MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Wakati Mutoto Wako Anasema Uongo

Wakati Mutoto Wako Anasema Uongo

TATIZO

Mutoto wako wa miaka tano iko anachezea katika chumba kingine. Mara moja, unasikia kitu fulani kinaanguka. Unaenda haraka kwenye iko, unamuona anasimama pembeni ya sahani ya udongo yenye kupasuka. Sura yake inakuonyesha kwamba yeye ndiye aliangusha sahani hiyo.

Kwa ukali unamuuliza: “Ni weye uliangusha sahani hii?”

Mara moja anajibu, “hapana Mama, haiko miye!”

Haiko mara ya kwanza mutoto wako wa miaka tano anakudanganya waziwazi hivyo. Hilo litakuhangaisha?

MAMBO AMBAYO UNAPASWA KUJUA

Uongo wowote ni kosa. Biblia inasema kwamba Yehova Mungu anachukia ‘ulimi wa uongo.’ (Methali 6:16, 17) Sheria iliyopewa Israeli ilitoa malipizi makali kwa mutu anayedanganya mwengine.—Walawi 19:11, 12.

Lakini, uongo unatofautiana. Aina fulani za uongo ni hatari; zinasemwa ili kumuumiza mwengine. Aina zingine zinasemwa kwa kuwa hali inalazimisha kufanya hivyo, pengine ili kuepuka haya ao malipizi. (Mwanzo 18:12-15) Hata ikiwa uongo wote ni mubaya, aina fulani za uongo ni mubaya zaidi kuliko zengine. Ikiwa mutoto wako anasema uongo, fikiria miaka yake na kile kilimufanya asiseme kweli.

Unapaswa kumusaidia mutoto wakati angali mudogo. Dr. David Walsh anaandika hivi: “Kusema kweli, zaidi sana wakati ni vigumu kufanya hivyo, ni fundisho la maana kwa mutoto. Ili kuwa na uhusiano muzuri na wengine inaomba kuwa mwenye kutumainika, kusema uongo kunafanya watu wasikutumainie tena.” *

Hata hivyo, usiogope. Ikiwa mutoto wako anasema uongo hilo halimaanishe mara moja kama amekuwa mutu mubaya. Kumbuka kwamba Biblia inasema: ‘Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa mutoto.’ (Methali 22:15) Watoto fulani wanaonyesha ujinga huo kwa kusema uongo, pengine wanawaza kwamba ni njia nyepesi ya kuepuka malipizi. Kwa hiyo, ni lazima ufikirie namna utamusaidia.

 MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Tafuta kujua sababu gani mutoto wako anasema uongo. Je, anaogopa malipizi? Hataki kukukatisha tamaa? Ikiwa mutoto wako anatunga hadisi za uongo ili kufurahisha rafiki zake, je, anafanya hivyo sababu hajakomaa na hajajua tofauti kati ya mambo ya kweli na ya kuwazia? Ikiwa unajua sababu gani mutoto wako anasema uongo, utakuwa na nafasi nzuri ya kumusaidia.—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 13:11.

Wakati fulani, tumia misemwa kuliko kutumia maulizo. Katika mufano tuliozungumuzia mwanzoni mwa habari hii, mama, ambaye tayari alijua jambo lililotokea, kwa ukali alimuuliza mutoto wake: “Ni weye uliangusha sahani hii?” Pengine mutoto alisema uongo kwa sababu ya kuogopa hasira ya mama yake. Kuliko kumuuliza kwa ukali, wazia kama mama angesema tu: “Aah, umevunja sahani!” Kwa kutumia musemwa kuliko kutumia ulizo, mama hamushawishi mutoto kusema uongo, lakini anamusaidia mutoto aseme kweli.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:9.

Umusifu mutoto kwa kusema kweli. Kwa kawaida watoto wanatamani kuwafurahisha wazazi wao, kwa hiyo, tumia muelekeo huo kwa faida yako. Acha mutoto wako ajue kama ni jambo la maana kusema kweli katika familia, na kwa hiyo unataka awe musema kweli.— Kanuni ya Biblia: Waebrania 13:18.

Umuonyeshe waziwazi kwamba kusema uongo kunafanya mutu asitumainiwe na kwamba ikiwa hawakutumainie, inaomba wakati murefu ili waanze kukutumainia tena. Uwe na zoezi la kumusifu mutoto wako wakati anasema kweli. Kwa mufano, unaweza kusema, “Unanifurahisha wakati unasema kweli.”

Uwe mufano muzuri. Ni wazi kwamba, hauwezi kutazamia mutoto wako aseme kweli ikiwa anakusikiliza ukisema mambo kama vile: “Umuambie kama siko nyumbani” wakati haupendi kuzungumuza na mutu kwenye telephone ao “sikutoka nyumbani leo kwa sababu niko mugonjwa,” lakini ukweli ni kwamba unataka tu kupumuzika.—Kanuni ya Biblia: Yakobo 3:17.

Tumia Biblia. Kanuni za Biblia na habari za watu wanaozungumuziwa ndani zinachochea mutu kusema kweli. Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mukuu, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, kinaweza kukusaidia kufundisha mutoto kanuni za Biblia. Sura 22 ina kichwa,“Kwa Nini Haupaswi Kusema Uongo?” (Soma maelezo fulani ya kitabu hicho katika kisanduku “Kitabu cha Kusaidia Mutoto Wako.”)

^ fu. 11 Ilichukuliwa katika kitabu No: Why Kids—of All Ages—Need to Hear It and Ways Parents Can Say It.