Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO

Mukazo Ni Nini?

Mukazo Ni Nini?

Mukazo ni namna mwili wetu unatenda wakati tuko mbele ya hali ngumu. Ubongo wako unatuma hormone mingi katika sehemu zote za mwili. Hormone hizo zinafanya moyo uanze kupiga mbiombio, zinabadilisha mwendo wa damu, zinapanua ao kufinya mapafu (mafafa), na zinakaza misuli yako. Mbele utambue kabisa jambo lenye kutendeka, mwili wako uko tayari kwa ajili ya kutenda. Wakati hali fulani yenye kuleta mahangaiko inamalizika, “mushtuko” unamalizika na mwili unarudia tena mu hali ya kawaida.

MUKAZO WA MUZURI NA WA MUBAYA

Mukazo ni uwezo wa kawaida wenye unatusaidia kupambana na tatizo ao hatari fulani. Hali hiyo inaanzia katika ubongo wetu. Mukazo wa muzuri unatusaidia tutende haraka. Kiasi fulani cha mukazo kinaweza kutusaidia kufikia miradi yetu ao kupata matokeo ya muzuri, pengine wakati wa mashindano ku masomo, wakati tunaulizwa maulizo kuhusu kazi, ao wakati wa muchezo fulani.

Lakini, mukazo wenye kuendelea, wenye kuvuka mipaka, ao wenye kukawia unaweza kukuletea matokeo ya mubaya. Wakati unajikuta kila mara katika mukazo ao uko na mukazo wenye kuendelea unaweza kuanza kuteseka kimwili, kihisia, na kiakili. Tabia yako, kutia ndani namna unatendea wengine vinaweza kubadilika. Mukazo wenye kuendelea unaweza pia kufanya mutu aanze kunywa pombe kupita kiasi, kutumia dawa za kulewesha na kufanya mambo ingine yenye haifae ili kujaribu kumaliza mukazo. Mukazo unaweza hata kukufanya ushuke moyo, uchoke kimwili na kiakili, ao kukufanya ukuwe na mawazo ya kujiua.

Hata kama mukazo hauwezi kuwa na matokeo ileile kwa kila mutu, unaweza kuleta magonjwa mingi. Na mukazo unaweza kugusa karibu kila sehemu ya mwili.