasuku!

Samaki-kasuku wanaishi katika maji mbalimbali ya tropiki. Samaki hao wanameza matumbawe, wanatosha ndani sehemu ndogo-ndogo za kulisha mwili na kisha wanatosha inje sehemu yenye kubaki, ni sehemu hiyo ndio inakuwa muchanga. Ili kufanya kazi hiyo, samaki-kasuku anatumia taya (mâchoires) zake zenye nguvu kama mudomo wa ndege na meno yake ya nyuma yenye kuwa ngumu sana. Aina fulani za samaki-kasuku wanaweza kuishi kufikia miaka 20, bila meno yao kupoteza nguvu.

Katika maeneo fulani, samaki-kasuku anatafuna-tafuna matumbawe yaliyokufa na anatoa muchanga mwingi zaidi kuliko kitu kingine cha asili chenye kutengeneza muchanga. Wachunguzi fulani wanasema kuwa samaki-kasuku wa kawaida anatoa karibu kilo 100 za muchanga kwa mwaka.

Samaki-kasuku mweusi

Samaki-kasuku anafanya kazi ingine ya lazima. Wakati anakula-kula sana matumbawe, yenye kufunikwa na mimea ya baharini ao uchafu wa mimea, anafanya pia matumbawe yabakie safi. Kwa hiyo, namna ya kujilisha ya samaki-kasuku isiyokuwa ya kawaida inafanya mwamba wa tumbawe ubakie katika hali ya muzuri. Katika maji yenye haina samaki-kasuku na wanyama wengine wa baharini wenye kula mimea, mwamba wa tumbawe unajaa haraka magugu na mimea mingine ya baharini. Kitabu kimoja (Reef Life) kinaeleza kuwa “wachunguzi fulani wanasema kuwa miamba ya matumbawe ya leo haingekuwa namna iko kama hakungekuwa wanyama wa baharini wenye kula majani.”

Kazi hiyo yote wakati wa muchana inaomba kupumuzika muzuri wakati wa usiku. Samaki-kasuku anashangaza katika njia hiyo pia. Usiku ni wakati wa hatari sana kwenye mwamba wa tumbawe, kwa sababu kuna maadui wengi. Mara nyingi samaki-kasuku wanajificha chini ya mwamba wakati wanalala, lakini sikuzote hiyo haiko nafasi ya muzuri ya kuwalinda wasiliwe na samaki wenye njaa, kama vile papa (requins).

Ili kujilinda zaidi, samaki-kasuku fulani wanajifunika wakati wa usiku. Ili kujifunika, wanatoa katika mwili wao umaji-maji fulani wenye kufanana nguo ya kulala nayo yenye kupitisha mwangaza. Wanasayansi wenye kuchunguza viumbe wa baharini wanaamini kuwa umaji-maji huo wenye kunuka mubaya unawalinda na maadui wao.

Samaki-kasuku iko kati ya samaki wenye kuonekana na kuvutia zaidi kwenye mwamba wa tumbawe. Mara nyingi samaki-kasuku wa kiume na kike wanazaliwa na rangi za kuangara-angara. Rangi hizo zinabadilika wakati wanakomaa. Na jambo la muzuri zaidi ni hili: Samaki hao hawaogope watu katika maeneo kwenye watu hawawavue sana. Kwa hiyo, wako kati ya samaki ambao ni vyepesi kuangalia.

Kukaribia samaki-kasuku, kumuona na kumusikiliza wakati anakula kwenye tumbawe, ni jambo lenye wachunguzi wengi wa mwamba wa tumbawe hawatasahau. Wakati samaki-kasuku wanaonyesha uzuri wao, wanatunza mazingira yao ili ifurahishe viumbe wengine wenye kuishi kwenye mwamba wa tumbawe na hata sisi wanadamu.