Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Mungu Anatusaidia Kupona”

“Mungu Anatusaidia Kupona”

NATALYA na Aslan, mutoto wake mwenye miaka 9, walikaa karibu na Zarina na Anzhelika, mutoto wake mwenye miaka 12. Watoto na watu wakubwa wengine zaidi ya 1000 walikaa pamoja karibu nao; watu wenye kuwa na bunduki za hali ya juu walikuwa wanawachunga ili wasikimbie.

Asubuhi ya hiyo Siku ya 3, tarehe 1 Mwezi wa 9, 2004, watoto na wazazi walikuwa katika uwanja wa masomo wanajitayarisha ili kufurahia siku ya kwanza ya mwaka wa masomo huko Beslan, muji mudogo wa Alania, katika inchi ya Russie. Mara moja watu wenye walikuwa na bunduki na waliojifunga mabomu kwenye mwili waliingia ndani ya masomo; walikuwa wanapiga masasi juu na kulalamika. Washambuliaji hao zaidi ya 30 walikusanya watu hao wengi wenye woga katika chumba cha mazoezi cha masomo kisha waliweka mabomu kuwazunguka.

Hali ya Watu Waliokamatwa

Kwa siku tatu zenye wasiwasi, majeshi ya usalama na washambuliaji walipima kuzungumuza ili kufikia mapatano ao kusikilizana. Natalya, ambaye alikuwa anajifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova anakumbuka hivi: “Siku hiyo nilisali sana kuliko siku zingine zote.”

Ilikuwa wakati wa joto, na chumba hicho kilikuwa na joto sana. Kuanzia asubuhi ya siku iliyofuata, ni kusema Siku ya 4, washambuliaji hawakupatia watu hao chakula ao maji, na Siku ya 5, watu fulani walianza kunywa mikoyo na kula maua yenye watoto walikuwa wameletea walimu wao. Natalya anasema hivi: “Mutoto mumoja mwanaume mwenye alikuwa anakaa karibu nasi alitia jani katika mukono wangu. Nililikata katika vipande viwili, nikapatia Anzhelika kipande kimoja na Aslan kipande kingine.”

Siku ya 5, mapigano yalianza. Natalya anaeleza hivi: “Mabomu yenye kulipuka yalinitupa chini. Moshi mukubwa ulijaa katika hewa na masasi ilianza kupigwa.” Wakati majeshi ya serikali yalikuwa yanatupiana masasi na washambuliaji, Natalya na Aslan walitambaa na kutoroka. Mukaaji mumoja wa Ossetia anayeitwa Alan aliwakokota inje ya masomo na kuwatia mahali salama. Wengine wengi hawakuweza kutoroka.

Matokeo

Anzhelika alikufa wakati wa mapigano hayo

Watoto na watu wakubwa wengi walikufa; Anzhelika naye alikufa. Kwa majuma mengi, sauti za kilio na kuomboleza zilisikika katika muji wa Beslan. Nyumba ya Natalya iko karibu na masomo hiyo; na hata wakati masomo mupya ilijengwa karibu, Aslan hangeweza kuenda hapo peke yake. Hakuwa hata anatoka inje kucheza. Natalya anasema hivi: “Tulimuomba sana Yehova amusaidie kumaliza woga wake.” Kisha wakati fulani, alipata nguvu ya kuenda tena kwenye masomo.

Jambo ngumu kwa Natalya ilikuwa kufika kwenye mikutano ya Kikristo kwenye Jumba la Ufalme. Anasema hivi: “Kila mara wakati nilikuwa na watu wengi katika chumba kidogo, nilikuwa ninawaza kama chumba hicho kitashambuliwa. Nilikuwa ninasali ili kusitokee jambo lolote. Kisha wakati fulani niliacha kuenda kwenye mikutano. Nilisumbuka pia kujua kama sisi tulipona lakini watu wengi walikufa.”

Kupona

“Natalya anasema hivi: “Niko mwenye shukrani sana kwa ndugu na dada katika kutaniko wenye waliendelea kunisaidia. Shahidi mumoja anayeitwa Tatyana alikuwa ananitembelea kisha kila siku tatu. Kisha alikuja na Ulyana, Shahidi mwingine mupole, mwenye busara, na mwenye kusema kwa utulivu; alikuwa anajua muzuri Biblia. Alinishukuru kwa mambo yenye nilikuwa nimejikaza kufanya, na alisikiliza kabisa wakati nilikuwa ninaongea.

“Sasa ninaweza kueleza juu ya siku hiyo bila kuwa na uchungu ao woga”

“Ulyana alinisomea maneno ya mutume Mukristo Paulo yenye kupatikana katika andiko la 2 Wakorintho 1:9. Kisha kupambana na hali ngumu sana katika Asia, Paulo alisema hivi: ‘Tuliona ndani yetu wenyewe kwamba tumepokea hukumu ya kifo.’ Alinisomea pia andiko la Isaya 40:31: ‘Wale wanaomutumaini Yehova watapata nguvu mupya. Wataruka juu kwa mabawa kama tai.’ Maandiko kama hayo pamoja na musaada wenye Ulyana na wengine walikuwa wananitolea kila mara ili nikuwe na amani ya akili, vilinipatia nguvu ya kufika tena kwenye mikutano ya Kikristo pamoja na watoto wangu. Hata hivyo, ningali ninasikia wasiwasi wakati niko katika jumba.”

Kisha wakati fulani, Zarina alikuwa Shahidi wa Yehova. Anangojea kwa hamu kumupokea Anzhelika wakati wa ufufuo, ili aishi katika dunia yenye kupendeza, yenye amani na yenye itaongozwa na Ufalme wa Mungu. (Mathayo 6:9, 10; Matendo 24:15) Natalya na watoto wake walibatizwa katika mwaka wa 2009. Wangali wanaishi karibu na chumba hicho cha mazoezi chenye kubomoka, lakini hawaogope tena. Natalya anasema hivi: “Sasa ninaweza kueleza juu ya siku hiyo bila kuwa na uchungu ao woga. Mungu anatusaidia kupona.”